Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,372
Wadau, amani iwe kwenu.
Ni dhahiri sasa kuwa CHADEMA inaelekea kufa. Ipo hoi bin taabani na hali ikiendelea hivi kwa zaidi ya miezi 3, kuna uwezekano viongozi watashinikizwa kujiuzulu. Time will tell.
Taarifa za kuaminika nilizopata hivi sasa ni kwamba, CHADEMA wapo hoi bin taabani kifedha. Mnyetishaji wangu toka Ufipa, yalipo Makao Makuu ya CHADEMA, anasema kuwa wafanyakazi wa Makao Makuu hawajalipwa fedha kwa muda wa mizei 3 sasa na kwamba hali ni ngumu kwa upande wao.
Mmoja wa wafanyakazi wa ofisi hiyo ambaye sitamtaja jina ila akisoma uzi huu atajijua amelalamika kuwa sikukuu za mwisho wa mwaka zimekaribia, pango la nyumba alilolipa miezi 6 iliyopita linaisha mwisho wa mwezi huu na watoto wanatakiwa kwenda shule Januari. Hana hakika ya fedha na kwamba wanaambiwa wavute subira kwa vile hali ya kifedha ni mbaya. Mbaya zaidi wanasikitika chama kutumia fedha kugharamia mikutano isiyo na tija badala ya kulipa mishahara watumishi wao.
Kwa hatua waliyofikia CHADEMA kwa sasa wanategemea miujiza ya Mungu tu kuwaokoa. Mnyetishaji wangu wa Makao Makuu ya CHADEMA amenidokeza kuwa hata sababu zilizotajwa na viongozi wa UKAWA za kutaka kususia uchaguzi wa marudio katika majimbo 3 hazina mashiko.
Kwamba, CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA hawana fedha za kugharamia mikutano ya kampeni kwa wagombea wake na ndo maana wametangaza kususia. Kwamba, hata kwenye chaguzi za Madiwani kwa kata 43 zilizomalizika, katika kata nyingi, CHADEMA hawakufanya mikutano ya kutosha ya kampeni na ndo maana wameshindwa vibaya.
Niwaombe sana viongozi wa CHADEMA. Hakuna dhambi mbaya kama kumtumikisha mtu kazi bila kumlipa ujira wake. Lipeni mishahara watumishi wenu ili muwe na hakika ya kuendesha mambo yenu kama taasisi. Vinginevyo mjiandae maumivu 2020.
Nawasilisha
Ni dhahiri sasa kuwa CHADEMA inaelekea kufa. Ipo hoi bin taabani na hali ikiendelea hivi kwa zaidi ya miezi 3, kuna uwezekano viongozi watashinikizwa kujiuzulu. Time will tell.
Taarifa za kuaminika nilizopata hivi sasa ni kwamba, CHADEMA wapo hoi bin taabani kifedha. Mnyetishaji wangu toka Ufipa, yalipo Makao Makuu ya CHADEMA, anasema kuwa wafanyakazi wa Makao Makuu hawajalipwa fedha kwa muda wa mizei 3 sasa na kwamba hali ni ngumu kwa upande wao.
Mmoja wa wafanyakazi wa ofisi hiyo ambaye sitamtaja jina ila akisoma uzi huu atajijua amelalamika kuwa sikukuu za mwisho wa mwaka zimekaribia, pango la nyumba alilolipa miezi 6 iliyopita linaisha mwisho wa mwezi huu na watoto wanatakiwa kwenda shule Januari. Hana hakika ya fedha na kwamba wanaambiwa wavute subira kwa vile hali ya kifedha ni mbaya. Mbaya zaidi wanasikitika chama kutumia fedha kugharamia mikutano isiyo na tija badala ya kulipa mishahara watumishi wao.
Kwa hatua waliyofikia CHADEMA kwa sasa wanategemea miujiza ya Mungu tu kuwaokoa. Mnyetishaji wangu wa Makao Makuu ya CHADEMA amenidokeza kuwa hata sababu zilizotajwa na viongozi wa UKAWA za kutaka kususia uchaguzi wa marudio katika majimbo 3 hazina mashiko.
Kwamba, CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA hawana fedha za kugharamia mikutano ya kampeni kwa wagombea wake na ndo maana wametangaza kususia. Kwamba, hata kwenye chaguzi za Madiwani kwa kata 43 zilizomalizika, katika kata nyingi, CHADEMA hawakufanya mikutano ya kutosha ya kampeni na ndo maana wameshindwa vibaya.
Niwaombe sana viongozi wa CHADEMA. Hakuna dhambi mbaya kama kumtumikisha mtu kazi bila kumlipa ujira wake. Lipeni mishahara watumishi wenu ili muwe na hakika ya kuendesha mambo yenu kama taasisi. Vinginevyo mjiandae maumivu 2020.
Nawasilisha