Wakati EAC inavunjika, nani alipata nini?

Ule mgawanyo wa Umbritch haukuwa fair, ila nchi zililazamika kukubaliana ili mambo yaishe hasa kwa vile wakati huo Tanzania na Uganda zilikuwa zimetoka vitani; alifanya kazi ya usuluhishi kwa karibu miaka kumi akamaliza mwaka 1982 baada ya vita. Ukisoma mahojiano yake hapa kwenye ukurasa wa 10 utaona kuwa hakukuwa na consensus kabisa kuhusu mgawanyo huo ambapo Kenya ilipata zaidi ya Tanzania wakati Uganda ndiyo iliyoonewa zaidi. Anasema mgawanyo wake ulifuata indicators za IMF, ambazo wakati huo zilikuwa zinaipendelea sana Kenya politically wakati huo kwa kuwa na uchumi ambao ni "market oriented"..
Nimesoma haya mahojiano yote, yanafungua macho. Shukrani kwa kuyaweka hapa.

Huyu doctor anasema hicho kigezo cha kutumia indicator za IMF nchi zilikipinga hivuo hawakukitumia. Bali walitumia sababu za kijiografia na kuangalia usawa. Pia waligawana madeni ya jumuiya ambapo anasema nchi zilikuwa zinalipa vizuri sana.

Anasema nchi zilizopata assets nyingi zilitakiwa kulipa zile zilizopata assets chache ili kufikia usawa. Naona kama jamaa alifanya kazi nzuri sana. Na ndiyo umefanya hata huu ushirikiano wa sasa uweze kuwepo. Sioni kama kuna mtu alionewa.

Hili jumuia ilikuwa kubwa sana. Wafanyakazi 100,000 siyo mchezo!
 
Kichuguu,

Kwanza, nikushukuru sana sana kwa kutuletea document yenye mahojiano ya Dr.Victor Umbricht. kwa kweli umeutendea HISANI kubwa mjadala wetu, na wachangiaji wake.

Pili, bila waTz kuandika kwamba hawakukubaliana na mapendekezo ya Dr.Umbricht, na kubainisha ni vipengele gani hawakukubaliana navyo, basi maelezo ya msuluhishi yatabaki kuwa ndio ukweli wenyewe.

Tatu, kuna mahali Dr.Umbricht anasema Uganda / Obote alipinga baadhi ya mapendekezo yake, lakini mapendekezo hayo yalipohakikiwa tofauti ya alichopendekeza msuluhishi na walichopendekeza independent experts kilikuwa ni asilimia 1 %. kwa hiyo binafsi nalazimika kuamini kwamba Dr.Umbricht alifanya kazi yake bila upendeleo.
 
Nashukuru sana mkuu

Ila kutokana na hoja hii, ilitakiwa kwenye Mkataba wa EAC2 wa 1999; Kenya ichangie zaidi kwa kuwa ilifaidika zaidi na anguko la EAC1

Kwa nini wachumi hawakulirudisha hili mezani

Hakuna nchi ambayo ilifaidika kwa anguko la EAC.

Kenya inaonekana kuwa "ilifaidika" kwasababu walikuwa na uchumi mkubwa kuliko majirani zake wakati tunaanzisha EAC. Kwa msingi huo basi wakati jumuiya inavunjika Kenya bado ilikuwa na uchumi mkubwa kuzidi majirani zake.

Vilevile, Kenya wamekuwa stable ktk falsafa na sera zao za kiuchumi kwa muda mrefu sana. Wenzetu hawajawahi kuchukua hatua kali za kubadili muelekeo wa kiuchumi kama Tanzania tulivyofanya ktk azimio la arusha, na baadae kukumbatia soko huria.

Zaidi, Kenya haijawahi kupigana vita iliyosababisha mbinyo wa kiuchumi kama Tanzania na Uganda zilivopigana vita, au vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waganda. Kwa hiyo kwa muda mrefu uchumi wa Kenya haujawahi kutikisika kama ambavyo uchumi wa Tanzania na Uganda umetikisika.

Hizi habari za kusema Wakenya walitudhulumu ni kichaka ambacho viongozi wetu wamekitumia kukwepa kuwajibika kwa kuendesha uchumi wetu vibaya. Matatizo ya uchumi ya Tanzania kwa kiwango kikubwa yamesababishwa na maamuzi mabaya ya viongozi wetu.
 
Kichuguu,
Kwanza, nikushukuru sana sana kwa kutuletea document yenye mahojiano ya Dr.Victor Umbricht. kwa kweli umeutendea HISANI kubwa mjadala wetu, na wachangiaji wake.

Pili, bila waTz kuandika kwamba hawakukubaliana na mapendekezo ya Dr.Umbricht, na kubainisha ni vipengele gani hawakukubaliana navyo, basi maelezo ya msuluhishi yatabaki kuwa ndio ukweli wenyewe.

Tatu, kuna mahali Dr.Umbricht anasema Uganda / Obote alipinga baadhi ya mapendekezo yake, lakini mapendekezo hayo yalipohakikiwa tofauti ya alichopendekeza msuluhishi na walichopendekeza independent experts kilikuwa ni asilimia 1 %. kwa hiyo binafsi nalazimika kuamini kwamba Dr.Umbricht alifanya kazi yake bila upendeleo.

Kuna makosa fulani katika mahojiano hayo, ndiyo maana mahojiano hayo yanabidi yachukuliwe kwa context ya hali halisi iliyokuwapo siyo kwa maneno ya mahojiano. Kwa mfano Umbritch ameweka tamko la Obote mwaka 1977 na waganda kukikimbia nchi lakini Amin alipokuja madarakani mwaka 1977 bado hawakurudi; unaona wazi kabisa kuwa statement hiyo haina ukweli ingawa maana yake ni sahihi.

Kusingetokea vita ya Uganda, ripoti ile isingekubaliwa kabisa, kwa hiyo Kenya walikua na opportunity kubwa sana kwa ya report hiyo kutolewa at the right time! Jambo lililosababisha KQ kunyanuka mara moja!
 
Nimesoma haya mahojiano yote, yanafungua macho. Shukrani kwa kuyaweka hapa.

Huyu doctor anasema hicho kigezo cha kutumia indicator za IMF nchi zilikipinga hivuo hawakukitumia. Bali walitumia sababu za kijiografia na kuangalia usawa. Pia waligawana madeni ya jumuiya ambapo anasema nchi zilikuwa zinalipa vizuri sana.

Anasema nchi zilizopata assets nyingi zilitakiwa kulipa zile zilizopata assets chache ili kufikia usawa. Naona kama jamaa alifanya kazi nzuri sana. Na ndiyo umefanya hata huu ushirikiano wa sasa uweze kuwepo. Sioni kama kuna mtu alionewa.

Hili jumuia ilikuwa kubwa sana. Wafanyakazi 100,000 siyo mchezo!
Hawakutumia kigezo cha IMF indicators, lakini mgawanyo wenyewe ulifanyika hivyo, kwani baada ya kuamaua kutumia geographical location na equality bado walikuwa wamo kwenye zile IFM indicators tu
 
Shirika kama NMC liliendeshwa vibaya na lilipokuja kubinafsishwa lilikuwa hoi bin taabani. Mamlaka za mazao mbalimbali nazo hazikuwa na ufanisi kama ule wa vyama vya ushirika.
Mkuu mashirika mengi yalikufa kwasababu ya kuendeshwa kisiasa zaid ya kiuchumi. Unakumbuka mwenyekiti wa tawi la chama katika shirika fulani alikuwa na nguvu kuliko meneja. Vyama vya wafanyakazi vikawa matawi ya chama tawala. Hakuna aliyeeleza ubovu au kuwasemea wafanyakazi.

Kuanzisha mamlaka na kuua vyama vya ushirika ilikuwa kosa kubwa sana kiuchumi. Vyama kama KNCU au Nyanza vilifikia mahali pa kutafuta masoko, kuendesha kilimo, kusambaza pembejeo n.k.

Vilisaidia sana kuondoa urasimu wa serikali wakati huo vikichangia pato la nchi
Azimio la Arusha lilikuwa baya sana kwa upande wa uchumi. Uzuri wa azimio upo ktk masuala ya maadili ya viongozi.
Azimio la Arusha liliharibu sehemu kubwa sana ya Uchumi wa nchi.
Pamoja na kujaribu kuwaleta watu pamoja, madhara yalikuwa makubwa.
Mfano, kutaifisha mashamba ya Mkonge kutoka kwa 'masetla' ilikuwa ujinga tu.
Bei ya mkonge ilipoanguka masetla wange transform kilimo kwenda kingine.
Mashamba yamebaki mapori ! ilikuwa mbaya sana
..Dr.Umbricht anasema timu yake ilitafuta mali / assets zote za zilizokuwa taasisi za East African Community na kuzigawa kwa namna ambayo nchi zote ziliridhika. Anasema alitafuta siyo mali kubwa-kubwa kama ndege, na mabehewa ya treni, bali alitafuta na kuhakiki mpaka mali ndogo kama typewriter!!
Kuna point hapa. Dr Umbricht alisimamia mali na madeni (assets and liabilities of the defunct EAC)
Kenya ilichukua mali nyingi lakini pia ilibeba sehemu kubwa ya madeni

Advantage waliyokuwa nayo Kenya ni kuwa taasisi za EAC ziliendelea kama mali zao.

Kenya hawakuanzisha shirika la ndege, walitumia za EAC, wala hawakununua mabehewa au Injini za Treni
Natamani sana mzee Mtei angefunguka hapa, nadhani atakuwa anafafanua declassified information.
 
Ila kutokana na hoja hii, ilitakiwa kwenye Mkataba wa EAC2 wa 1999; Kenya ichangie zaidi kwa kuwa ilifaidika zaidi na anguko la EAC1. Kwa nini wachumi hawakulirudisha hili mezani
Hapa kuna mambo mawili unatakiwa kuyaangalia.

1. Kwanini na nani alikuwa nyuma ya anguko la EAC. Kama utakumbuka mtu mashuhuri aliyepelekea anguko ni Charles Njonjo. Huyu alikuwa na nguvu sana wakati wa Kenyatta ingawa Moi alikuwa ndani ya serikali.

Kuanzishwa kwa EAC ilikuwa ni suala la majadiliano ya Moi, Museveni na Mzee Mwinyi

Sijui unawezaje kuwaadhibu Kenya kwa makosa ya viongozi wao waliondoka na kama hilo lingeleta utangamano

2. Uchumi ; Apparently unaweza kuona kama Kenya ilifaidika sana, kiuhalisia Kenya iliathirika kama nchi nyingine.
Kwa wale walioishi zama hizo akina Joka, watakumbuka Nairobi ilikuwa 'manufacturing Hub' ya EAC
Viwanda viilitumia nembo ya ' East Africa Manufacturing-Nairobi' Bidhaa zote zilitoka Nairobi

Viwanda vya TanBond vilijengwa kama mbadala wa 'Blue Band'. Kiwanda cha Gardenia Tanga vilianzishwa haraka kama mbadala, ikiwemo vile vya dawa za whitedent kama chokaa , Matshushita n.k.

Pamoja na hayo, soko la bidhaa za Kenya ilikuwa nchi za EA.
Kwahiyo kufa kwa EAC kuliiathiri Kenya na pengine kuimarisha nchi zingine na ndiyo maana kwenye EAC ya sasa nchi washirika wana nguvu kuliko ilivyokuwa.

Ukitaka kujua Kenya iliathirika kiasi gani, baada ya EAC ya sasa kuanzishwa Kenya ilifurahi sana na kutaka kufanya kila jambo 'fasta' . Kama utamkumbuka yule msemaji wa serikali ya Kenya aliyekuwa anajificha nyuma ya jina la mwandishi wa habari Warigi Kamau, akiishambulia Tanzania eti haina kasi

Kutokana na funzo la 1977 Tanzania ilisita na imekuwa na uangalifu sana historia isije ikajirudia.
Upo msemo '' Fool me once , shame on you, fool me twice, shame on me'
 
Nguruvi3,

..naomba hapo ulipomjibu Sita Sita uongezee kwamba nchi zote zilikuwa na mchango ktk kuanguka kwa EAC.

..Tanzania tulikuwa tunafuata mlengo wa KIJAMAA ambao hauendani vizuri na siasa za wenzetu wa Kenya.

..Kenya walikuwa ni MABEPARI ambao walikuwa wanatishiwa na ujamaa wa Tanzania.

..Uganda walikuwa wanatawaliwa na DIKTETA asiyetabirika na aliyekuwa na mgogoro wa kisiasa na majirani zake.

..Kuna taarifa kwamba ilifika mahali viongozi wakuu, yaani Kenyatta, Nyerere, na Iddi Amini, walikuwa hawawezi kukaa meza moja, kujadili, na kuamua masuala ya EAC.

..Tusiwalaumu Wakenya peke yao kwamba ndio waliovunja jumuiya. Kama Wakenya na Charles Njonjo ndiyo waliofitini jumuiya, mbona Tanzania na Uganda hazikuendeleza mashirikiano na kuunda jumuiya / coalition ya nchi mbili [ Tz & Ug ]?
 
Nguruvi3,

..naomba hapo ulipomjibu Sita Sita uongezee kwamba nchi zote zilikuwa na mchango ktk kuanguka kwa EAC.

..Tanzania tulikuwa tunafuata mlengo wa KIJAMAA ambao hauendani vizuri na siasa za wenzetu wa Kenya.

..Kenya walikuwa ni MABEPARI ambao walikuwa wanatishiwa na ujamaa wa Tanzania.

..Uganda walikuwa wanatawaliwa na DIKTETA asiyetabirika na aliyekuwa na mgogoro wa kisiasa na majirani zake.

..Kuna taarifa kwamba ilifika mahali viongozi wakuu, yaani Kenyatta, Nyerere, na Iddi Amini, walikuwa hawawezi kukaa meza moja, kujadili, na kuamua masuala ya EAC.

..Tusiwalaumu Wakenya peke yao kwamba ndio waliovunja jumuiya. Kama Wakenya na Charles Njonjo ndiyo waliofitini jumuiya, mbona Tanzania na Uganda hazikuendeleza mashirikiano na kuunda jumuiya / coalition ya nchi mbili [ Tz & Ug ]?
Thanks Bro

Pamoja na kupigana na Uganda, Tanzania ilikua busy na ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika (Namibia, Angola, Zimbabwe, Afrika Kusini)
Resources nyingi zilipelekwa kuhudumia kambi za wapiganaji na familia zao

Kwa hiyo EAC ilionekana kama mzigo usio na manufaa kwa wananchi wa kawaida

kwa kuwa ilikua inanufaisha zaidi Kampuni kubwa zilizokuwa na uwezo wa kufanya cross border trade ambazo nyingi zilitokea Kenya na wamiliki wake ni Mabepari wenye asili ya nchi za Uingereza, Uholanzi na India.

Baada ya WW, Tanzania iliwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza, Hawa jamaa kwa kuwa walikua na interests zaidi hapo Nairobi, walitugeuza sisi soko la bidhaa zao from Kenya. Mfumo wa kutegemea bidhaa za Kenya ulianzia hapa.

Hata ilivyokuja EAC ilijitahidi kupunguza utegemezi wa viwanda vya Kenya lakini bado haikuwezekana.

So far situation ipo hivyo hivyo, EAC inanufaisha zaidi Kampuni kubwa za Kenya

Unga wa Bhakressa unaletewa zengwe kuingia Kenya

Kioo Limited nao walipigwa kodi za ajabu ajabu wasiweze kuingia Kenya

Konyagi nao wanapigwa zengwe kila siku

Tutaendelea hivi mpaka siku tukiweza kuwafundisha watoto wetu umuhimu wa kutumia bidhaa za Tanzania.
 
Jamani mwaka 1977 nchi ya Uganda ilikuwa chini ya Idi Amini Dadaa, sasa Obote alipata wapi nafasi ya kuwa msemajia wa nchi ya Uganda Kumbuka Idi Amini aliongia madarakani mwaka 1971.
Kuna makosa fulani katika mahojiano hayo, ndiyo maana mahojiano hayo yanabidi yachukuliwe kwa context ya hali halisi iliyokuwapo siyo kwa maneno ya mahojiano. Kwa mfano Umbritch ameweka tamko la Obote mwaka 1977 na waganda kukikimbia nchi lakini Amin alipokuja madarakani mwaka 1977 bado hawakurudi; unaona wazi kabisa kuwa statement hiyo haina ukweli ingawa maana yake ni sahihi.

Kusingetokea vita ya Uganda, ripoti ile isingekubaliwa kabisa, kwa hiyo Kenya walikua na opportunity kubwa sana kwa ya report hiyo kutolewa at the right time! Jambo lililosababisha KQ kunyanuka mara moja!
 
..kulikuwa na crisis baada ya jumuiya kuvunjika, na ktk crisis hiyo ndiyo unasikia habari za rubani kutoroka na ndege. pia nimewahi kusikia habari ya mpaka wa Tz na Kny kufungwa, etc etc.

..lingine unalopaswa kukumbuka ni kwamba kila nchi mwanachama ilikuwa ina-host taasisi za Jumuiya kama vile bandari, reli, posta, shirika la ndege, pamoja na mali na miundombinu ya taasisi hizo. Kwa hiyo kila nchi ilirithi taasisi za jumuiya na kuzifanya za kitaifa.

vilevile kulikuwa na wafanyakazi wa Jumuiya. Wako waTz walikuwa wakifanya kazi Kenya, au Uganda, na pia walikuwepo raia toka nchi majirani waliokuwa wakifanya kazi Tz. kutokana hali hiyo ilibidi kila nchi ichukue raia wake na kuwarejesha nyumbani.

..Lakini baada ya hapo nchi wanachama zilimteua Dr.Victor Umbricht ambaye alifanya kazi kubwa ya kuhakikisha mali na madeni ya jumuiya yanagawanywa kwa haki. Binafsi sijasikia popote pale serikali yetu ikilalamikia utendaji na kazi iliyofanywa na Dr.Umbricht.

..Kuhusu nchi gani iliumia zaidi, nadhani ilitegemea nchi husika ilikuwa imara kiasi gani wakati wa kuanzishwa kwa jumuiya. Kama nchi A ilikuwa na uchumi mdogo kuliko nchi B wakati wa kuanzisha jumuiya basi hali ilikuwa hivyohivyo wakati jumuiya inavunjika.
Nimewahi kukaa ofisi moja na mtu aliyekuwa mtaalam wa computer wa EAC huko Nairobi ambaye ni mtanzania,anasema wakenya walijiandaa kuvunja EAC kimya kimya, watumishi wa kitanzania na waganda walikuwa wanafichwa baadhi ya documents na kutengwa,ndege na treni nzuri zilipoingia Kenya hazikuruhusiwa kurudi Tz au Uganda, mpaka walipokamilisha walichokihitaji ndio wakatangaza hawahitaji tena EAC, japo mtu mmoja senior officer (kileo) wa Tz alitoa alert kwa Baba wa Taifa, labda ilisaidia kidogo.

Huyo mfilisi alikuja kuwekwa miaka miwili baadae wakati hizo mali zote waliendelea kuzitumia smoothly as if EAC bado ipo ,wakati Tz na Uganda zikiumia kutafuta replacements ya zile zilizotoroshewa Kenya, Tanzania na Uganda ziliumia na hali hiyo. Sidhani kama utetezi wa maana sana, huyo rubani alisaidia kwa sababu inaonekana hiyo ndio ndege kubwa pekee tuliyoambulia.
 
Nasikia hii ilivunjika mwaka 1977. Nimekuwa nikisikia hadithi nyingi kuwa watu waligawana mali kama washenzi(barbarians). Hili limewapa baadhi ya watu vinyongo hadi leo kuwa walidhulumiwa, naomba kujua kwenye kugawana huko, Uganda alipata nini, Kenya alipata nini na Tanzania alipata nini?

Bila kusahau mafao ya wazee wa east africa wa kila nchi walilipwaje? TZ waliondoka na Tsh 20 ,wengi 30 Tsh etc
 
Jamani mwaka 1977 nchi ya Uganda ilikuwa chini ya Idi Amini Dadaa, sasa Obote alipata wapi nafasi ya kuwa msemajia wa nchi ya Uganda Kumbuka Idi Amini aliongia madarakani mwaka 1971.
Ndiyo makosa niliyosema
 
Baada ya EAC kuvunjika nchi wanachama zilimteua, Dr.Victor Umbricht, raia wa Uswizi, kuwa msuluhishi wa kugawa mali na madeni ya jumuiya.

Kwa msingi huo, siyo sahihi kusema kwa nchi fulani ilidhulumiwa, au kuwa na chuki na nchi fulani kwamba imeiba mali za jumuiya.

Kwa upande mwingine, serikali ya Tanzania ilipewa fedha za pensheni za watumishi waliokuwa wakifanya kazi ktk taasisi mbalimbali za jumuiya. kwa bahati mbaya serikali ilizipangia fedha hizo matumizi mengine na kusababisha malalamiko na mgogoro mkubwa wa "wastaafu wa jumuiya ya afrika mashariki."

cc Nguruvi3, Mohamed Said
Hili tatizo la kupangia pesa za watu matumizi mengine ni sugu sana.
 
Nimewahi kukaa ofisi moja na mtu aliyekuwa mtaalam wa computer wa EAC huko Nairobi ambaye ni mtanzania,anasema wakenya walijiandaa kuvunja EAC kimya kimya, watumishi wa kitanzania na waganda walikuwa wanafichwa baadhi ya documents na kutengwa,ndege na treni nzuri zilipoingia Kenya hazikuruhusiwa kurudi Tz au Uganda, mpaka walipokamilisha walichokihitaji ndio wakatangaza hawahitaji tena EAC, japo mtu mmoja senior officer (kileo) wa Tz alitoa alert kwa Baba wa Taifa, labda ilisaidia kidogo.

Huyo mfilisi alikuja kuwekwa miaka miwili baadae wakati hizo mali zote waliendelea kuzitumia smoothly as if EAC bado ipo ,wakati Tz na Uganda zikiumia kutafuta replacements ya zile zilizotoroshewa Kenya, Tanzania na Uganda ziliumia na hali hiyo. Sidhani kama utetezi wa maana sana, huyo rubani alisaidia kwa sababu inaonekana hiyo ndio ndege kubwa pekee tuliyoambulia.

..asante kwa mchango wako.

..ni kweli kwamba wakati jumuiya inavunjika nchi zetu zilikuwa ktk mahusiano mabaya.

..vilevile jumuiya haikuvunjika ghafla bin vu, dalili za jumuiya kuvunjika zilianza kuonekana kwa muda mrefu.

..siyo sahihi kusema kwamba kuvunjika kwa jumuiya ni tukio ambalo lilizishtukiza nchi wanachama.

..madai kwamba Kenya ilikuwa na mkakati wa kutorosha mali za jumuiya yanaweza kuwa na ukweli.

..kwa mfano, baada ya jumuiya kuvunjika, Kenya ilichukua ndege 14 za East African Airways, Tanzania ilichukua ndege 3, na Uganda haikupata ndege yoyote.

..Lakini pamoja na ukweli huo, mali na madeni ya jumuiya yalipogawanywa, aliyepata mali nyingi alilazimika kulipa zaidi ktk madeni, na aliyepata mali kidogo alibeba mzigo mdogo wa madeni.
 
Thanks Bro

Pamoja na kupigana na Uganda, Tanzania ilikua busy na ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika (Namibia, Angola, Zimbabwe, Afrika Kusini)
Resources nyingi zilipelekwa kuhudumia kambi za wapiganaji na familia zao

Kwa hiyo EAC ilionekana kama mzigo usio na manufaa kwa wananchi wa kawaida

kwa kuwa ilikua inanufaisha zaidi Kampuni kubwa zilizokuwa na uwezo wa kufanya cross border trade ambazo nyingi zilitokea Kenya na wamiliki wake ni Mabepari wenye asili ya nchi za Uingereza, Uholanzi na India.

Baada ya WW, Tanzania iliwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza, Hawa jamaa kwa kuwa walikua na interests zaidi hapo Nairobi, walitugeuza sisi soko la bidhaa zao from Kenya. Mfumo wa kutegemea bidhaa za Kenya ulianzia hapa.

Hata ilivyokuja EAC ilijitahidi kupunguza utegemezi wa viwanda vya Kenya lakini bado haikuwezekana.

So far situation ipo hivyo hivyo, EAC inanufaisha zaidi Kampuni kubwa za Kenya

Unga wa Bhakressa unaletewa zengwe kuingia Kenya

Kioo Limited nao walipigwa kodi za ajabu ajabu wasiweze kuingia Kenya

Konyagi nao wanapigwa zengwe kila siku

Tutaendelea hivi mpaka siku tukiweza kuwafundisha watoto wetu umuhimu wa kutumia bidhaa za Tanzania.

..Sisi Watanzania tunapenda sana kulalamika.

..EAC ya kwanza ilivunjika mwaka 1977.

..EAC mpya ilizaliwa mwaka 1999.

..Sasa tujiulize kwanini hatukujiimarisha ktk hiyo miaka 22 tuliyokuwa nje ya jumuiya?

..Halafu toka 1999 mpaka hivi tunavyozungumza ni miaka 20+ lakini bado Watanzania tuna malalamiko yaleyale kama ilivyokuwa mwaka 1977.

..Naipenda sana Tz na ninapenda tunufaike kutokana na mashirikiano na majirani zetu, lakini wakati mwingine nadhani Watanzania tunatumia muda mwingi kulalamika na hali hiyo inatuzuia kutafuta mbinu za kunufaika na fursa zilizoko ktk jumuiya.

cc Nguruvi3, Kichuguu
 
..Sisi Watanzania tunapenda sana kulalamika.

..EAC ya kwanza ilivunjika mwaka 1977.

..EAC mpya ilizaliwa mwaka 1999.

..Sasa tujiulize kwanini hatukujiimarisha ktk hiyo miaka 22 tuliyokuwa nje ya jumuiya?

..Halafu toka 1999 mpaka hivi tunavyozungumza ni miaka 20+ lakini bado Watanzania tuna malalamiko yaleyale kama ilivyokuwa mwaka 1977.

..Naipenda sana Tz na ninapenda tunufaike kutokana na mashirikiano na majirani zetu, lakini wakati mwingine nadhani Watanzania tunatumia muda mwingi kulalamika na hali hiyo inatuzuia kutafuta mbinu za kunufaika na fursa zilizoko ktk jumuiya.

cc Nguruvi3, Kichuguu
Mkuu nakubaliana nawe 101%. Watanzania bado wanalalamika kuhusu resources zilizotumika katika ukombozi
Nilishangaa sana watu na tena viongozi wakubwa tu wakisema muda wa kutumia rasilimali kwa wengine umepita

Ukweli kwa tulioona ni kwamba Tanzania haikutumia rasilimali kukomboa nchi za SADC.
Tanzania ilitoa hifadhi lakini siliha zilitoka nchi nyingine. Waliokwenda kutafuta ni Wapigania Uhuru, Tanzania iliwapa passport na logistic. Misaada ya wakimbizi ilitoka nje, Tanzania ilikuwa host tu wa Makambi ya wakimbizi

Lakini pia watu lazima waelewe, tulitumia rasilimali kidogo kwa usalama wetu.
Watu wa Mtwara wanajua hali ilikuwaje wakati huo Mreno akiwepo. Hivyo, tulikuwa na chaguo la kutafuta usalama au tukabiliane na madhila.Jiografia haikutuweka sawa na Kenya au Uganda.
Ushiriki wetu katika ukombozi ulikuwa kwa faida yetu.

Ukombozi ulitupa fursa ya SADC na ushirika na Zambia ilikuwa kielelezo cha awali.
Tumeshindwa kutumia fursa hizo sasa tunalalamika rasilimali za ukombozi.
Msumbiji ilikombolewa miaka 45 iliyopita ,tunalalama tu kwamba tumetumia rasilimali badala ya kutafuta fursa.

Tukirudi EAC nako ni kama JokaKuu alivyooeleza. Sisi tuna fursa ya kuwa wazalishaji wakubwa wa chakula na soko lipo tayari. Badala ya kuchangamkia fursa bado tunalalama Kenya na EAC ya 1977.

Katika EAC ya 1977 haukubeba mzigo wowote. Wakati tunatumia bidhaa za Maswiani na Jinja, Blue Band na Lifebuoy etc Nyerere alianza kutujengea uwezo wa viwanda ambavyo tulishindwa kuviendeleza na kuviuza kama si kugeuza maghala. Kenya au Uganda wanahusika vipi?

Tumezidi kulalamika hatuna new ideas. Watanzania siyo creative kwa namna nyingi.
Hatuwezi kuishi kwa historia, lazima tubadilike! tuwe wabunifu na tuelewa majirani zetu si maadui ni washindani

Jiulize kwanini Kahawa ilimwe Kagera , soko liwe Uganda? Kwanini Iliki ilimwe K'njaro soko liwe Kenya?

Kwanini tuagize mchele Korea badala ya Kenya na Uganda kuagiza kutoka Mbarali?

Kwanini mahindi yaoze maghalani Mbeya wakati Kenya kuna njaa? wakati Burundi na Kongo wanahitaji?

Kwanini tupige debe la SGR ya Mwanza halafu tushindwe kutumia SGR ya Tazara kusafirisha bidhaa?

Tukwama wapi ku negotiate na Zambia hata kama ni kuwalipa kidogo ili tunafaike zaidi?

Tuache kulalama, tunakiwa tukimbie na wenzetu .
 
..kwanini Waganda hawako bitter na jinsi jumuiya ilivyovunjika mwaka 1977 kulinganisha na sisi Watanzania?

..au kwanini Waganda hawana hofu na jumuiya mpya kulinganisha na Watanzania tunavyoiogopa jumuiya?

..kwanini Watanzania hatuko tayari ku-embrace / ku-dominate jumuiya mpya ya afrika mashariki wakati tulikuwa na miaka 43+ ya kujiandaa toka 1977 mpaka 2021?
 
Back
Top Bottom