Wakati EAC inavunjika, nani alipata nini?

..kwanini Waganda hawako bitter na jinsi jumuiya ilivyovunjika mwaka 1977 kulinganisha na sisi Watanzania?

..au kwanini Waganda hawana hofu na jumuiya mpya kulinganisha na Watanzania tunavyoiogopa jumuiya?

..kwanini Watanzania hatuko tayari ku-embrace / ku-dominate jumuiya mpya ya afrika mashariki wakati tulikuwa na miaka 43+ ya kujiandaa toka 1977 mpaka 2021?
Mkuu ni kwasababu zifuatazo
1. hatukubali kuwa tuna matatizo ya kulitambua tatizo na kwamba tuna uwezo wa kuwa bora
Tumetawaliwa na inferiority complex hata pale tulipo na upper hand.

Mfano, sisi tulikubali soko huria , kwa muda mfupi tukawa mbali sana hasa kwa mawasiliano
Vyuo vyetu vinatoa watu bora (zama hizo nadhani) sisi hatuwezi kuwatumia wenzetu wanawatumia n.k.

2. Watanzania hatuna ujasiri wa kukabiliana katika ushindani. Hatukubali kuwa ushindani unatufanya tuwe bora na si uadui. Kwamba, tunahitaji changamoto ili kuongeza uwezo wetu wa kufikiri.

Mfano, badala ya kuifanya ATCL itoe huduma bora na ijiendeshe kibiashara, tumeua mashirika mengine ili kutoa monopoly. !!! Sasa hivi ATCL ni local haiwezi kushindana na KQ kwasababu rahisi , inaishi kwa monopoly na hakuna 'challenge' katika soko.

Ili uweze kutengeneza Tanbond bora lazima kuwe na Blue Band ya ushindani.

Tazama mfano wa kitaaluma. Ipo wapi UDSM iliyozalisha viongozi wa Afrika?
Iliyokuwa kitovu cha kweli cha wanasheria na Wachumi? Tumeua UDSM kwasababu hatutaki kusikia tofauti.

Nenda Makerere na Nairobi utaona tofauti kubwa , ule uhuru wa kitaaluma unawajenga na kutoa wasomi bora. Tukienda soko la ajira tunalalamika Wakenya wanachukua nafasi zetu.
Tunaweka sheria lukuki badala ya kuwaandaa vijana wetu kiushindani.

Tazana mijadala ya UDSM ya leo na udhaifu wake, unaweza kudhani ni uvccm vikaoni.

Kwa wale tuoijua UDSM ya zama hizo, ya leo inatushangaza.
Katika mazingira kama hayo, sera za nchi, mwelekeo na mtazamo hauchambuliwi kisomi.
UDSM inajifia taratibu, huko Makerere na Nairobi wanachanja mbuga.

Ironically, vijana wetu hawawezi kwenda kugombea soko la Uganda au Kenya. Sio kwamba hawawezi, la hasha, hawakujengwa katika ushindani. Wamelelewa katika monopoly na wanaishi na inferiority complex

Inasikikitisha nusu karne bado tunalalama na kuwaza kama zamani.

Tunalaumu EAC na Ukombozi tena wanaofanya hivyo ni watu tusiotarajia waseme hayo! hawana hoja hawatafuti majibu wanatafuta flimsy excuse
 
..nadhani wakati umefika kwa Tz kuwa na MKAKATI wa muda mfupi, na muda mrefu, wa kuwaandaa vijana wetu kwa mabadiliko na fursa zinazojitokeza ktk Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mkuu ilipoanza EAC ya leo mjadala ulikuwa kuhusu transition period.
Tanzania ilitaka miaka 10 na nakumbuka miaka ya Kikwete ilikusudiwa hivyo.

Haraka haraka za CoW (Coalition of Willing) zililete mzozo na hoja kubwa ya Tz ilikuwa muda wa kujiandaa. Ni miaka 15 tangu JK aondoke na zaidi ya 23 ya EAC mpya, bado hatujajiandaa!

Kwa muda mfupi, soko liwe huru hasa la ajira. Vijana wetu watajifunza ushindani na si kulindwa na monopoly zilizojengwa juu ya sheria.

Kwa muda mrefu,lazima mitaala ya elimu iangaliwe, ijengwe katika uhalisia wa mazingira na si kukariri.

Maeneo ya taaluma yawe huru ili kuibua chem chem za fikra, kupambanisha hoja, kuchambua na kuchambuliwa.

Ndivyo Makerere na Nairobi wanavyofanya na hilo linawajengea sana vijana uwezo wa kutafiti, kujieleza na kutetea hoja kwa mantiki.

Utakumbuka zama UDSM kulikuwa na mijadala kila kona ya namna mbali mbali, iwe sheria, uchumi, siasa n.k

Palipokuwa na mjadala pale Nkrumah wanafunzi wa vyuo jirani walihudhuria
Wageni kama Marais walialikwa UDSM

Leo hali ipoje? ni kama highschool kubwa tu kwasababu uhuru wa taaluma ''academic freedom' haupo.

Katika soko la utandawazi ''globalization'' dunia haitafuti mabingwa wa kukariri, inatafuta watu wanaofikiri, kuyaona matatizo, kuyaeleza na kutafuta ufumbuzi. Swali, vijana wetu nafasi yao ipo wapi?

Kama kuna mambo yanayokera ni kusikia eti kuna Wakenya/Waganda wamenyimwa vibali vya kazi Tanzania.

Mashirika na Kampuni za dunia zinatafuta 'waajiriwa local' ili kupunguza gharama, lakini zinachukua wa nje
Swali, ni kwanini organization zimekubali kuchukua gharama hizo?

Pengine jibu ni rahisi kwamba ukipata qualified person mwenye mtazamo mpana ni bora kuliko kijana wa Tanzania atakayeajiriwa bila tija katika organization husika.

Solution si kuwanyima vibali, bali kuwaachai watoe changamoto kwa vijana wenyewe wakisema '' watatia akili''.

Bila hivyo huu mwendo wa mbeleko unazidi kuwadumaza tu!

Matokeo yake ni kutaka protection kila siku badala ya kufikiri namna ya kupambana.
 
Mkuu ilipoanza EAC ya leo mjadala ulikuwa kuhusu transition period.
Tanzania ilitaka miaka 10 na nakumbuka miaka ya Kikwete ilikusudiwa hivyo.

Haraka haraka za CoW (Coalition of Willing) zililete mzozo na hoja kubwa ya Tz ilikuwa muda wa kujiandaa. Ni miaka 15 tangu JK aondoke na zaidi ya 23 ya EAC mpya, bado hatujajiandaa!

Kwa muda mfupi, soko liwe huru hasa la ajira. Vijana wetu watajifunza ushindani na si kulindwa na monopoly zilizojengwa juu ya sheria.

Kwa muda mrefu,lazima mitaala ya elimu iangaliwe, ijengwe katika uhalisia wa mazingira na si kukariri.

Maeneo ya taaluma yawe huru ili kuibua chem chem za fikra, kupambanisha hoja, kuchambua na kuchambuliwa.

Ndivyo Makerere na Nairobi wanavyofanya na hilo linawajengea sana vijana uwezo wa kutafiti, kujieleza na kutetea hoja kwa mantiki.

Utakumbuka zama UDSM kulikuwa na mijadala kila kona ya namna mbali mbali, iwe sheria, uchumi, siasa n.k

Palipokuwa na mjadala pale Nkrumah wanafunzi wa vyuo jirani walihudhuria
Wageni kama Marais walialikwa UDSM

Leo hali ipoje? ni kama highschool kubwa tu kwasababu uhuru wa taaluma ''academic freedom' haupo.

Katika soko la utandawazi ''globalization'' dunia haitafuti mabingwa wa kukariri, inatafuta watu wanaofikiri, kuyaona matatizo, kuyaeleza na kutafuta ufumbuzi. Swali, vijana wetu nafasi yao ipo wapi?

Kama kuna mambo yanayokera ni kusikia eti kuna Wakenya/Waganda wamenyimwa vibali vya kazi Tanzania.

Mashirika na Kampuni za dunia zinatafuta 'waajiriwa local' ili kupunguza gharama, lakini zinachukua wa nje
Swali, ni kwanini organization zimekubali kuchukua gharama hizo?

Pengine jibu ni rahisi kwamba ukipata qualified person mwenye mtazamo mpana ni bora kuliko kijana wa Tanzania atakayeajiriwa bila tija katika organization husika.

Solution si kuwanyima vibali, bali kuwaachai watoe changamoto kwa vijana wenyewe wakisema '' watatia akili''.

Bila hivyo huu mwendo wa mbeleko unazidi kuwadumaza tu!

Matokeo yake ni kutaka protection kila siku badala ya kufikiri namna ya kupambana.
Wakenya wanatutaniaga kwamba bado tuna hangover ya ujamaa. Kikweli siyo hangover bali bado tumelewa. Ujamaa ndiyo unafanya monopoly na protectionism kila sehemu. Monopoly hadi kwenye elimu. Kukiwa na monopoly ubunifu kunakuwa hakuna kabisa.

Hii nchi bado ni ya kijamaa. Watu wanaweza sema ujamaa umebaki jina ila tunaishi kibepari, si kweli. Sheria zetu, taasisi zetu na mfumo mzima wa kuendesha mambo ni wa kijamaa. Inatakiwa kuukana rasmi ujamaa hapo ndiyo tunaweza kubadilika. Tusitegemee utaisha wenyewe. Ukiukana rasmi hata sheria zako, taratibu zako na jinsi unavyiendesha mambo itakuwa tofauti.

Mfano, kwenye nchi za ujamaa kulikuwa na sheria kali sana kuhusu watu kutoka nje ya nchi yao. Ndiyo kisa hata kujenga ukuta wa Berlin. Leo hii hilo suala lipo hapa kwetu. Mtu kutoka nje kunakuwa na vikwazo vingi sana.

Vijana hawawezi kushindana sababu ujamaa hauja wa drill kushindana. Hata elimu yetu imeathiriwa na mtindo huo wa kijamaa, elimu ya kijamaa huwa haizalishi wabunifu na washindani. Serikali, muajiri wao mkubwa haangalii sana vitu hivyo.
 
Nimewahi kusikia kuwa EAC ya mwanzo ilianzishwa kama pilot project ya European Union,sijui ina ukweli kiasi gani?
 
Baada ya EAC kuvunjika nchi wanachama zilimteua, Dr.Victor Umbricht, raia wa Uswizi, kuwa msuluhishi wa kugawa mali na madeni ya jumuiya.

Kwa msingi huo, siyo sahihi kusema kwa nchi fulani ilidhulumiwa, au kuwa na chuki na nchi fulani kwamba imeiba mali za jumuiya.

Kwa upande mwingine, serikali ya Tanzania ilipewa fedha za pensheni za watumishi waliokuwa wakifanya kazi ktk taasisi mbalimbali za jumuiya. kwa bahati mbaya serikali ilizipangia fedha hizo matumizi mengine na kusababisha malalamiko na mgogoro mkubwa wa "wastaafu wa jumuiya ya afrika mashariki."

cc Nguruvi3, Mohamed Said

Mpaka sasa ni miaka 43 imepita wazee hao bado hawajalipwa stahiki zao! walilipwa nauli tu ya kurudi makwao(Passage).
 
Mie ule mgogoro nilikuwepo Ila Tanzania tulipendelewa sana ajili ya midomo yetu ! tulifika mahala tukawa tunapiga ngenga kwa kiswahili tuuuu!...kenya kwa sababu hawakukipenda kiswahili saaana walipata mali kidogo mnooo!!

mpaka nikawaonea huruma kuumbe Lugha ya kwenu nayo inasaidia, usijifanye hujui kikwenu eti unaongea tuuu lugha ya kibeberu jamani!
 
Kuna makosa fulani katika mahojiano hayo, ndiyo maana mahojiano hayo yanabidi yachukuliwe kwa context ya hali halisi iliyokuwapo siyo kwa maneno ya mahojiano. Kwa mfano Umbritch ameweka tamko la Obote mwaka 1977 na waganda kukikimbia nchi lakini Amin alipokuja madarakani mwaka 1977 bado hawakurudi; unaona wazi kabisa kuwa statement hiyo haina ukweli ingawa maana yake ni sahihi.

Kusingetokea vita ya Uganda, ripoti ile isingekubaliwa kabisa, kwa hiyo Kenya walikua na opportunity kubwa sana kwa ya report hiyo kutolewa at the right time! Jambo lililosababisha KQ kunyanuka mara moja!
Amini aliingia 1971 nadhani umeteleza kidogo
 
Back
Top Bottom