COMPLICATOR2011
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 254
- 35
Nimeona wafanyakazi wa wizara ya habari, utamaduni na michezo wakifukuzwa kwenye nyumba (ofisi) walizopanga mali ya NHC iliyo chini ya wizara ya nyumba kwa madai ya kutolipa kodi hali ambayo imepelekea deni kufika mil391. Wakati hayo yakijiri jijini Dar waziri mwenye dhamana na wizara hii alikuwa akitafuna fedha za walalahoi kwa kuzindua maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Sasa kama serikali ya magamba wanashindwa kulipa kodi za pango je cc wananchi tutaishi maisha gani?