Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,415
RAIS wa Kenya Uhuru Kenyatta amewasili Rwanda kwa ziara ya kikazi na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Rwanda Dkt. Richard Sezibera mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kigali.
Mara baada ya kupokelewa Rais Kenyatta alijkwenda katika chuo cha mafunzo ya Kijeshi cha Gabiro, wilayani Gastibo ambako alikutana na Rais wa Rwanda Paul Kagame.
Kagame pamoja na maafisa wa serikali kuu wa ngazi za juu na sekta binafsi na mashirika binafsi wanakutana Gabiro Ijumaa kwa ajili ya mkutano wa kitaifa wa viongozi (Umwiherero).
Akiwa nchini humo, Kenyatta anatarajiwa kufanya mazungumzo na Rais Paul Kagame.
Kenya ni mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo inaongozwa na Rais Kagame.
Nchi mbili hizo zinamahusiano ya karibu katika Nyanja mbalimbali zikiwemo biashara, usalama, kujenga uwezo na uwekezaji miongoni mwa mengine.
Kwa mara ya mwisho, Rais Kenyatta aliwasili Rwanda mapema mwaka jana wakati wa mkutano wa wakuu wa Umoja wa Afrika.
https://zanzibarleo.co.tz/2019/03/11/kenyatta-ziarani-rwanda/
Mara baada ya kupokelewa Rais Kenyatta alijkwenda katika chuo cha mafunzo ya Kijeshi cha Gabiro, wilayani Gastibo ambako alikutana na Rais wa Rwanda Paul Kagame.
Kagame pamoja na maafisa wa serikali kuu wa ngazi za juu na sekta binafsi na mashirika binafsi wanakutana Gabiro Ijumaa kwa ajili ya mkutano wa kitaifa wa viongozi (Umwiherero).
Akiwa nchini humo, Kenyatta anatarajiwa kufanya mazungumzo na Rais Paul Kagame.
Kenya ni mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo inaongozwa na Rais Kagame.
Nchi mbili hizo zinamahusiano ya karibu katika Nyanja mbalimbali zikiwemo biashara, usalama, kujenga uwezo na uwekezaji miongoni mwa mengine.
Kwa mara ya mwisho, Rais Kenyatta aliwasili Rwanda mapema mwaka jana wakati wa mkutano wa wakuu wa Umoja wa Afrika.
https://zanzibarleo.co.tz/2019/03/11/kenyatta-ziarani-rwanda/