Wajuvi wa mambo msaada tafadhari

holy holm

JF-Expert Member
May 6, 2017
4,670
8,670
Heshima kwenu wakuu
Nipeni tofauti ya maneno haya
KUPENDA na KUTAMANI maana nashindwa kuyatofautisha vizur
msaada please kwa anae fahamu.
 
Kwa mm ninavyoelewa ni kuwa kutamani ni kukitaka ki2 kwa muda ili kukata hamu za muhusika na baada ya hapo unakuwa haukiitaji tena ki2 hicho inaweza kuwa ni chakula,mwanamke,mwanaume, n.k ila kupenda ni hitajio linalotoka ndani ya moyo kutaka ki2 husika na hii huwa hainaga muda maalum ila unahitajia kuwa nacho mara zote na inaambatana na huruma pia
 
"kupenda" ni hisia chanya ya kuingiwa na kitu moyoni kwa sababu ya mvuto au uzuri wake. Lakini kutamani ni hisia ama chanya au hasi ya kuwa na shauku kubwa na kitu. Mfano ukiwa na shauku kubwa ya machungwa, basi unaweza kusema, "Natamani machungwa." Na hiyo ni hisia chanya. Lakini inakuwa hasi pale inapochanganyikana na hisia ya kutotaka wengine wapate. Mfano, umepewa chakula kiasi chako, lakini unataka upate zaidi (yaani bila kujali kuwa mwingine atakosa) - hiyo ni tamaa - lakini kama hisia hasi.
 
Kupenda huja baada ya kutamani. Kupenda ni hisia ya ndani inayoingia baada ya kutazama kitu na si kuona tu. Ukitazama kwa kuchamganua basi utajikuta sasa umependa.
 
Back
Top Bottom