Mentor
JF-Expert Member
- Oct 14, 2008
- 20,328
- 23,879
FlasMwenzenu yamenikuta, yaloukuta mtete
nilijiona ukuta, yasingenifika mentor
kaniona wa kupita, nimebaki hali tete
sijui nipigane, au kipepeo nimuache.
Labda nianze hivi...
"I wanna be with you.
I want us to make it work.
I dont know how, but we can try.
Am saying yes, Mentor.
I wanna be ur gal & only urs.
Bt u also have to promise to love me only.
I really do love you..."
disemba mbili na kumi, aliutuma ujumbe
masomo nilimaliza sasa narudi nyumbani
kamuaga wangu hani japo tutakuwa mbali
penzi silibadili siku moja tule wali.
Na machozi akalia nami kaona huruma
kweli mi nilimpenda ukweli siezi ficha
nikajua tamuoa ndani awe wangu mke
sijui nipigane, au kipepeo nimuache!
Flash back...
ilikuwa septemba nilimuona mrembo
marafiki si tukawa tukazidisha upendo
mcheshi, mzuri moyo, msafi dharau kando
kaniteka taratibu kwake nikashindwa toka.
nikaufungua moyo yote nikamueleza
pengi nimeshajaribu kaishia kuteleza
kwake sitaki sababu nitapigana kupata
sijui mi nipigane, au kipepeo nimuache!
naye akanieleza, alivyonipenda tangu
alikuwa kwa gereza, tena amefungwa pingu
nikaja nikalegeza, moyo wake kauteka
kaniahidi upendo, na vyote vitavyopatika.
fast forward....
september
october
november
december
january
february
march
april
may
june
july...
wiki ya jana...
simu nampigia mwenzangu hakupokea
nikapatwa na simanzi nini kimemtokea
kauliza marafiki wote wakanigomea
moyo ukanisinyaa kuwaza lilotukia.
ghafla kapata ujumbe ulonitatiza moyo...
"I hate that I have to do this bcz i know ur genuine with me.
Im sory.
But u and I cant be!"
Paa!
ni kama vile gobole limepiga moyo wangu
sikuyaamini macho limenitokea kwangu
sababu hataki nipa yote imekula kwangu
sijui nipiganie, au kipepeo nimuache!
Wahenga walishasema ukipendacho pigana
kwani si ndo walifanya Romeo na julieta
Julius Kaisari na kaka Valentino
wengine nimesahau ila nataka wafuata.
Wahenga tena wakanena ukipendacho kiache
kama chako kitarudi si chako kitapepea
mapenzi kama kipepeo ukifuata charuka
sijui nipiganie, au kipepeo nimuache!
Hilo ndo langu tatizo kwani bado nampenda
nimuache bila vita taonekana mnyonge
ila nitapopigana na hakuwa wangu kweli
mwisho itakula kwangu na pweke nijibakie.
GENUINE:
nini alimaanisha ati mimi kwake genuine
kwani alitaka feki bado sijamuelewa
ama yeye ndiye feki kwangu asingeliweza
sijui nipiganie au kipepeo nimuache!
Jana usiku manane, tanesco weshaniudhi
nikapokea mwingine, ujumbe kanitumia...
"I blv ur a truly genuine guy
& the last thing i wanna do is is hurt ur filingz.
U deserve beta than that.I'm seeing another guy
been wit him a month noW!"
Sikulihitaji hili na sidhani ni faraja
nilimkosea nini au umbali ndo shida
lakini tuliafiki kupendana bila hoja
kweli umeniumiza, na moyo kanipondea.
swali moja nauliza na hili nataka jibu
wakati upi wakuacha na upi wa kupigana
niendelee shikilia ama kamba niachie
sijui nipiganie au kipepeo nimuache!
nilijiona ukuta, yasingenifika mentor
kaniona wa kupita, nimebaki hali tete
sijui nipigane, au kipepeo nimuache.
Labda nianze hivi...
"I wanna be with you.
I want us to make it work.
I dont know how, but we can try.
Am saying yes, Mentor.
I wanna be ur gal & only urs.
Bt u also have to promise to love me only.
I really do love you..."
disemba mbili na kumi, aliutuma ujumbe
masomo nilimaliza sasa narudi nyumbani
kamuaga wangu hani japo tutakuwa mbali
penzi silibadili siku moja tule wali.
Na machozi akalia nami kaona huruma
kweli mi nilimpenda ukweli siezi ficha
nikajua tamuoa ndani awe wangu mke
sijui nipigane, au kipepeo nimuache!
Flash back...
ilikuwa septemba nilimuona mrembo
marafiki si tukawa tukazidisha upendo
mcheshi, mzuri moyo, msafi dharau kando
kaniteka taratibu kwake nikashindwa toka.
nikaufungua moyo yote nikamueleza
pengi nimeshajaribu kaishia kuteleza
kwake sitaki sababu nitapigana kupata
sijui mi nipigane, au kipepeo nimuache!
naye akanieleza, alivyonipenda tangu
alikuwa kwa gereza, tena amefungwa pingu
nikaja nikalegeza, moyo wake kauteka
kaniahidi upendo, na vyote vitavyopatika.
fast forward....
september
october
november
december
january
february
march
april
may
june
july...
wiki ya jana...
simu nampigia mwenzangu hakupokea
nikapatwa na simanzi nini kimemtokea
kauliza marafiki wote wakanigomea
moyo ukanisinyaa kuwaza lilotukia.
ghafla kapata ujumbe ulonitatiza moyo...
"I hate that I have to do this bcz i know ur genuine with me.
Im sory.
But u and I cant be!"
Paa!
ni kama vile gobole limepiga moyo wangu
sikuyaamini macho limenitokea kwangu
sababu hataki nipa yote imekula kwangu
sijui nipiganie, au kipepeo nimuache!
Wahenga walishasema ukipendacho pigana
kwani si ndo walifanya Romeo na julieta
Julius Kaisari na kaka Valentino
wengine nimesahau ila nataka wafuata.
Wahenga tena wakanena ukipendacho kiache
kama chako kitarudi si chako kitapepea
mapenzi kama kipepeo ukifuata charuka
sijui nipiganie, au kipepeo nimuache!
Hilo ndo langu tatizo kwani bado nampenda
nimuache bila vita taonekana mnyonge
ila nitapopigana na hakuwa wangu kweli
mwisho itakula kwangu na pweke nijibakie.
GENUINE:
nini alimaanisha ati mimi kwake genuine
kwani alitaka feki bado sijamuelewa
ama yeye ndiye feki kwangu asingeliweza
sijui nipiganie au kipepeo nimuache!
Jana usiku manane, tanesco weshaniudhi
nikapokea mwingine, ujumbe kanitumia...
"I blv ur a truly genuine guy
& the last thing i wanna do is is hurt ur filingz.
U deserve beta than that.I'm seeing another guy
been wit him a month noW!"
Sikulihitaji hili na sidhani ni faraja
nilimkosea nini au umbali ndo shida
lakini tuliafiki kupendana bila hoja
kweli umeniumiza, na moyo kanipondea.
swali moja nauliza na hili nataka jibu
wakati upi wakuacha na upi wa kupigana
niendelee shikilia ama kamba niachie
sijui nipiganie au kipepeo nimuache!