Wakali wa hesabu!!!

Mzee

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
13,596
5,787
Salaam wana JF
Kuna swali juzi nimeulizwa na mtoto angu mdogo. Sikuweza kumjibu vizur. Ktk saa, mfano saa mbili kwa kiswahili ni 2 ila kwa kizungu ni 8. Akaniuliza sababu gani inayofanya namba ktk saa zibadilike kutokana na lugha, na kwanini iwe ktk masaa tu na wala si ktk dk na sekunde?..
Ila msinicheke mwenzenu. Nisaidieni!!
 
huyo mwanao ana umri gani?!!!! mwambie ni utaratibu tu uliowekwa na wagunduzi.....
 
Kwasababu mshale wa saa tunausoma katika opposite direction. Yaani ule mshale ingebidi uwe mrefu ila ungezuia mshale wa dakika.
Nenda kwenye saa ya ukutani utaelewa ninachokimaanisha.
Ukikosa jibu mjibu hvyo mwanao jibaba usiaibike.
 
Kwasababu mshale wa saa tunausoma katika opposite direction. Yaani ule mshale ingebidi uwe mrefu ila ungezuia mshale wa dakika.
Nenda kwenye saa ya ukutani utaelewa ninachokimaanisha.
Ukikosa jibu mjibu hvyo mwanao jibaba usiaibike.

na hizi saa za "kimwekumweku", Digital nazo zina mishale?
 
<br />
<br />
saa za kwanza kugunduliwa ni zipi?

saa za kwanza kugundulika ni zile zilizokuwa zinatumia heavy Liquid (Hasa Mercury) kwenye tube, kwa hiyo drop moja moja ilikuwa inadondoka na baada ya masaa sita inageuzwa kwenda upande wa pili
 
Kwa mzungu mwanzo wa siku ni saa sita usiku hivo hadi "kunakucha" keshahesabu masaa sita. Sisi waswahili siku mpya inaanza jua linapochomoza saa kumi na mbili(mwisho wa usiku wenye jumla masaa kumi na mbili) Mchana nao masaa kumi na mbili hadi jua linatua. Kimsingi mfumo wa saa wa kiswahili una reflect hali halisi ya muda kuliko mfumo kizungu,hayo mawazo yangu tu.
 
  • Thanks
Reactions: mja
kwa mzungu ile 8 ni saa nane kweli, kwanza waaanza kuhesabu usiku, wao wansema one.. in the ,morning (morning yao ni mpaka 11:59) kwa hiyo saa moja yao ni usiku ule, kwa waswahili saa moja yetu ni iles asubuhi wakati wao ni saa saba yao. seven oclok.
 
Mimi nadhani waliamua kufanya hivyo ili kuzuia watu wasilale sana. Kwasababu walijua waafrika ni wavivu sana kwahiyo ukiwaachia wasome saa kwa kiswahili wataendekeza starehe na bia tu mpaka asubuhi.
 
Kwa mzungu mwanzo wa siku ni saa sita usiku hivo hadi "kunakucha" keshahesabu masaa sita. Sisi waswahili siku mpya inaanza jua linapochomoza saa kumi na mbili(mwisho wa usiku wenye jumla masaa kumi na mbili) Mchana nao masaa kumi na mbili hadi jua linatua. Kimsingi mfumo wa saa wa kiswahili una reflect hali halisi ya muda kuliko mfumo kizungu,hayo mawazo yangu tu.

Mkuu Simplemind hilo ndilo jibu sahihi kabisa.

Unajua kiswahili kimetohoa maneno mengi ya kiarabu na baadhi ya Culture za kiarabu na za middle East kwa ujumla
utamaduni uliokuwepo middle East ni kuwa siku inaanzia asubuhi (Mchomoko wa jua) na kuishia jioni (Mzamo wa jua) hiyo huwa ni siku moja, na kuanzia jua kuzama mpaka kuchomoza ni siku nyingine,

kwa hiyo hesabu yao inaanzia asubuhi na kuishia jioni (refer to Sabath day), huo utaratibu ndio ulikuja Tanzania kupitia Waarabu kuwa siku inaanzia asubuhi, hivyo inakuwa saa moja asubuhi na kuishia saa kumi na mbili jioni na kisha siku nyingine inaanza na saa moja usiku na kuishia saa kumi na mbili alfajili,

Wazungu wao siku yao inaanzia saa sita usiku na kuishia saa tano na dakika 59 na sekunde kadhaa usiku,

Sasa Watanzania tukazichukua taratibu zote mbili (za kizungu na za kiarabu/Middle east), hivyo basi siku ya kizungu inapoanza na saa moja (Saa saba ya usiku kiswahili) mpaka inapokuja kukutana na saa moja ya Kiarabu(Kiswahili) yeye atakuwa na 0700hrs na Waswahili tutakuwa na 1.00kamili Asubuhi Hapa ndipo kwenye hoja ya mtoa mada

na sababu sio saa za mishale wala Crockwise na Anticrockwise kamawachangiaji wengine walivyosema
 
huyo mwanao ana umri gani?!!!! mwambie ni utaratibu tu uliowekwa na wagunduzi.....
nyi ndo mnafanya watoto wawe kama nape nauye yaani unam-traini kuto reason asee ,wagunduzi ndo kina nani ? wananini tofauti na mtoto huyu ? ,....kama ni mimi ninge admit sijui na kumwahidi kutafuta sababu ,hii inamjenga mtoto kujua yeye anawajibu wa ku formulate nini kinachodhaniwa ukweli na jamii na si mtekelezaji wa fikra za wengine
 
nyi ndo mnafanya watoto wawe kama nape nauye yaani unam-traini kuto reason asee ,wagunduzi ndo kina nani ? wananini tofauti na mtoto huyu ? ,....kama ni mimi ninge admit sijui na kumwahidi kutafuta sababu ,hii inamjenga mtoto kujua yeye anawajibu wa ku formulate nini kinachodhaniwa ukweli na jamii na si mtekelezaji wa fikra za wengine

Haya ndio yale ya Mzungu kagundua Mlima Kilimanjaro, Au kagundua Ziwa Victoria
 
Kama wachangiaji wengi walivyosema, siku moja ina masaa 24, na inaanza usiku, yaani 0000hrs, ni saa kamili usiku na 0100hrs ni saa saba usiku hadi kunakucha ni 0600hrs ambayo sisi tunasema saa 12 asubuhi na hiyo aliyotaja mtoa mada 0800hrs ndo saa mbili asubuhi lakini kiuhalisia siku tajwa itakuwa tayari ishakata masaa manane toka ianze.
 
nyi ndo mnafanya watoto wawe kama nape nauye yaani unam-traini kuto reason asee ,wagunduzi ndo kina nani ? wananini tofauti na mtoto huyu ? ,....kama ni mimi ninge admit sijui na kumwahidi kutafuta sababu ,hii inamjenga mtoto kujua yeye anawajibu wa ku formulate nini kinachodhaniwa ukweli na jamii na si mtekelezaji wa fikra za wengine
<br />
<br />
thats true. Niliona swali lake lina logical ambayo mimi baba yake nilishindwa kuigundua. Nilimwambia kuwa nimechoka ila leo jioni nitamjibu, kwan swal lake linahitaji maelezo marefu.
 
Back
Top Bottom