Wakati Kapuya karejea kutoka India akiwa hajambo...

Mlalahoi

JF-Expert Member
Aug 31, 2006
2,182
883
Source:Majira


...Kada aliyepata ajali na Kapuya afariki-3rd


Na Waandishi wetu, Dar na Tabora

MWENYEKITI wa CCM wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Bw Twaha Ngosso ambaye hivi karibuni alipata ajali akiwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Prof. Juma Kapuya, amefariki dunia jana baada ya kuwa amelazwa hospitali ya Muhimbili alikokuwa akitibiwa majeraha aliyopata.

Kwa mujibu wa Katibu wa CCM mkoa wa Tabora. Bw Daniel Fussi marehemu amefariki dunia saa mbili asubuhi na mwili wake unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda mkoani Tabora kwa mazishi.

Bw. Fusi alisema kuwa mwili huo unatarajiwa kuwasili kwa ndege majira saa tano asubuhi ambapo utasafirishwa hadi kijijini kwake Usindi na kwamba taratibu za mazishi zimekamilika.

Alisema kuwa mazishi hayo yanatarajiwa kufanyika majira ya saa tisa alasiri baada ya kuwasili kijijini kwake na taratibu zote zimekamilika.

" Hivi sasa uongozi wa mkoa tupo katika kikao cha maandalizi ya mazishi na tunatarajiwa kupokea mwili wa marehemu kesho saa tisa alasiri na utasafirishwa kwenda Urambo kwa mazishi," alifafanua.

Wakati huo huo, Waziri Kapuya ambaye alikuwa amepelekwa nchini India kwa matibabu zaidi mara baada ya ajali hiyo, amerejea nchini juzi mchana na hali yake inaendelea vizuri.

"Nimetoka kuzungumza naye hivi sasa, yupo Dar es Salaam na anaendelea vyema. Alikuwa akisumbuliwa na kifua kwa sababu ajali ilipotokea alibanwa sana na mkanda na anaweza kujimudu kutembea mwenyewe," kilisema chanzo chetu kilicho karibu na Waziri huo.

Inasemekana kwamba laiti uhai wa kada huyu ungepewa uzito unaostahili basi yeye ndiye aliyepaswa kwenda nje kwa matibabu kwani hali yake ilikuwa mbaya zaidi ya ile ya Kapuya.Hatahivyo,kazi ya Mungu haina makosa japo kuna wakati uzembe na ubinafsi wa binadamu unachangia sana "kuharakisha maamuzi ya Mola eg kifo.
 
Hiyo ni picha kamili jinsi gani Watanzania wasio na fedha wanakufa katika hospotali za Tanzania ambazo hazina huduma bora wakati viongozi na familia zao wanakwenda kutibiwa nje ya nchi. Viongozi wetu wangeboresha huduma katika hospitali zetu, naamini hata wao wasingekua na sababu ya kwenda kutibiwa nje na maisha ya Watanzania wengi yangesalimishwa.
 
Inasemekana kwamba laiti uhai wa kada huyu ungepewa uzito unaostahili basi yeye ndiye aliyepaswa kwenda nje kwa matibabu kwani hali yake ilikuwa mbaya zaidi ya ile ya Kapuya.Hatahivyo,kazi ya Mungu haina makosa japo kuna wakati uzembe na ubinafsi wa binadamu unachangia sana "kuharakisha maamuzi ya Mola eg kifo.

Cheo chake ni kidogo, na nafikiri hakuwa na fedha ya kutosha kumpeleka nje.

Anyway mimi nafikiri kama Kapuya alipelekwa nje kulikuwa na haja hata yeye kupeleka.

Anyway mungu amlaze mahala pema peponi Amina.
 
Tunaambiwa Balali anaendelea na matibabu huko Marekani ilhali hata ugonjwa wake haufahamiki.Naamini kuwa gharama za matibabu zinatoka kwa walipa kodi wa TZ.
 
...ajali ya kapuya ilikuwa mbaya sana ..at least ukiangalia mtu pekee atakayejuwa amepona ni kapuya..inabidi amshukuru sana mungu...yaani kupona kwa kapuya kwenye ile gari iliyoumia kama ya salome..ni as if useme salome angepona..ni kama ngamia kupenya kwenye tundu la sindano..
 
kwani umeshasikia anayemzungumzia dereva wa mama Mbatia? wote walipata ajali na wote walikuwa katika kutumikia taifa kila mmoja kwa nafasi yake lakini hata sijui kama mwili uliletwa au ulizikwa Iringa. Hii ndio hali halisi mwenye nacho ndie hujaliwa zaidi ukiwa masikini probability ya kufa mapema ni kubwa hata kwa vifo vinavyozuilika.
 
Tunaambiwa Balali anaendelea na matibabu huko Marekani ilhali hata ugonjwa wake haufahamiki.Naamini kuwa gharama za matibabu zinatoka kwa walipa kodi wa TZ.

Balali siyo mgonjwa ameenda kupunguza stress!

Maamuzi yake ya kisiasa ndiyo yanamsumbua.

Hapa inabidi hata wanachama wa chama tawala wajue kuwa kina wenyewe na wenyewe ni wazito tu wadogowadogo hawala lao.
 
mlalahoi balali aliazimwa WB na pia anayo isurance policy..sasa nafikiri ana option yta kulipiwa na WB, au serikali but bora alipiwe na wamarekani siunajua sisi masikini...
 
mlalahoi balali aliazimwa WB na pia anayo insurance policy..sasa nafikiri ana option yta kulipiwa na WB, au serikali but bora alipiwe na wamarekani siunajua sisi masikini...

Ina maana aliazimwa kwa zaidi ya miaka 10? Hiyo insurance policy unayoisema Mzee Phill inalipiwa na nani? BoT au WB ama yeye mwenyewe? Kama wafanyakazi wa BoT wanalipiwa bima za afya (local) kwanini yeye Ballali asilipiwe matibabu yake nje ya nchi? Kama alikuwa tayari kuchota mabilioni ambayo ametuhumiwa kwenye ufisadi unategemea awe na huruma ya kutochota hela za matibabu yake akiwa US?

Nimeona kwenye post nyingi sana hapa JF watu wanasema Ballali alikuwa anafanya kazi WB, hii si kweli bali alikuwa akifanya kazi IMF. Alitoka IMF akaja Bongo kama mshauri wa Rais wa maswala ya kiuchumi kabla ya kuteuliwa kuwa Gavana wa BoT mwaka 1998 details zaidi ziko hapo chini kwenye profile yake.

Profile ya Ballali hii hapa:

Personal Profile:
1965, BA in Economics, Howard University, Washington DC; 1967, MA in Economics, Catholic University of America, Washington DC. 1967-1976, with the Bank of Tanzania: 1967-71, Economist; 1971, Senior Economist; 1972, Acting Director, Research; 1972-76, Secretary to the Board; 1973-76, Director, Research. 1976-97, with the International Monetary Fund: 1976-79, Economist, Fiscal Affairs Department, working as a Fiscal Specialist, Caribbean, West African and Asian countries; 1979-82, Desk Economist, Ghana; 1982-86, Senior Economist, working as Desk Economist, 1982-84, Ghana, 1985-86, Zimbabwe and 1984-85, Head, missions to Ghana; 1986-97, Deputy Division Chief, heading IMF missions to negotiate economic reform programmes, supervise and monitor the implementation of these reforms; 1997, Adviser. 1997-98, Economic Adviser to the President, State House, Dar es Salaam. Since 1998, current position. [ World Economic Forum - Retrieved on 3/7/2006 - www.weforum.org ]


or http://www.afdevinfo.com/htmlreports/org/..\peo\peo_510.aspx
 
Mungu ampumzishe Kada huyo, Kapuya umepona mwenzio ameondoka, ila Kapuya uwezo wa kifedha pia umekusaidi kupona kwako ukilinganisha na mwenzio ambaye angestahili kwenda huko ulikokuwa lakina hana uwezo, ila ni wazi kuwa hao maskini ndio wanaowapigia debe nyinyi wakubwa na kuwafikisha hapo mlipo.
 
Mnashangaa ya Kapuya.. vipi Mbowe (form 4 with poor grades) kwenda kusoma Hull (is struggling there), wakati bright young Mnyika with straight "A"( Division 1 points 7)anahangaika Kinondoni pale.

Ndio dunia wenye nacho wanaongozewa......
 
Mnashangaa ya Kapuya.. vipi Mbowe (form 4 with poor grades) kwenda kusoma Hull (is struggling there), wakati bright young Mnyika with straight "A"( Division 1 points 7)anahangaika Kinondoni pale.

Ndio dunia wenye nacho wanaongozewa......


samvula thank you, maaana hawa waangalia pande zote za shilingi upande mmoja huuangalia kwa makengeza
 
Mnashangaa ya Kapuya.. vipi Mbowe (form 4 with poor grades) kwenda kusoma Hull (is struggling there), wakati bright young Mnyika with straight "A"( Division 1 points 7)anahangaika Kinondoni pale.

Ndio dunia wenye nacho wanaongozewa......

Mnyika anahangaika kivipi? Hajaenda university na grades hizo? Nitashangaa sana, labda kama kuna tatizo lingine la ajabu kabisa, lakini watu wa namna hiyo Tanzania huwa wanaenda university bila kipingamizi chochote.
 
Mnashangaa ya Kapuya.. vipi Mbowe (form 4 with poor grades) kwenda kusoma Hull (is struggling there), wakati bright young Mnyika with straight "A"( Division 1 points 7)anahangaika Kinondoni pale.

Ndio dunia wenye nacho wanaongozewa......


i agree with u ila nachoona wajaribu hamisha mind na change the topic kijanja...kapuya ofcourse kapelekwa india kwa fweza zetu sie wananchi..tena kwa fungu ambalo yawezekana limeibwa walaa halijaandikwa mahali..sasa kama ni kupewa afya it means uhai wa ule mwingine haukuwa muhimu kwa ccm??wote walikua in one ajali...ila ndio hivyo dunia haiko fair ila ccm imezidiiiiiii
 
Back
Top Bottom