Bowie
JF-Expert Member
- Sep 17, 2016
- 4,372
- 6,078
Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee ameendesha kwa kasi kampeni zake za kusaka kura kwa ajili ya uchaguzi wa marudio utakaofanyika tarehe 26 October 2017.
Chama cha Jubilee kimejizatiti kutaka kuungwa mkono katika ngome za chama cha upinzani NASA huko Magharibi ya Kenya, kwasasa chama hicho kinauhakika kupata kura za uhakika kutoka bonde la ufa na mkoa wa kati ambayo ina wapiga kura wengi zaidi. Jubilee kwa kutumia wabunge, masenate na magavana walio wengi bungeni wamejipanga kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo.
Chama cha NASA chini ya Raila Odinga hakifanyi kampeni ipasavyo na imekuwa ni chama cha kulalamika na migomo, hali ya kifedha ya chama hicho nalo limekuwa tatizo katika kuendesha kampeni hizo. Jubilee wameweka mikakati mikubwa kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo.
Chama cha Jubilee kimejizatiti kutaka kuungwa mkono katika ngome za chama cha upinzani NASA huko Magharibi ya Kenya, kwasasa chama hicho kinauhakika kupata kura za uhakika kutoka bonde la ufa na mkoa wa kati ambayo ina wapiga kura wengi zaidi. Jubilee kwa kutumia wabunge, masenate na magavana walio wengi bungeni wamejipanga kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo.
Chama cha NASA chini ya Raila Odinga hakifanyi kampeni ipasavyo na imekuwa ni chama cha kulalamika na migomo, hali ya kifedha ya chama hicho nalo limekuwa tatizo katika kuendesha kampeni hizo. Jubilee wameweka mikakati mikubwa kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo.