Wakati Tanzania "imekaza" nati kwa wawekezaji wa Migodi, gesi na masuala mengine,inataka Uganda ilegeze kwa wawekezaji wa mafuta

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
11,983
20,633
Ama kweli duniani kuna mambo!

Tanzania kwa muda sasa imekuwa ikikabana koo na wawekezaji wa gesi, migodi ya dhahabu na wengine ikiwadai kodi!

Maelfu wamefilisiwa kwa sababu ya kodi!

Leo tunawashauri Uganda wasamehe kodi katika mafuta na bomba la mafuta!

Uganda lazima iangalie maslahi yake, mafuta sio mchicha kwamba utaota,tuwaache wajipange katika mambo ambayo yataangazia maslahi yao!

Sisi hatuna hasara, kwetu linapita bomba tu!
 
Nimeona mheshimiwa Rais JPM kamshauri M7 kwa kusema kwamba apoteze kidogo ili baadaye apate zaidi. Amesema kwamba bomba likianza kazi Uganda itaongeza makusanyo na kuwa nchi ya kwanza Afrika kwa uchumi, au sijasikia vizuri! Nimeyakumbuka maneno ya JK kwamba ukitaka kula na wewe kubali kuliwa japo kidogo! Uganda kama wamekaza basi walegeze watu wapate ajira. Mbona nasikia Tanzania imelegeza sana kwenye huo mradi kwa nini na wao wasilegeze.
 
Back
Top Bottom