Wakati CCM wanaimarisha wadhamini, Wapinzani wameanza kuwatukana wadhamini.

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Kushinda Uchaguzi wa siasa na kushika dola unahitaji udhamini wa makundi muhimu katika jamii. Haijalishi unashinda kwa kuiba kura au kutoiba kura lakini la muhimu sana kama hujapata udhamini wa makundi muhimu katika jamii huwezi kushinda kura na kuchukua dola.

Kila nchi inatofautiana kuhusu aina ya makundi muhimu ya wadhamini yanayopelekea kushinda uchaguzi mkuu na kushika dola. Kwa mfano katika nchi ya Uingereza, makundi muhimu ya wadhamini ambayo huwezi kuyadharau ni mashoga na wayahudi. Ukidharau hata kundi moja katika haya mawili basi usahau pia kushinda uchaguzi na kushika dola.

Kwa Tanzania ukikumbatia kundi la Ushoga kuna uwezekano mkubwa huwezi kushinda Uchaguzi Mkuu na kushika dola. Hata hivyo Tanzania hatuna kundi kubwa la Wayahudi na kwa mantiki hii sio kigezo katika mustakabali wa uchaguzi mkuu.

Makundi ya udhamini kwa Tanzania ambayo ni muhimu sana kukumbatia wakati wa Uchaguzi Mkuu ili ushinde na kushika dola ni kundi la madhehebu ya dini na pia wananchi wanaoishi vijijini na mjini ambao wana kipato cha chini.

CCM kwa kutambua umuhimu huu ndio maana wameanza kujiimarisha kwenye haya makundi wakati wapinzani wakianza kuyadharau na kuyatukana.

Hii imeonekana baada ya Rais Magufuli kukutana na makundi ya madhehebu ya dini na wachimbaji wadogo wa madini na wafanya biashara ndogo ndogo.

Viongozi wa Upinzani ambao wengine ni wajumbe wa Kamati Kuu za vyama vyao wamejitokeza na kuanza kuyashambulia makundi haya mpaka wengine wanayatukana.

Tumewasikia kina Godbless Lema, Peter Msigwa, Halima Mdee, John Heche na Boniface Jacob ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wakiwatukana viongozi wa madhehebu ya dini baada ya kukutana na Rais Magufuli.

Mashambulizi haya hayawasaidii wapinzani bali yanaisaidia sana CCM kuzidi kujiimarisha zaidi kadri Uchaguzi Mkuu unavyokaribia. Kwa mwendo huu 2020 itakuwa hali mbaya sana kwa wapinzani.

GONGA LINK>>>Askofu Kakobe: Viongozi wa CHADEMA watubu hadharani kwa kuwatukana viongozi wa dini

Kwa mfano, nchi masikini kama Tanzania huwezi kupata wanaojitoa mhanga kuandamana kwa kutegemea pekee kundi/tabaka aali (elite). Hili ni tabaka ambalo lilichonacho ni kikubwa zaidi ya kitacholifanya liandamane. Hili ni kundi linaongea sana lakini matendo ni zero. Kwa mfano Godbless Lema wa sasa sio yule wa kabla hajapata ubunge. Lema wa sasa ameingia kwenye kundi la aali (elite) na kwa sababu hii huwezi kumuona eti anahamasisha maandamano ‘’haramu’’. Alichonacho kwa sasa ni zaidi ya kile atakipata kwenye maandamano ‘’haramu’’.

Aliyekuwa Rais wa DRC, Joseph Kabila amlipigwa kwa nguvu kuongeza muhula mwingine wa utawala na makundi hayo muhimu niliyoyataja na sio kundi la aali (elite). Makundi ya madhehebu ya dini na wananchi masikini walijitokeza kwenye maandamano bila kujali athari zao kimaisha kwa sababu hakuna walichokuwa wanapoteza katika maandamano mpaka Rais Kabila akaondoa nia hiyo.

Niliwahi kusema kwenye Thread hii,
GONGA LINK>>>Nape na Bashe wamewapa CHADEMA somo la siasa za CCM

Tumeona kwenye chaguzi ndogo ambapo wale wanachama wa CCM ambao walidhaniwa kuwa ni ‘’waasi ndani ya CCM’’ walijitokeza na kuongoza kampeni za CCM katika chaguzi hizo wakati wapinzani wakishindwa hata kuungana na kusimamia mgombea mmoja.

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wapinzani hufarakana wakati CCM huungana na hujiimarisha kwa sababu wanajua umuhimu wake. Hii imeanza kujitokeza.

Siasa sio jazba bali ni sayansi ambayo ina misingi yake kutokana na mazingira. Huwezi kufanikiwa kisiasa kama unadharau misingi yake.

CCM pamoja na mapungufu yao lakini wanajua maana ya sayansi ya siasa katika mazingira ya Tanzania.
 
Kushinda Uchaguzi wa siasa na kushika dola unahitaji udhamini wa makundi muhimu katika jamii. Haijalishi unashinda kwa kuiba kura au kutoiba kura lakini la muhimu sana kama hujapata udhamini wa makundi muhimu katika jamii huwezi kushinda kura na kuchukua dola.

Kila nchi inatofautiana kuhusu aina ya makundi muhimu ya wadhamini yanayopelekea kushinda uchaguzi mkuu na kushika dola. Kwa mfano katika nchi ya Uingereza, makundi muhimu ya wadhamini ambayo huwezi kuyadharau ni mashoga na wayahudi. Ukidharau hata kundi moja katika haya mawili basi usahau pia kushinda uchaguzi na kushika dola.

Kwa Tanzania ukikumbatia kundi la Ushoga kuna uwezekano mkubwa huwezi kushinda Uchaguzi Mkuu na kushika dola. Hata hivyo Tanzania hatuna kundi kubwa la Wayahudi na kwa mantiki hii sio kigezo katika mustakabali wa uchaguzi mkuu.

Makundi ya udhamini kwa Tanzania ambayo ni muhimu sana kukumbatia wakati wa Uchaguzi Mkuu ili ushinde na kushika dola ni kundi la madhehebu ya dini na pia wananchi wanaoishi vijijini na mjini ambao wana kipato cha chini.

CCM kwa kutambua umuhimu huu ndio maana wameanza kujiimarisha kwenye haya makundi wakati wapinzani wakianza kuyadharau na kuyatukana.

Hii imeonekana baada ya Rais Magufuli kukutana na makundi ya madhehebu ya dini na wachimbaji wadogo wa madini na wafanya biashara ndogo ndogo.

Viongozi wa Upinzani ambao wengine ni wajumbe wa Kamati Kuu za vyama vyao wamejitokeza na kuanza kuyashambulia makundi haya mpaka wengine wanayatukana.

Tumewasikia kina Godbless Lema, Peter Msigwa, Halima Mdee, John Heche na Boniface Jacob ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wakiwatukana viongozi wa madhehebu ya dini baada ya kukutana na Rais Magufuli.

Mashambulizi haya hayawasaidii wapinzani bali yanaisaidia sana CCM kuzidi kujiimarisha zaidi kadri Uchaguzi Mkuu unavyokaribia. Kwa mwendo huu 2020 itakuwa hali mbaya sana kwa wapinzani.

Kwa mfano, nchi masikini kama Tanzania huwezi kupata wanaojitoa mhanga kuandamana kwa kutegemea pekee kundi/tabaka aali (elite). Hili ni tabaka ambalo lilichonacho ni kikubwa zaidi ya kitacholifanya liandamane. Hili ni kundi linaongea sana lakini matendo ni zero. Kwa mfano Godbless Lema wa sasa sio yule wa kabla hajapata ubunge. Lema wa sasa ameingia kwenye kundi la aali (elite) na kwa sababu hii huwezi kumuona eti anahamasisha maandamano ‘’haramu’’. Alichonacho kwa sasa ni zaidi ya kile atakipata kwenye maandamano ‘’haramu’’.

Aliyekuwa Rais wa DRC, Joseph Kabila amlipigwa kwa nguvu kuongeza muhula mwingine wa utawala na makundi hayo muhimu niliyoyataja na sio kundi la aali (elite). Makundi ya madhehebu ya dini na wananchi masikini walijitokeza kwenye maandamano bila kujali athari zao kimaisha kwa sababu hakuna walichokuwa wanapoteza katika maandamano mpaka Rais Kabila akaondoa nia hiyo.

Niliwahi kusema kwenye Thread hii,
GONGA LINK>>>Nape na Bashe wamewapa CHADEMA somo la siasa za CCM

Tumeona kwenye chaguzi ndogo ambapo wale wanachama wa CCM ambao walidhaniwa kuwa ni ‘’waasi ndani ya CCM’’ walijitokeza na kuongoza kampeni za CCM katika chaguzi hizo wakati wapinzani wakishindwa hata kuungana na kusimamia mgombea mmoja.

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wapinzani hufarakana wakati CCM huungana na hujiimarisha kwa sababu wanajua umuhimu wake. Hii imeanza kujitokeza.

Siasa sio jazba bali ni sayansi ambayo ina misingi yake kutokana na mazingira. Huwezi kufanikiwa kisiasa kama unadharau misingi yake.

CCM pamoja na mapungufu yao lakini wanajua maana ya sayansi ya siasa katika mazingira ya Tanzania.
Mkuu japo umeongea mambo mazito utaloweshwa matusi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu;
Mimi wala huwa sijali mtu anayetukana kwa sababu hanijui na simjui.

Wakati mwingine huwa ninatumia dhana ya mapigano inayosema, fight fire with fire katika kukabiliana na matusi ya watu wajinga wajinga

Kwenye post yako namba 1 ndio umeongea ukweli. Haijalishi unashinda kwa kuiba au vipi. Mengine ni blanla. Hiki wanachokifanya ccm sasa kupitia madaraka ya urais ni kutakatisha kura chafu hiyo 2020. Cdm hawana cha kuwabembeleza hao viongozi wa dini zaidi ya kuwapa ukweli wao. Ccm ndio ina hofu ya kukubalika hivyo inabidi ijipendekeze.
 
Kwenye post yako namba 1 ndio umeongea ukweli. Haijalishi unashinda kwa kuiba au vipi. Mengine ni blanla. Hiki wanachokifanya ccm sasa kupitia madaraka ya urais ni kutakatisha kura chafu hiyo 2020. Cdm hawana cha kuwabembeleza hao viongozi wa dini zaidi ya kuwapa ukweli wao. Ccm ndio ina hofu ya kukubalika hivyo inabidi ijipendekeze.
Hoja yako nimeishaijibu katika bandiko langu.

Hao wapinzani watapata wapi hizo nguvu za umma (Peoples Power) kama wanawatukana wenye mizizi ya nguvu za umma. Ndio maana tunasema mwaka 2020 ni kifo cha upinzani nchini.

Hakuna cha maandamano wala uungwaji mkono katika harakati zao za upinzani hata kama ''wataibiwa kura''.
 
Mkuu mtoa mada;kwani kuna kipindi ccm ilikua na ugomvi na wadhamini?kwa akili ya kawaida kinachofanywa na mh rais ni afya kwa nchi?

Je kila kada waombe nafasi kuongea na mh Rais ikulu....kuanzia kwa watoto...vijana...walemavu....walimu n.k. Iwapo rais anaona watendaje hawatendi ipasavyo insbidi awaite watendaje na kuwauliza tatzo ni nini.
 
Hoja yako nimeishaijibu katika bandiko langu.

Hao wapinzani watapata wapi hizo nguvu za umma (Peoples Power) kama wanawatukana wenye mizizi ya nguvu za umma. Ndio maana tunasema mwaka 2020 ni kifo cha upinzani nchini.

Hakuna cha maandamano wala uungwaji mkono katika harakati zao za upinzani hata kama ''wataibiwa kura''.

Unachekesha walionuna, hao viongozi wa dini Magufuli anawataka wajipendekeze kwake tu, wakiongea au kuwa jaribu na wapinzani wanaambiwa wanachanganya siasa na dini. Aina ya siasa za Magufuli tunazijua hata hao viongozi wa dini wanamjua hivyo wanapretend kumkubali.
 
yeah itashangaza sana kama viongozi wa dini watu ambao kwa namna yoyote tunategemea kweli yenye ujasiri inaishi na wao, kumbe nao wakuwa wanaliwa timing tu na wanasiasa na kutekwa akili zao. Kama viongozi wa dini watashindwa kuisimamia kweli hakuna namna nyingine ,watu wengine pengine hata wasioijua dini watainuliwa na Mungu ili waisimamie Kweli yenye ukweli,
 
Kwenye post yako namba 1 ndio umeongea ukweli. Haijalishi unashinda kwa kuiba au vipi. Mengine ni blanla. Hiki wanachokifanya ccm sasa kupitia madaraka ya urais ni kutakatisha kura chafu hiyo 2020. Cdm hawana cha kuwabembeleza hao viongozi wa dini zaidi ya kuwapa ukweli wao. Ccm ndio ina hofu ya kukubalika hivyo inabidi ijipendekeze.
yeah itashangaza sana kama viongozi wa dini watu ambao kwa namna yoyote tunategemea kweli yenye ujasiri inaishi na wao, kumbe nao wakuwa wanaliwa timing tu na wanasiasa na kutekwa akili zao. Kama viongozi wa dini watashindwa kuisimamia kweli hakuna namna nyingine ,watu wengine pengine hata wasioijua dini watainuliwa na Mungu ili waisimamie Kweli yenye ukweli,
 
Mkuu mtoa mada;kwani kuna kipindi ccm ilikua na ugomvi na wadhamini?kwa akili ya kawaida kinachofanywa na mh rais ni afya kwa nchi?

Je kila kada waombe nafasi kuongea na mh Rais ikulu....kuanzia kwa watoto...vijana...walemavu....walimu n.k. Iwapo rais anaona watendaje hawatendi ipasavyo insbidi awaite watendaje na kuwauliza tatzo ni nini.
Nimeandika wanaimarisha wadhamini. Hii ina maana kuwa walikuwa na wadhamini.

Kwa mfano ukisikia timu fulani inaimarisha kikosi cha washambuliaji haina maana kuwa timu ilikuwa haina washambuliaji.

Kama alivyofanya Rais ni afya au sio afya kwa nchi, hilo ni suala lingine ambalo ni relative.
 
Hoja yako nimeishaijibu katika bandiko langu.

Hao wapinzani watapata wapi hizo nguvu za umma (Peoples Power) kama wanawatukana wenye mizizi ya nguvu za umma. Ndio maana tunasema mwaka 2020 ni kifo cha upinzani nchini.

Hakuna cha maandamano wala uungwaji mkono katika harakati zao za upinzani hata kama ''wataibiwa kura''.
Uchaguzi ujao upinzani una wakati mgumu. 2015 angalau waliungana na kushambulia kama Ukawa lakini safari hii kila mmoja ana lake. Huku Lisu, huku Zitto, huku sijui nani. Sidhani kama upepo wa Lowassa utavuma tena kipindi kijacho.
 
Nimeandika wanaimarisha wadhamini. Hii ina maana kuwa walikuwa na wadhamini.

Kwa mfano ukisikia timu fulani inaimarisha kikosi cha washambuliaji haina maana kuwa timu ilikuwa haina washambuliaji.

Kama alivyofanya Rais ni afya au sio afya kwa nchi, hilo ni suala lingine ambalo ni relative.

Hakuna kiongozi wa dini anathubutu kuongea mbele ya kiongozi ambaye matumizi ya bunduki, mauaji na kutekwa wasiomsujudia ni kawaida. Hapo hawana namna zaidi ya kwenda kuongelea yale ambayo hayatamkwaza. Hatuna cha kuwalaumu viongozi wa dini maana hawana choice zaidi ya aidha wajipendekeze au wakae mbali na wapinzani.
 
Aina ya siasa za Magufuli tunazijua hata hao viongozi wa dini wanamjua hivyo wanapretend kumkubali.
Mara hii umeshakuwa mpiga ramli!

Sasa kama wanampretend kumkubali mbona wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wametokwa na mapovu huku wengine wakiwatukana!

Ina maana unajua wewe tu kuwa wanampretend lakini viongozi wakuu wa CHADEMA hawajui!
 
Hivi tunatarajia nini wakati uwanja wa siasa kaudhibiti ccm pekee,anafanya mikutano,anaimarisha chama,anatumia fund za serikali kujenga ccm. Wakati huohuo upinzani uko jela,viongozi wake wanafunguliwa kesi na wengine kupandikiziwa viongozi feki akina lipmba na kesi iko mahakamani ,kila siku date.
MIMI NADHANI UPINZANI USUSIE CHAGUZI ZOTE NA WANANCHI WEMA WAACHANE KABISA KUPIGA KURA.HERI HUYU JIWE APITE BILA KUPINGWA NA BUNGENI WABAKI PEKEYAO.WAFANYE WATAKAVYO.SISI TUTAFUTE ALTERNATIVES. Tukifanya boycot italeta faida na raia tutakuwa salama na kutiwa kwenye viroba hakutakuwepo.TELL HIM NOTHING BUT SILENCE PROTESTS.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye post yako namba 1 ndio umeongea ukweli. Haijalishi unashinda kwa kuiba au vipi. Mengine ni blanla. Hiki wanachokifanya ccm sasa kupitia madaraka ya urais ni kutakatisha kura chafu hiyo 2020. Cdm hawana cha kuwabembeleza hao viongozi wa dini zaidi ya kuwapa ukweli wao. Ccm ndio ina hofu ya kukubalika hivyo inabidi ijipendekeze.
Kwanini ijipendekeze nao wana uhakika wa ushindi kwa kuiba kura kama walivyo Cdm na uhakika wa kushindwa ndio maana haibembelezi!
 
Mara hii umeshakuwa mpiga ramli!

Sasa kama wanampretend kumkubali mbona wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wametokwa na mapovu huku wengine wakiwatukana!

Ina maana unajua wewe tu kuwa wanampretend lakini viongozi wakuu wa CHADEMA hawajui!

Wamewapa ukweli wao hao viongozi kwamba kujipendekeza hakuwatoi. Simply Magu hajui siasa hasa za ushindani zaidi ya kutumia madaraka kuhakikisha kila mtu anamsujudia. Na hiyo unaayosema ccm, kwa taarifa yako hakuna ccm bali kundi linalotegemea nguvu na madaraka ya rais kufanya siasa na nafasi ya kupatia madaraka.
 
Hoja yako nimeishaijibu katika bandiko langu.

Hao wapinzani watapata wapi hizo nguvu za umma (Peoples Power) kama wanawatukana wenye mizizi ya nguvu za umma. Ndio maana tunasema mwaka 2020 ni kifo cha upinzani nchini.

Hakuna cha maandamano wala uungwaji mkono katika harakati zao za upinzani hata kama ''wataibiwa kura''.
Hakuna mtanzania mwenye kumuogopa Mungu anayeweza kuheshimu wale wachungaji na Mashehe waoga wanaomkiri Shetani huku wakijua mauaji aliyoyafanya na kuua demokrasia , mtoa rushwa anayenunua binadamu wenzake , huku akiwatukana matusi ya nguoni waliopata majanga badala ya kuwafariji .

Itakuwa aibu kubwa sana kwa Muumini wa kweli kuheshimu watu wale
 
Hakuna kiongozi wa dini anathubutu kuongea mbele ya kiongozi ambaye matumizi ya bunduki, mauaji na kutekwa wasiomsujudia ni kawaida. Hapo hawana namna zaidi ya kwenda kuongelea yale ambayo hayatamkwaza. Hatuna cha kuwalaumu viongozi wa dini maana hawana choice zaidi ya aidha wajipendekeze au wakae mbali na wapinzani.
Kama hakuna kiongozi wa dini mbona viongozi wa dini wa DRC wamethubutu. DRC is even worse than Tanzania mpaka Rais wa nchi anaapishwa huku amevaa bulletproof vest.

Mkuu acha kujifariji kwa mambo ambayo huhitaji kutumia akili kubwa kujua ukweli wake.

Wapinzani hawana ushawishi kwa makundi muhimu nchini badala yake wanayadharau na kuyatukana.
 
Kwanini ijipendekeze nao wana uhakika wa ushindi kwa kuiba kura kama walivyo Cdm na uhakika wa kushindwa ndio maana haibembelezi!

Hapo wanatakatisha tu wizi wa kura ili wakijitangaza ionekane wanakubalika. Cdm haina uhakika wa kutangazwa ila sio ushindi kwani hawana sauti juu ya vyombo vya dola.
 
Back
Top Bottom