Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Kizazi kipya wamekuwa wakijidhalilisha na kuthibitisha hawana mikakati ya kujitegema kiuchumi na ndiyo maana hujisalimisha kwa wanasiasa hususani wa CCM katika kipindi cha kampeni.
Huko huambulia makombo tu. Angalia mwanadada mmoja iliripotiwa ndani ya jamvi hili kuwa aliachwa kwenye msafara wa JK huko Singida na ikabidi ajikodishie pikipiki imrudishe kule alikofikia. Wanamuziki wa kizazi kipya wamejikuta katika hali mbaya kifedha kiasi kwamba wanasiasa huwatumia na baadaye kuwatelekeza.
Mfano katika mkutano mkuu wa CCM wa mwaka 2007 uliomtawaza JK kuwa Mwenyekiti wa CCM, JK aliwaumbua wanamuziki hao baada ya matumbuizo yao pale aliposema......" Hawa tulikuwa nao na tuliwatumia katika kampeni zetu za 2005.."
Ungelitegemea basi baada ya kauli ya bosi huyo wa CCM, kizazi kipya wangelijifunza na kuachana na tabia hiyo ya kujidhalilisha kwenye kampeni za CCM ambako uchunguzi wangu umebaini malipo wanayolipwa ni kiduchu sana.
Lakini mwanamuziki wa kwaya ya dini au "gospel" mwanamama Rose Mhando amewaonyesha njia kizazi kipya kwani huko Kenya ameingia mkataba mnono na Safaricom na nyimbo zake sasa zinatumika katika mtandao huo naye hulipwa pesa kibao.
Mfano wimbo wake wa "Nibebe" sasa unamwingizia zaidi ya Tshs 16 Milioni kwa mwezi au Kshs 800, 000/= kwa Exchange rate of one Kshs for 20 Tshs.
Kwa kitega uchumi kama hicho Rose Mhando anapata zaidi ya Tshs 152 Milioni kwa mwaka kwa wimbo mmoja tu. Na anazo nyimbo nyingi kwenye mtandao wa Safaricom na hivi sasa ana matamasha mengi huko Kenya kutangaza nyimbo zake ili watumiaji wa mtandao wa safaricom waweze kuwa wanazitumia kwenye milio ya sauti ya simu zao.
Sidhani hata kampeni ikiendelea kwa miaka kumi ijayo kama kizazi kipya kilichojisalimisha kwa wanasiasa wetu wa CCM kitakaa kiweze kupambana na mapato ya gwiji huyu wa miziki ya kidini.
Ushauri wangu ni kuwa vijana hawa wa kizazi kipya ni vyema wakajiangalia tena na kujipima wako wapi, wanatoka wapi na wanakwenda wapi.
Huko huambulia makombo tu. Angalia mwanadada mmoja iliripotiwa ndani ya jamvi hili kuwa aliachwa kwenye msafara wa JK huko Singida na ikabidi ajikodishie pikipiki imrudishe kule alikofikia. Wanamuziki wa kizazi kipya wamejikuta katika hali mbaya kifedha kiasi kwamba wanasiasa huwatumia na baadaye kuwatelekeza.
Mfano katika mkutano mkuu wa CCM wa mwaka 2007 uliomtawaza JK kuwa Mwenyekiti wa CCM, JK aliwaumbua wanamuziki hao baada ya matumbuizo yao pale aliposema......" Hawa tulikuwa nao na tuliwatumia katika kampeni zetu za 2005.."
Ungelitegemea basi baada ya kauli ya bosi huyo wa CCM, kizazi kipya wangelijifunza na kuachana na tabia hiyo ya kujidhalilisha kwenye kampeni za CCM ambako uchunguzi wangu umebaini malipo wanayolipwa ni kiduchu sana.
Lakini mwanamuziki wa kwaya ya dini au "gospel" mwanamama Rose Mhando amewaonyesha njia kizazi kipya kwani huko Kenya ameingia mkataba mnono na Safaricom na nyimbo zake sasa zinatumika katika mtandao huo naye hulipwa pesa kibao.
Mfano wimbo wake wa "Nibebe" sasa unamwingizia zaidi ya Tshs 16 Milioni kwa mwezi au Kshs 800, 000/= kwa Exchange rate of one Kshs for 20 Tshs.
Kwa kitega uchumi kama hicho Rose Mhando anapata zaidi ya Tshs 152 Milioni kwa mwaka kwa wimbo mmoja tu. Na anazo nyimbo nyingi kwenye mtandao wa Safaricom na hivi sasa ana matamasha mengi huko Kenya kutangaza nyimbo zake ili watumiaji wa mtandao wa safaricom waweze kuwa wanazitumia kwenye milio ya sauti ya simu zao.
Sidhani hata kampeni ikiendelea kwa miaka kumi ijayo kama kizazi kipya kilichojisalimisha kwa wanasiasa wetu wa CCM kitakaa kiweze kupambana na mapato ya gwiji huyu wa miziki ya kidini.
Ushauri wangu ni kuwa vijana hawa wa kizazi kipya ni vyema wakajiangalia tena na kujipima wako wapi, wanatoka wapi na wanakwenda wapi.