Wakaguzi wa dhahabu wagundua upungufu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Wakaguzi wa dhahabu wagundua upungufu
Raymond Mihayo, Kahama
Daily News; Monday,November 17, 2008 @20:00

Kitengo cha Ukaguzi wa Dhahabu (GAP), kimebaini upungufu mkubwa katika mikataba ya uchimbaji wa madini ya dhahabu katika migodi ya Bulyanhulu, Geita ambayo imekuwa ikiipatia serikali hasara.

Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Utawala cha Ukaguzi wa Dhahabu katika migodi mikubwa nchini, Bruno Mteta alipozungumza na viongozi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa Bulyanhulu.

Alizungumza hayo katika Kijiji cha Kakola wilayani hapa juu ya programu ya uelimishaji wa umma mkoani Shinyanga juu ya migodi mikubwa ya dhahabu. Mteta alikuwa akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na viongozi hao waliowawakilisha wananchi wao walipohoji mikataba na upungufu uliokwishabainika kupitia ukaguzi wa kitengo hicho kilichoanzishwa Agosti mwaka jana.

Alisema baada ya kitengo hicho kuanza ukaguzi katika mgodi wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Barrick Gold Corporation na Geita Gold Mine mali ya Anglo Gold Ashanti, imebainika kumekuwapo na taarifa zisizo sahihi huku wawekezaji hao wakidai kuwa wanapata hasara, jambo alilosema si la kweli.

Alisema pamoja na kuwa ujenzi wa mgodi hauhitaji fedha nyingi na huchelewa kupata faida, lakini baadhi ya maeneo yamekuwa yakitolewa taarifa zisizo sahihi. Akitoa mfano katika mgodi wa Geita, alisema GAP imebaini kuwapo kwa taarifa za uongo juu ya matumizi ya uendeshaji wa mgodi, hali iliyosababisha mwekezaji huyo kukiri upungufu na kuahidi kulipa Sh bilioni 30 zilizokuwa zisilipwe serikalini kwa madai tu ya kugharamia shughuli za uendeshaji wa mgodi, jambo ambalo baada ya ukaguzi, iligundulika siyo kweli kwa vile haliingiliani na mkataba.

Aidha, katika ukaguzi huo imebainika kuwa wawekezaji hao wamekuwa wakijiamulia kujinunulia vitu ovyo kutoka nje ya nchi licha ya kuwa baadhi ya vitu hivyo vinapatikana nchini. Pia katika mgodi wa Bulyanhulu imebainika wazi kuwa yapo matumizi mengine ya uendeshaji wa mgodi yamekuwa yakisomeka isivyo na baada ya GAP kukagua vitabu vya mwekezaji huyo ambaye ni Barrick Gold Corporation, walikiri kuwapo kwa makosa na wameanza kuyarekebisha.

Kitengo hicho kinachosimamiwa na Wizara ya Nishati na Madini, kina kazi ya kuhakiki wingi na ubora wa dhahabu inayozalishwa na kusafirishwa nje na migodi mikubwa ili kujua thamani yake halisi na kiwango cha mrabaha kinachostahili kuingia serikalini. Kimeanzishwa baada ya Kampuni ya kigeni ya Alex Stewart (Assayers) iliyokuwa ikijihusisha na ukaguzi huo kwa niaba ya serikali. Ukaguzi huo utaendelea katika migodi mingine ikiwamo ya Tulawaka, North Mara na Golden Pride Mine
 
Wakaguzi wa dhahabu wagundua upungufu
Raymond Mihayo, Kahama
Daily News; Monday,November 17, 2008 @20:00


Alisema baada ya kitengo hicho kuanza ukaguzi katika mgodi wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Barrick Gold Corporation na Geita Gold Mine mali ya Anglo Gold Ashanti, imebainika kumekuwapo na taarifa zisizo sahihi huku wawekezaji hao wakidai kuwa wanapata hasara, jambo alilosema si la kweli.

Duh! Hawa Barrick pamoja na kuchukua 97% ya mapato ya dhahabu yetu ambayo bei yake katika soko la dunia imeongezeka kwa kiasi kikubwa bado wanapata hasara tu!!!! ama kweli wajinga ndiyo waliwao!!! :(
 
serikali ni sawa na mchuma janga. Ilidhani hilo janga itakula na hao wawekezaji, itakula na sisi wananchi. Ndio hayo sasa, kila siku wakiambiwa wanabisha na kutetea visivyotetewa.
 
Auditors uncover how gold mining companies swindle treasury

2008-11-20 10:31:28
By Anceth Nyahore PST, Kahama

One year old Gold Audit Program (GAP) has exposed stunning anomalies in record keeping by some big mining companies whose effect is to deny government huge tax and royalty revenues.

The Head of Finance and Administrative Department at the Gold Audit Program, Bruno Mteta said here last week that mine administration(s) are furnishing the government with incorrect information regarding their actual earnings as contrivance for cheating on levy obligations.

Mentioned are the Bulyanhulu Gold Mine which is owned by Barrick Gold Corporation and Geita Gold Mine under the management of Anglo Gold Ashanti whose books of accounts claim to have both sustained loses over time, but GAP auditors later discovered that financial records provided did not represent the true picture of operations, Mteta revealed.

He was addressing representatives from surrounding villages who had gathered at Kakola village in Kahama district to attend a special event organized by GAP as part of community sensitisation activities about the contribution of gold mining to national economy.

Mteta further told the gathering of villagers that although profit was not possible to be realised instantly in mining business, some of the companies utterly lied on the gains in order to cheat on royalty payments to the government.

He specifically zeroed in on cheat GAP discovered during recent past upon verification of initial report submitted by Geita Gold Mine administration which indicated huge spending by the scale of millions on construction work and administrative duties.

This report was deliberately twisted in order to justify non-remission of worthy revenue to the government.

Sequel to auditing, GAP came to discovered 30bn/- was overstated in that category of financial records.

Moreover, he claimed expenditures were not even part of the concluded mining contracts.


It is due to rampant cheating by some of the large scale miners in the country that GAP suggested to the Commissioner for Minerals to initiate a process for the review the existing mining policy and Act to ensure that even the common man benefits from the gold windfall.

A most important proposal includes scrapping some incentives enshrined in Mining Policy (1997) and Act, mostly notorious being the 15 percent additional allowance on unredeemed qualifying capital expenditure so that investors are made to pay 30 percent tax corporate.


This would be in addition to paying three percent royalty, withholding taxes, stamp duty, pay as you earn (PAYE), annual rent and application and preparation fees.

Last month, the parliament advised the government to stop issuing any new mining licenses and contracts until new legislations are passed that would ensure government raises its take from foreign mining companies to claw back more money for the county�s exchequer.

SOURCE: Guardian
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom