Wakati taifa likikabiliwa na njaa na mafuriko wasomi wetu wanagomea chakula!

Omuregi Wasu

JF-Expert Member
May 21, 2009
749
148
Wanafunzi Muhimbili wagomea chakula




Na Hellen Mwango



10th January 2010


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa



comment_bubble.png

Maoni





Wanafunzi wa Taasisi ya Vyuo Shirikishi Muhimbili (Muhas) wamefanya mgomo wa kula wakipinga hatua ya kubadilishiwa ratiba ya chakula ikiwemo kukosa kuku, mayai na matunda.
Hatua hiyo ilifikiwa juzi baada ya wanafuzi hao kukuta ratiba mpya ya chakula ikiwa imebandikwa katika bwalo lao chakula.
Mgomo huo ulianza juzi usiku baada ya wanafunzi hao kuingia bwaloni mwao na kukuta wamepikiwa ugali na maharage badala ya wali na nyama kama ratiba ya awali ilivyokuwa inatakiwa.
Akiongea na Nipashe Jumapili Rais wa taasisi hiyo, Richard Molega, alisema wamechoshwa na matukio ya kubadilishiwa chakula tangu Oktoba 12, mwaka jana.
Molega alisema walipofungua chuo mwaka jana ratiba ya chakula ilibadilika ambapo waliondoa kuku, maziwa, mayai, matunda na nyama kutoka mara tatu kwa wiki na kubaki mara mbili.
Alisema walipohoji kubadilishwa kwa ratiba hiyo hawakupatiwa ufafanuzi wala maelezo yoyote hali iliyosababisha wajilazimishe kula chakula hicho pasipokujua hatima ya ratiba hiyo mpya.
"Hata hivyo tulisikia Rais Jakaya Kikwete anakuja kufungua jengo hapa Muhimbili tukauambia uongozi wa hospitali kama hawatabadilisha ratiba ya chakula tutagoma kula na kumfikishia malalamiko yetu mheshimiwa rais," alisema.
Aliongeza kuwa uongozi ulibadilisha ratiba halisi ya chakula ikiwa ni kuku, maziwa, mayai, matunda na nyama kama ilivyopangwa.
"Tumeshangaa jana (juzi) jioni kukuta imebandikwa ratiba ambayo inaonyesha kupunguzwa baadhi ya vyakula kama kuku, maziwa, mayai, na nyama kwa hiyo tumegoma kula kama ilivyo kawaida mtu akiwa na njaa hawezi kufanyakazi wala kusoma hata darasani itakuwa sio rahisi kuingia kama hakutakuwa na ufumbuzi," alisema Molega.
Aliongeza kuwa ratiba hiyo iliyoonyesha mabadiliko ya chakula haina mhuri wala sahihi ya mtu aliyeitoa hali inayiowapa mashaka kufanyiwa mambo kienyeji.
Naye Kaimu Mkrugenzi wa Taasisi Lalison Ndolele aliwasihi wanafunzi hao kula chakula kilichopo ili ifikapo kesho suala lao lizungumzwe na kufanyiwa kazi.
Ndolele alikiri kuwapo kwa mabadiliko ya ratiba ya chakula hali inayosababishwa na mabadiliko ya mfumo wa bei za vyakula kwa sasa.
"Mimi nawasihi kuleni chakula kilichopo ili kesho (Jumatatu) tukae chini kuliongelea suala lenu na hali itakuwa nzuri tafadhali," alisema.
Hata hivyo bila kutarajia wanafunzi hao walisikika wakipaza sauti na kusema "Hatuli chakula hadi kieleweke tutaendelea kugoma."
"Mimi sina la kusema kama mnaendelea kugoma sawa lakini wale ambao wataona sio vyema kugoma nawasihi wale chakula kilichopo," alisema Mkurugenzi huyo.
Wanafunzi waliofanya mgomo huo ni zaidi ya 600 na kwamba hadi Nipashe Jumapili inaondoka bwaloni hapo ilishuhudia masufuria ya vyakula yakiwa yamejaa vyakula .



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Mafuriko yanahusiana vipi na watu kulishwa ugali na maharage
bila ridhaa yao??????????????
 
hivi kumbe vyuo vikuu vya bongo wanapikiwa/ wanapewa msosi?..raha ilioje. ningejua ningesoma bongo
 
hivi kumbe vyuo vikuu vya bongo wanapikiwa/ wanapewa msosi?..raha ilioje. ningejua ningesoma bongo

Umeambiwa ni vyuo vingapi wanapikiwa??? Kumbuka Muhimbili ni chuo cha udaktari so huwa kuna baadhi ya mambo bado yanaendeshwa na utawala kama kuwapatia chakula badala ya pesa.

Halafu kupikiwa siyo raha ndo maana unaona wanagoma......wangepewa pesa za mkopo usinge sikia mtu anagoma.
 
Wanafunzi Muhimbili wagomea chakula




Na Hellen Mwango



10th January 2010


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa



comment_bubble.png

Maoni





Wanafunzi wa Taasisi ya Vyuo Shirikishi Muhimbili (Muhas) wamefanya mgomo wa kula wakipinga hatua ya kubadilishiwa ratiba ya chakula ikiwemo kukosa kuku, mayai na matunda.
Hatua hiyo ilifikiwa juzi baada ya wanafuzi hao kukuta ratiba mpya ya chakula ikiwa imebandikwa katika bwalo lao chakula.
Mgomo huo ulianza juzi usiku baada ya wanafunzi hao kuingia bwaloni mwao na kukuta wamepikiwa ugali na maharage badala ya wali na nyama kama ratiba ya awali ilivyokuwa inatakiwa.
Akiongea na Nipashe Jumapili Rais wa taasisi hiyo, Richard Molega, alisema wamechoshwa na matukio ya kubadilishiwa chakula tangu Oktoba 12, mwaka jana.
Molega alisema walipofungua chuo mwaka jana ratiba ya chakula ilibadilika ambapo waliondoa kuku, maziwa, mayai, matunda na nyama kutoka mara tatu kwa wiki na kubaki mara mbili.
Alisema walipohoji kubadilishwa kwa ratiba hiyo hawakupatiwa ufafanuzi wala maelezo yoyote hali iliyosababisha wajilazimishe kula chakula hicho pasipokujua hatima ya ratiba hiyo mpya.
"Hata hivyo tulisikia Rais Jakaya Kikwete anakuja kufungua jengo hapa Muhimbili tukauambia uongozi wa hospitali kama hawatabadilisha ratiba ya chakula tutagoma kula na kumfikishia malalamiko yetu mheshimiwa rais," alisema.
Aliongeza kuwa uongozi ulibadilisha ratiba halisi ya chakula ikiwa ni kuku, maziwa, mayai, matunda na nyama kama ilivyopangwa.
"Tumeshangaa jana (juzi) jioni kukuta imebandikwa ratiba ambayo inaonyesha kupunguzwa baadhi ya vyakula kama kuku, maziwa, mayai, na nyama kwa hiyo tumegoma kula kama ilivyo kawaida mtu akiwa na njaa hawezi kufanyakazi wala kusoma hata darasani itakuwa sio rahisi kuingia kama hakutakuwa na ufumbuzi," alisema Molega.
Aliongeza kuwa ratiba hiyo iliyoonyesha mabadiliko ya chakula haina mhuri wala sahihi ya mtu aliyeitoa hali inayiowapa mashaka kufanyiwa mambo kienyeji.
Naye Kaimu Mkrugenzi wa Taasisi Lalison Ndolele aliwasihi wanafunzi hao kula chakula kilichopo ili ifikapo kesho suala lao lizungumzwe na kufanyiwa kazi.
Ndolele alikiri kuwapo kwa mabadiliko ya ratiba ya chakula hali inayosababishwa na mabadiliko ya mfumo wa bei za vyakula kwa sasa.
"Mimi nawasihi kuleni chakula kilichopo ili kesho (Jumatatu) tukae chini kuliongelea suala lenu na hali itakuwa nzuri tafadhali," alisema.
Hata hivyo bila kutarajia wanafunzi hao walisikika wakipaza sauti na kusema "Hatuli chakula hadi kieleweke tutaendelea kugoma."
"Mimi sina la kusema kama mnaendelea kugoma sawa lakini wale ambao wataona sio vyema kugoma nawasihi wale chakula kilichopo," alisema Mkurugenzi huyo.
Wanafunzi waliofanya mgomo huo ni zaidi ya 600 na kwamba hadi Nipashe Jumapili inaondoka bwaloni hapo ilishuhudia masufuria ya vyakula yakiwa yamejaa vyakula .



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Mtoa hoja unamawazo ya karne ya 17.........kwa kuwa kuna mafuriko basi mambo mengine ysiendelee.......watu wasi dai haki zao???
 
Back
Top Bottom