Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,427
- 154,272
Yaani sijui ni ugumu wa maisha au sijui ni kukua kwa utandawazi.Walaji wa sungura hapa nchini wameongezeka na wanazidi kuongezeka kwa kasi kweli kweli, kuliko hata walaji wa kuku, mbuzi, Kitimoto, ng'ombe nk.
Sungura mmoja aliyechomwa au kubanikwa huuzwa kati ya TZS 36 - 65,000.
Kampuni ya NAMAINGO ndiyo kampuni inayojishughulisha na uuzwaji na usambazaji wa sungura nje na ndani ya nchi. Wanafanya kazi na benki ya NMB na TFDA - Tanzania Food & Drugs Authority katika kuwahakikishia walaji ubora wa chakula /nyama ya sungura.
Wahi fursa hiyo.
Watanzania wenzangu msidanganyike na kuingia kwenye biashara hii. This is a typical white elephant business.
Ni nani ambaye yuko tayari kununua sungura mmoja kati ya TZS.36,000/- hadi 65,000/-????
Mnunuzi yuko Tanzania hii hii ya Magufuli ambayo hadi mabiashara makubwa yanaanguka kwa kukosa wateja?
Namaingo acheni utapeli. Namaingo acheni ubabaishaji. jsenyinah tafuta shughuli halali ambayo MUNGU atakubariki nayo, wacha kuwaingiza wenzako choo cha watoto ambacho kimejaa ma poti na pampas zilizotumika, wakapata aibu ya kujisaidia maungoni.