Wakaguzi wa mifuko ya plastiki wapewa muongozo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Picha

OFISI ya Makamu wa Rais imetoa mwongozo wenye vipengele tisa kwa wakaguzi na watekelezaji wa katazo la mifuko ya plastiki katika halmashauri zote nchini, utakaoanza kutumia Juni mosi mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Mei 23, mwaka huu, wakaguzi wameagizwa kutumia busara kutekeleza agizo hilo huku matumizi ya nguvu ikiwamo kuwapiga au kuwabeba watu na kuwaweka ndani yakikatazwa.

Kwa mujibu wa mwongozo huo, vipengele hivyo ni kuwataka wakaguzi kufanya ukaguzi huo madukani, magengeni, viwandani, masokoni, mipakani, kwenye maduka makubwa na maeneo mengine yanayouza bidhaa.

Kipengele cha pili cha mwongozo huo ni kuwataka wakaguzi wote wajitambulishe na kuonesha vitambulisho vyao kwa wahusika kwenye maeneo wanayokagua, huku ukiwakataza wakaguzi kuwasimamisha watu au mtu na kumpekua au kupekua migizo yake ili kutafuta mifuko ya plastiki.

Vilevile, mwongozo huo unamkataza mkaguzi kutoingia kwenye makazi ya watu au kusimamisha magari au vyombo vingine vya usafiri ili kutafuta mifuko hiyo.

Taarifa hiyo ya Ofisi ya Makamu wa Rais ilisema, lakini iwapo magari au vyombo vingine vya usafiri vitasimamishwa kwa sababu nyingine na kukutwa na shehena ya mifuko ya plastiki, adhabu stahiki itatolewa na wahusika wataelekezwa mahali mahususi kwa kupeleka shehena hiyo.

Aidha, ilisisitiza kuwa atakayekutwa na kosa la kuendelea kuuza, kuhifadhi au kutumia mifuko hiyo ya plastiki kuanzia Juni Mosi, mwaka huu, ataelekezwa mahali pa kuipeleka kisha atapigwa faini na kupewa muda wa kulipa na iwapo atakataa kusaini au kushindwa kulipa katika muda aliopewa, atafunguliwa mashitaka.

Kadhalika, watakaotozwa au kulipa faini watapewa risiti za serikali kwa malipo hayo na pia mwongozo huo ukiwaonya pia wale wote watakaokaidi kwa kutotoa ushirikiano katika ukaguzi huo, kuzuia au kuhujumu utekelezaji wake, kuwa watachukuliwa hatua kali zaidi kwa mujibu wa sheria nyingine za nchi.

Aprili mwaka huu serikali ilitoa taarifa rasmi ya katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki litakaloanza kutumika Juni Mosi, mwaka huu na kuwataka wazalishaji, wauzaji na wanunuzi kutumia mifuko mbadala. Sambamba na hilo, pia elimu imeendelea kutolewa kuhusu matumizi mbadala wa mifuko hiyo na kuwataka wafanyabiashara na wajasiriamali kutumia fursa hiyo kuzalisha mifuko rafiki wa mazingira.
 
Muda wa kuanza kutembea na vikapu umewadia. Hakuna namna. Shughuli itakuwa kwenye ununuzi wa nyama. Ile mifuko ya karatasi nadhani haitakuwa rafiki kabisa.
 
Enzi zile za miaka ya 80's tulitumia mofuko ya karatasi au magazeti kubebea nyama.
Mifuko ya karatasi ilikua inatengenezwa na mifuko ya cement na ilikia inatengenezwa mitaani watu wanapata rizki zao.

Zoezi la kwanza ukishanunua nyama ni kubandua hiyo karatasi kabla hujaanza kuikata na kuipika
Muda wa kuanza kutembea na vikapu umewadia. Hakuna namna. Shughuli itakuwa kwenye ununuzi wa nyama. Ile mifuko ya karatasi nadhani haitakuwa rafiki kabisa.
 
Makatazo-rafiki kama haya tulishayasahau sikuhizi ni ubabe,vitisho na vifungo Tu...
Asante January makamba Kwa kuwa msikivu
 
Enzi zile za miaka ya 80's tulitumia mofuko ya karatasi au magazeti kubebea nyama.
Mifuko ya karatasi ilikua inatengenezwa na mifuko ya cement na ilikia inatengenezwa mitaani watu wanapata rizki zao.

Zoezi la kwanza ukishanunua nyama ni kubandua hiyo karatasi kabla hujaanza kuikata na kuipika
Kwaio unataka miaka ya themanini irudi 2019
 
Kuna bidhaa tunazo hemea zinazotoka china zimefungwa na mifuko ya plastiki mojakwa kwamoja je? hapo inakueje au kunautaratibu gani
 
Enzi zile za miaka ya 80's tulitumia mofuko ya karatasi au magazeti kubebea nyama.
Mifuko ya karatasi ilikua inatengenezwa na mifuko ya cement na ilikia inatengenezwa mitaani watu wanapata rizki zao.

Zoezi la kwanza ukishanunua nyama ni kubandua hiyo karatasi kabla hujaanza kuikata na kuipika
Siku hizi maendeleo yameleta mageuzi. Kuna makaratasi special kwa kufungia nyama au kuwekea vyakula.
 
Zoezi La kukurupuka utadhani Tz pekee ndo utumia mifuko ya plastic labda tu kama 10% tayari kwenye mifuko mbadala.
 
Wao wangezalisha Kwa wingi mifuko mbadala wakaiachia ikaingia Sokoni kushindana,
Kukamata watu ni sawa Na kuwakamata wavuvi hali wao si wazalishaji nyavu wanashindwa zuia uzalishaji viwandani,automatic mitaani itapotea
_labda tu kama lengo ni kutaka kupata Pesa tokana Na kukamata watu
-Ni heri niichome moto kuliko kuisalimisha kama narudishiwa hela sawa.
_Tungewafundisha wanafunzi kutengeneza madawati tokana Na mifuko chakavu ya plastic ingesaidia kuondoa kuzagaa Kwa plastic mtaani.
_taka za plastic wawekeza tengeneza dizeli,petrol, mafuta ya taa, tofali,vigae,mabati ya kuezeka,lami,nk hii ingesaidia kuondoa plastic mtaani.
_tuwezacho ni marufuku, makatazo hatuna ubunifu kujifunza kutengeneza fursa tokana Na taka.
 
Sjui kama wamewaskia.....
Kama nawaona vile wagambo na PT
Wakatavyo kamata watu+mitama

Ova
 
Back
Top Bottom