Wajuzi wa mambo naomba uzoefu kwa huyu Msichana

proxy

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
1,468
1,329
Habari za mida hii wana JF wote, natumaini mnaendelea vizuri na ujenzi wa nchi yetu lakini mkichukua tahadhari zote zinazohusiana na Covid 19.

Nije kwenye mada, leo nimepokea sms kutoka kwa msichana aliyenisumbua huko nyuma yaani takribani mwezi miwili imepita sasa. Nilijaribu kufanya jitihada zote ili niweze kumpata lakini akawa anazungusha zungusha sana huku akitoa sababu za hapa na pale najua mnanielewa.

Baada ya kumpotezea leo kanitumia sms kwamba nimuazime Elfu 30000 na amehaidi kunirudishia, binafsi moyo umeshtuka kidogo kama mnavyojua hii wakati huu wa nchi ya viwanda inahitaji umakini kidogo katika pesa. Mpaka sasa sijamjibu chochote nikaona ngoja nije kwa mabaharia ili tujadili kidogo hii mada.
 
Hapo amesha kukubalia ombi lako kwaiyo niwewe tu kujiongeza ule vitu vitam
 
Ana mimba sahivi huyo sasa hiyo thelathini itaamua uwe baba wa hiari au Bata tu Kama Bata nyengine.
 
Habari za mida hii wana JF wote, natumaini mnaendelea vizuri na ujenzi wa nchi yetu lakini mkichukua taadhari zote zinazohusiana na Covid 19.

Nije kwenye mada, leo nimepokea sms kutoka kwa msichana aliyenisumbua huko nyuma yaani takribani mwezi miwili imepita sasa. Nilijaribu kufanya jitihada zote ili niweze kumpata lakini akawa anazungusha zungusha sana huku akitoa sababu za hapa na pale najua mnanielewa.

Baada ya kumpotezea leo kanitumia sms kwamba nimwazime Elfu 30000 na amehaidi kuniludishia, binafsi moyo umesituka kidogo kama mnavyojua hii wakati huu wa nchi ya viwanda inahitaji umakini kidogo katika pesa. Mpaka sasa sijamjibu chochote nikaona ngoja nije kwa mabaharia ili tujadili kidogo hii mada.
Nipe namba yake ya simu
 
Kamwe wajinga hawatakaa waishe

Hili nalo la kuomba ushauri


Chunga utapigwa sana na ushamba wako
Mkuu unaelewa maana ya forum? Sio kila mtu anayeandika hapa kwa ajili ya kuomba ushauri ni mjinga na mshanga, hapa ni mahali pa watu kushirikishana mambo mbalimbali ya kushare experiences mbalimbali, sio kwamba huyu msichana nashindwa cha mjibu hapana ila nimeleta uzi huu ili kushirikishana na kupata uzoefu wa matatizo kama haya kwa maana naamini hata ni mahali penye watu wenye busara na uzoezi.
 
Kama unayo itoe ukijua ya kwamba unamsaidia...

Kama unayo pungufu yake na unaona unaweza msaidia, basi msaidie ukijua ya kwamba unamsaidia...

Kama hauna kabisa basi kiroho safi mjibu kuwa hauna...

Kumbuka ya kuwa huwa hatutoi kwa kuwa tunataka turudishiwe, bali huwa tunatoa kwa sababu tuna uwezo kwa kutoa/kusaidia...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom