Wakati Nchimbi akiwa Butiama kuadhimisha miaka 50 ya uhuru huku nyuma....

COMPLICATOR2011

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
254
35
Nimeona wafanyakazi wa wizara ya habari, utamaduni na michezo wakifukuzwa kwenye nyumba (ofisi) walizopanga mali ya NHC iliyo chini ya wizara ya nyumba kwa madai ya kutolipa kodi hali ambayo imepelekea deni kufika mil391. Wakati hayo yakijiri jijini Dar waziri mwenye dhamana na wizara hii alikuwa akitafuna fedha za walalahoi kwa kuzindua maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Sasa kama serikali ya magamba wanashindwa kulipa kodi za pango je cc wananchi tutaishi maisha gani?
 
Taarifa ya habari TBC1 wafanyakazi wa wizara ya vijana, habari , utamaduni na michezo leo wamejikuta wakitolewa nje ya ofisi zao na mafaili ya serikali kuzagaa kila kona kwa kile kinachosemekana ni udeni sugu wa mil391 wizara ya nyumba na makazi.
My take: kuna umhimu gani wa kuadhimisha uhuru wakati....
Mkuu kama hawalipi wakati kila mwaka budget ya pango huwa inatengwa basi wafukuzwe ili iwe mfano kwao na wengine wenye tabia kama hiyo. Nimesikia watu wa NHC wanasema wameanza na watoto yaani Idara ya Habari na wataendelea na kuwatoa kwenye nyumba zao wale wote ambao hawajalipa pango ikiwemo Wizara yenyewe ya Habari na Utamaduni! Tusubiri tuone siku ambayo vifaa vya Waziri Nchimbi vitakapokuwa vinatolewa nje!
 
Wanataka kumlipa dowans harakaharaka kwa kuwa ni mgao wao huku Serikali inashindwa kulipa kodi ? Kweli nimeshangaa sana jambo .Bajeti yake iko wapi hadi zinafikia 300mn ?
 
Waziri wa habari Nchimbi ile kesi ya kukimbia na sanduku la kura kisha kweda kujifuta aibu kwenye vyombo vya habari imeishia wapi? Ana ubavu wa kupindisha ukweli ulioanikwa na vyombo vya habari wakati hata madiwani wa CCM wenyewe wanagomea kumtambua huyo meya?
 
Naona Tanzania tunayoihitaji ndio tunakoelekea kama watu wanapewa pesa ya kodi na wanaweka kwenye mifuko yao shirika la nyumba litaendeleaji nmeifurahia saana hiyo hali leo ni mfano mzuri.Big up saana msimamizi wa zoezi hilo please usiteteleke Mkuu
 
10_11_hhu58m.jpg


SDC10003.JPG
SDC10005.JPG

SDC10018.JPG

Baazi ya wapagazi wakiwa wamesimama kidogo katika zoezi linaloendelea la kutoa vitendea kazi vya
MAELEZO Dar es Salaam leo zoezi ambalo linaendeshwa na NHC la kuwatoa kwa nguvu wadeni wao.


IKIWA ni katika muendelezo wa kukusanya madeni na kuwatoa wadeni wake Shirika la Nyumba (NHC)leo asubuhi rungu lao lilitua katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) ambapo wafanyakazi wake wamejikuta wakilazimika kutoka nje kutokana na kudaiwa kodi ya miezi saba ambayo ni kiasi cha sh.mil.47 Ilifahamika kuwa Kodi ya mwezi waliyotakiwa kulipa ni sh.mil7,149,000.Kabla ya MAELEZO kupatwa na kadhia hiyo NHC walianza katika ofisi ya Utamaduni ambako wanadaiwa sh mil87


 
Nimeona wafanyakazi wa wizara ya habari, utamaduni na michezo wakifukuzwa kwenye nyumba (ofisi) walizopanga mali ya NHC iliyo chini ya wizara ya nyumba kwa madai ya kutolipa kodi hali ambayo imepelekea deni kufika mil391. Wakati hayo yakijiri jijini Dar waziri mwenye dhamana na wizara hii alikuwa akitafuna fedha za walalahoi kwa kuzindua maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Sasa kama serikali ya magamba wanashindwa kulipa kodi za pango je cc wananchi tutaishi maisha gani?

Did you expect him to skip the fete because NHC were going to evict the Ministry? Kwanza deni hili lina miaka kadhaa toka kabla hata ya yeye kuja hapo wizarani.
 
Jambo hili limefikia wapi Mhe Tundu Lissu. CHADEMA inashambuliwa kushoto kulia na BAKWATA, CCM, na waheshimiwa Mafisadi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom