Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania imewatangazia kuanzia kesho Alhamisi bodaboda na bajaji zote hazitaruhusiwa kuingia katikati ya Jiji hilo.
=================
TAARIFA HII IMEKANUSHWA
DAR: BODABODA WAPEWA VITUO 9 MJINI
Baada ya kudaiwa bodaboda na Bajaji za biashara zimezuiwa kuingia Mjini Jijini Dar es Salaam, mamlaka zimekanusha zuio hilo na kuelezea kuna vituo 9 vimetengwa maalum kwa vyombo hivyo, mchakato ukishirikisha viongozi wa Bodaboda, TARURA, Jiji, Polisi na LATRA.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng`wilabuzu Ndatwa Ludigija amesema kuwa utaratibu wa vituo hivyo utawapa urahisi wa kushusha na kupakia abiria na siyo vituo holela kama ilivyokuwa awali.
Aidha, Msemaji wa Shirikisho la Vyama vya Madereva Pikipiki Mkoa wa Dar, Tito Lazaro amesema: “Utaratibu huo utapunguza uhalifu kwa kuwa kuna wasimamizi, mavazi maalum ya madereva, madereva watawasilisha nyaraka za utambulisho.
“Vituo hivyo ni Nasra Tower (Kariakoo), Sabasaba (Msimbazi), JK Park (Mnazi Mmoja), Fire, Mindu & Maliki (Upanda), Suwata (Kariakoo), Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mnazi Mmoja na Kongo (Kariakoo).”
=================
TAARIFA HII IMEKANUSHWA
DAR: BODABODA WAPEWA VITUO 9 MJINI
Baada ya kudaiwa bodaboda na Bajaji za biashara zimezuiwa kuingia Mjini Jijini Dar es Salaam, mamlaka zimekanusha zuio hilo na kuelezea kuna vituo 9 vimetengwa maalum kwa vyombo hivyo, mchakato ukishirikisha viongozi wa Bodaboda, TARURA, Jiji, Polisi na LATRA.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng`wilabuzu Ndatwa Ludigija amesema kuwa utaratibu wa vituo hivyo utawapa urahisi wa kushusha na kupakia abiria na siyo vituo holela kama ilivyokuwa awali.
Aidha, Msemaji wa Shirikisho la Vyama vya Madereva Pikipiki Mkoa wa Dar, Tito Lazaro amesema: “Utaratibu huo utapunguza uhalifu kwa kuwa kuna wasimamizi, mavazi maalum ya madereva, madereva watawasilisha nyaraka za utambulisho.
“Vituo hivyo ni Nasra Tower (Kariakoo), Sabasaba (Msimbazi), JK Park (Mnazi Mmoja), Fire, Mindu & Maliki (Upanda), Suwata (Kariakoo), Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mnazi Mmoja na Kongo (Kariakoo).”