Wajumbe mnahitaji kutumia busara sana katika uchaguzi wa UVCCM

KADA08

Member
Dec 2, 2017
44
152
Mmeletewa wagombea takribani 7 lakini kwa upeo wangu mnapaswa kuzingatia mambo kadhaa kabla ya kuamua:-
1. Mchagueni mgombea anayeijua jumuiya
2. Mchagueni mgombea mwenye uwezo wa kuwasemea ninyi na vijana wengine wa Tanzania
3. Mchagueni mgombea anayekidhi matakwa ya kisiasa kwa sasa kwa maana mwenye uwezo mkubwa wa kisiasa hususani public speaking au uwezo mzuri wa kuzungumza kwa hoja za ushawishi
4. Mchagueni mgombea anayependa haki na ukweli, pia awe jasiri wa kuimamia haki na ukweli kwa gharama yoyote
5. Mchagueni mgombea atakayeiunganisha jumuiya na kuifanya iwe tumaini kwa vijana na ikipe chama jeuri na matumaini kuelekea chaguzi au kukabili misukosuko ya kisiasa

Kwa mtazamo wangu namuona Kheri Denis James kuwa anatosha kwa sasa kutuvusha 2017-2022. Naomba mtupatie anakidhi sifa hizo nilizoainisha.
 
Kanda ya ziwa ndio imemtoa Rais wa JMT na mwenyekiti wa TAIFA wa CCM lakini wametoa wagombea wengi zaidi katika jumuiya mbili zenye nguvu ndani ya chama hicho yaani UWT na UVCCM ambao wote wanatajwa kuchuana vikali.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya CCM nafasi zote hizi kubwa kutokea ukanda mmoja kama ikitokea hivyo basi mtiririko utakuwa:-

1. Mwenyekiti CCM TAIFA kanda ya ziwa
2. Mwenyekiti UWT TAIFA kanda ya ziwa kwani wagombea karibu wote ni kutoka kanda ya ziwa.
3. Mwenyekiti UVCCM TAIFA kanda ya ziwa kwani nako wagombea 4 kati ya 7 wanatoka kanda ya ziwa.

Ifahamike kwa mujibu wa katiba ya CCM wajumbe wote hawa ni wajumbe wa kikao cha kamati kuu, moja ya vikao vya juu kabisa vya CCM katika kufanya maamuzi mbalimbali.

Ikitokea hivyo maana yake uongozi wenye sura ya kitaifa haupo!

Wajumbe wanapaswa kutumia busara sana ili kuliepusha hili lisitokee kwani yatakuwa ya CHADEMA na ukaskazini.

Fikra Mpya
Hata kwenye maofisi now wakurugenzi au wakuu wa Idara wengi ni from huko huko,
Ndio wakati wenu huu
 
Kwa hiyo kama hao wa makanda mengine hawatoshi sifa hao wa kanda ya ziwa wasiwe wenyeviti wee vipi kwenda kule!
 
Haya mambo ya kanda ccm hatuna na hatuangaliani kwa kanda
Ukanda upo chadema 96% ya watu wenye maamuzi wanatoka kaskazini
 
Kada, kwani ndo moja ya milestones za ccm awamu hii au malengo ya kiuchumi ya kanda ya ziwa?...anyways kila LA kheri na mnada maana mnanunua mifugo ya wengine (upinzani) na ya kwenu at the same time?!!!(ccm)
 
Haya mambo ya kanda ccm hatuna na hatuangaliani kwa kanda
Ukanda upo chadema 96% ya watu wenye maamuzi wanatoka kaskazini



Kuna uwezekano mkubwa ubongo wako umeathiriwa na harufu kali iliyokuwa inatoka kwenye "expansion joint"kipindi kile ulipokuwa unashangilia push-ups za majukwaani,pole sana.
 
Sijaona la maana kwenye post yako. Nyakati hizi si za kuwaza ukabila bali uwezo na ubunifu wa kiongozi haijalishi anatoka ukanda upi as long ni mtanzania. Tunataka mabadiliko chanya, Twende na Mathias Simon Kipala!
 
Kanda ya ziwa ndio imemtoa Rais wa JMT na mwenyekiti wa TAIFA wa CCM lakini wametoa wagombea wengi zaidi katika jumuiya mbili zenye nguvu ndani ya chama hicho yaani UWT na UVCCM ambao wote wanatajwa kuchuana vikali.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya CCM nafasi zote hizi kubwa kutokea ukanda mmoja kama ikitokea hivyo basi mtiririko utakuwa:-

1. Mwenyekiti CCM TAIFA kanda ya ziwa
2. Mwenyekiti UWT TAIFA kanda ya ziwa kwani wagombea karibu wote ni kutoka kanda ya ziwa.
3. Mwenyekiti UVCCM TAIFA kanda ya ziwa kwani nako wagombea 4 kati ya 7 wanatoka kanda ya ziwa.

Ifahamike kwa mujibu wa katiba ya CCM wajumbe wote hawa ni wajumbe wa kikao cha kamati kuu, moja ya vikao vya juu kabisa vya CCM katika kufanya maamuzi mbalimbali.

Ikitokea hivyo maana yake uongozi wenye sura ya kitaifa haupo!

Wajumbe wanapaswa kutumia busara sana ili kuliepusha hili lisitokee kwani yatakuwa ya CHADEMA na ukaskazini.

Fikra Mpya
Kwani huko uvccm mnachagua Kanda au mtu?
 
Kanda ya Magu iko ndani ya Kanda ya Ziwa

Inawezekana kabisa ukawa sahihi kwamba kanda ya Magu iko ndani ya kanda ya ziwa.

Na kama hilo ni sahihi, kuiita kanda ya Magu kanda ya ziwa, si sahihi.

Nitakupa mfano.

Dar es salaam ipo ndani ya Tanzania, lakini Dar es salaam si Tanzania. Kwa sababu Tanzania ni kubwa kuliko Dar es salaam.

Population ya Dar si ya Tanzania. Uchumi wa Dar si wa Tanzania. Ni sehemu ya population ya Tanzania, ni sehemu ya uchumi wa Tanzania.

Kuna watu wa kanda ya ziwa tuna heshima zetu hatutaki kuhusishwa na Magufuli. Tunamuona anachemka.

Kwa hiyo, ukianza kuhusisha ujinga wa Magufuli na kanda ya ziwa, unatuvunjia heshima na kutupaka matope wakati hatuhusiani lolote na ujinga huo.

Ndiyo maana nakwambia hizo habari kama ni za kanda ya Magufuli, sema za kanda ya Magufuli.

Kanda ya ziwa ni pana kuliko "Team Magufuli".

Obise tole na masala , totatogwile ontemi sagala.
 
Kanda ya ziwa ndio imemtoa Rais wa JMT na mwenyekiti wa TAIFA wa CCM lakini wametoa wagombea wengi zaidi katika jumuiya mbili zenye nguvu ndani ya chama hicho yaani UWT na UVCCM ambao wote wanatajwa kuchuana vikali
Hee! yaani we unataka watu wanyimwe fulsa ya kugombea kisa wanatoka eneo alilotoka Mheshimiwa
 
Kanda ya ziwa ndio imemtoa Rais wa JMT na mwenyekiti wa TAIFA wa CCM lakini wametoa wagombea wengi zaidi katika jumuiya mbili zenye nguvu ndani ya chama hicho yaani UWT na UVCCM ambao wote wanatajwa kuchuana vikali.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya CCM nafasi zote hizi kubwa kutokea ukanda mmoja kama ikitokea hivyo basi mtiririko utakuwa:-

1. Mwenyekiti CCM TAIFA kanda ya ziwa
2. Mwenyekiti UWT TAIFA kanda ya ziwa kwani wagombea karibu wote ni kutoka kanda ya ziwa.
3. Mwenyekiti UVCCM TAIFA kanda ya ziwa kwani nako wagombea 4 kati ya 7 wanatoka kanda ya ziwa.

Ifahamike kwa mujibu wa katiba ya CCM wajumbe wote hawa ni wajumbe wa kikao cha kamati kuu, moja ya vikao vya juu kabisa vya CCM katika kufanya maamuzi mbalimbali.

Ikitokea hivyo maana yake uongozi wenye sura ya kitaifa haupo!

Wajumbe wanapaswa kutumia busara sana ili kuliepusha hili lisitokee kwani yatakuwa ya CHADEMA na ukaskazini.

Fikra Mpya


Tulieni mnyolewe, maana tulipo waambia tupige UKUTA mkakataaa, sasa mnalialia nini?
 
Kwa mara ya kwanza katika historia ya CCM nafasi zote hizi kubwa kutokea ukanda mmoja kama ikitokea hivyo basi mtiririko utakuwa:-

1. Mwenyekiti CCM TAIFA kanda ya ziwa
2. Mwenyekiti UWT TAIFA kanda ya ziwa kwani wagombea karibu wote ni kutoka kanda ya ziwa.
3. Mwenyekiti UVCCM TAIFA kanda ya ziwa kwani nako wagombea 4 kati ya 7 wanatoka kanda ya ziwa.
Una jicho la kibaguzi

End of the story.
 
Sijaona la maana kwenye post yako. Nyakati hizi si za kuwaza ukabila bali uwezo na ubunifu wa kiongozi haijalishi anatoka ukanda upi as long ni mtanzania. Tunataka mabadiliko chanya, Twende na Mathias Simon Kipala!
Mlevi sana huyo na mzinzi
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom