Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Wanawake wanaofuata mali China
ijumaa wikienda
Uwepo wa wajasiriangono hao ndiyo zao la maduka mengi madogo madogo ya kuuza bidhaa kutoka China ndani ya Jiji la Dar na mikoa mingine, hususan nguo, viatu na vipodozi.
Gazeti the Biggest IQ Ijumaa Wikienda ndilo pekee linaloweza kuthubutu na kuanika uchafu wote unaofanywa na baadhi ya wanawake wanaounga msafara wa wajasiriamali kwenda China ambapo wakiwa huko hugeuka wawekezaji wa ngono.
Mwandishi wetu aliyerejea juzi-kati nchini akitokea kwenye Jiji la Guangzhou, China ana ripoti kamili ya wanawake hao wanaoichafua sifa njema ya Tanzania kwenye himaya ya Rais Hu Jintao.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa paparazi wetu, wanawake wengi wanaokwenda China hupendelea kufikia kwenye Jiji la Guangzhou ambako huweka makazi yao kwenye hoteli za Dongfen, Shushanlo na Baowani.
Uchunguzi huo umebaini kuwa wanawake wengi wakifika katika hoteli hizo, hupanga chumba kwa kushirikiana kisha kuanza kujiuza kwa wanaume ambapo kwa kupitia biashara hiyo, huweza kujiingizia kipato cha kuwawezesha kununua bidhaa za kujaza kwenye maduka yao.
Imebainika kuwa wakifika hotelini, hulipia chumba kwa fedha za China, Yuan RMBI 200 ambazo ni sawa na Shilingi 40,000 za Kitanzania na hutoa huduma ya chapchap a.k.a short-time kwa Yuan RMBI 100 (shilingi 20,000) kwa kichwa.
Kutokana na hali hiyo, wajasiriangono hao hujitahidi kwa kadiri wawezavyo kuwahudumia wateja wengi ili kujiingizia kipato kikubwa, hivyo kuifanya safari yao kuwa na mafanikio.
Kila wanavyojiuza, malipo yao huyatumia kununulia bidhaa kama nguo, viatu, vipodozi, dawa za nywele, ngozi na vitu vingine. Hununua taratibu na wakipata mzigo wa kutosha ndiyo hurejea Bongo, inasema ripoti hiyo ya mwandishi wetu.
Uchunguzi zaidi wa mwandishi wetu umebaini kuwa wanawake hao wa Kitanzania kwenye kazi yao ya kujiuza, wateja wao wakubwa ni Waafrika wanaoishi nchini humo kutoka Nigeria, Mali, Senegal na baadhi ya Watanzania.
Akiwa jijini Guangzhou, paparazi wetu alizungumza na mhudumu mmoja wa Hoteli ya Shushanlo ambaye alisema kuwa pamoja na kwamba hivi sasa mambo yanaonekana kwenda sawia kwa Watanzania, lakini huko nyuma biashara ya ngono ilikuwa inawalipa zaidi.Kwa huduma ya dakika 30, mwanamke wa Kitanzania alilipwa Yuan RMBI 200 (shilingi 40,000 au dola 30) lakini baada ya soko kuvamiwa na wanawake kutoka Rwanda na Uganda, thamani ilishuka ndiyo maana sasa hivi wanachukuliwa kwa Yuan RMBI 100, alisema mhudumu huyo (jina tunalihifadhi).
Ripoti ya mwandishi wetu inaongeza: Japo si wote wanaojiuza na kuendesha maduka yao kwa jeuri ya miili yao lakini hali ni mbaya, kwa wanaume wenye wake zao ambao wanakwenda China kufuata bidhaa za biashara ni vema kuangalia nyendo zao. Hali ni mbaya.
Kumbe maduka mengi yanayochomoza kama uyoga Dar na kwingine, hayatokani na nguvu ya ujasiriamali tunayoijua bali ni faida ya miili yao. Wanawake hao wanaichafua Tanzania.
Gazeti hili linalaani vikali vitendo vya wanawake hao na linawataka kutambua utu wao kuliko kitu kingine chochote. Maradhi ni mengi lakini pia fedha si kila kitu katika maisha. Mhariri
ijumaa wikienda
Gazeti the Biggest IQ Ijumaa Wikienda ndilo pekee linaloweza kuthubutu na kuanika uchafu wote unaofanywa na baadhi ya wanawake wanaounga msafara wa wajasiriamali kwenda China ambapo wakiwa huko hugeuka wawekezaji wa ngono.
Mwandishi wetu aliyerejea juzi-kati nchini akitokea kwenye Jiji la Guangzhou, China ana ripoti kamili ya wanawake hao wanaoichafua sifa njema ya Tanzania kwenye himaya ya Rais Hu Jintao.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa paparazi wetu, wanawake wengi wanaokwenda China hupendelea kufikia kwenye Jiji la Guangzhou ambako huweka makazi yao kwenye hoteli za Dongfen, Shushanlo na Baowani.
Uchunguzi huo umebaini kuwa wanawake wengi wakifika katika hoteli hizo, hupanga chumba kwa kushirikiana kisha kuanza kujiuza kwa wanaume ambapo kwa kupitia biashara hiyo, huweza kujiingizia kipato cha kuwawezesha kununua bidhaa za kujaza kwenye maduka yao.
Imebainika kuwa wakifika hotelini, hulipia chumba kwa fedha za China, Yuan RMBI 200 ambazo ni sawa na Shilingi 40,000 za Kitanzania na hutoa huduma ya chapchap a.k.a short-time kwa Yuan RMBI 100 (shilingi 20,000) kwa kichwa.
Kutokana na hali hiyo, wajasiriangono hao hujitahidi kwa kadiri wawezavyo kuwahudumia wateja wengi ili kujiingizia kipato kikubwa, hivyo kuifanya safari yao kuwa na mafanikio.
Kila wanavyojiuza, malipo yao huyatumia kununulia bidhaa kama nguo, viatu, vipodozi, dawa za nywele, ngozi na vitu vingine. Hununua taratibu na wakipata mzigo wa kutosha ndiyo hurejea Bongo, inasema ripoti hiyo ya mwandishi wetu.
Uchunguzi zaidi wa mwandishi wetu umebaini kuwa wanawake hao wa Kitanzania kwenye kazi yao ya kujiuza, wateja wao wakubwa ni Waafrika wanaoishi nchini humo kutoka Nigeria, Mali, Senegal na baadhi ya Watanzania.
Akiwa jijini Guangzhou, paparazi wetu alizungumza na mhudumu mmoja wa Hoteli ya Shushanlo ambaye alisema kuwa pamoja na kwamba hivi sasa mambo yanaonekana kwenda sawia kwa Watanzania, lakini huko nyuma biashara ya ngono ilikuwa inawalipa zaidi.Kwa huduma ya dakika 30, mwanamke wa Kitanzania alilipwa Yuan RMBI 200 (shilingi 40,000 au dola 30) lakini baada ya soko kuvamiwa na wanawake kutoka Rwanda na Uganda, thamani ilishuka ndiyo maana sasa hivi wanachukuliwa kwa Yuan RMBI 100, alisema mhudumu huyo (jina tunalihifadhi).
Ripoti ya mwandishi wetu inaongeza: Japo si wote wanaojiuza na kuendesha maduka yao kwa jeuri ya miili yao lakini hali ni mbaya, kwa wanaume wenye wake zao ambao wanakwenda China kufuata bidhaa za biashara ni vema kuangalia nyendo zao. Hali ni mbaya.
Kumbe maduka mengi yanayochomoza kama uyoga Dar na kwingine, hayatokani na nguvu ya ujasiriamali tunayoijua bali ni faida ya miili yao. Wanawake hao wanaichafua Tanzania.
Gazeti hili linalaani vikali vitendo vya wanawake hao na linawataka kutambua utu wao kuliko kitu kingine chochote. Maradhi ni mengi lakini pia fedha si kila kitu katika maisha. Mhariri