Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,600
- 218,001
Hii ni kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa CCM, Mh Chongolo alipokuwa anatoa takwimu za usajili wa wanachama wa CCM kwa njia ya kisasa, katika maadhimisho ya miaka 45 ya chama hicho huko Mkoani Mara, ametumia pia muda huo kumkabidhi kadi ya kidigitali mwenyekiti wake Samia Suluhu Hassan (Kumbe naye alikuwa hana!)
Hapa ndio ambapo unaweza kujiuliza, inakuwaje CCM yenye facilities zote inakwama kusajili wanachama wake kidigitali , Lakini CHADEMA yenye kesi kwenye Mahakama zote nchini Tanzania imeweza kusajili kidigitali wanachama zaidi zaidi ya milioni 12.7?
Tatizo la CCM liko wapi? Je, watu wameichoka kutokana na uduni wa maisha unaoongezeka kwa kasi , na kuifanya ccm kuwa chama cha viongozi pekee na watoto wao au kuna lingine?
Hapa ndio ambapo unaweza kujiuliza, inakuwaje CCM yenye facilities zote inakwama kusajili wanachama wake kidigitali , Lakini CHADEMA yenye kesi kwenye Mahakama zote nchini Tanzania imeweza kusajili kidigitali wanachama zaidi zaidi ya milioni 12.7?
Tatizo la CCM liko wapi? Je, watu wameichoka kutokana na uduni wa maisha unaoongezeka kwa kasi , na kuifanya ccm kuwa chama cha viongozi pekee na watoto wao au kuna lingine?