Waitara: Sugu aliandika barua ya kujiuzulu Ubunge ndani ya CHADEMA!

idawa

JF-Expert Member
Jan 20, 2012
25,284
38,312
Waitara ameongea mengi,ila hili limenifikirisha zaidi.

Ameyasema hayo jana wakati wa kufunga kampeni za udiwani kata mojawapo huko Mbeya.

Amesema mwaka 2010 mara baada ya Chadema kuchukua jimbo, ulifika wakati wa kuteua mbunge viti maalum... wakati Sugu akitegemea jina litatoka ndani ya mkoa wa Mbeya hasa kwa kina mama wa kawaida.

Alishangaa kuletewa jina kwenye bahasha toka Dar la Mwana mama Naomi Kaihula makazi wa Kawe Jiji Dar kuwa mbunge viti maalum wa Jiji la Mbeya.

Kitendo hicho kilimkwaza sana Sugu hali iliyopelekea kwenda Makao Makuu Chadema kuhoji swala hilo, kuwa kwa nini jina halijatoka Mbeya kwa akina mama aliohangaika nao usiku na mchana kusaka kura.

Kabla hajajibiwa Sugu aliandika barua ya kujiuzulu Ubunge.. baadaye vikakaliwa vikao kumshawishi Sugu asijiuzulu na kumwahidi kuwa ushauri wake utazingatiwa 2015..

Watahakikisha mbunge viti maalum anatoka mkoa wa Mbeya, Mbowe pia akamsihi atulie jina lake litaingia kwenye Kamati Kuu ya Chama.

2015 Chadema wakashinda tena ubunge Mbeya, jina la viti maalum likatoka tena Dara (Sofia Mwakaganda) na sio kwa akina mama wa jiji la Mbeya kama walivyomwahidi 2010...kwa kuwa Sugu walimhonga kwa kumpa ujumbe Kamati Kuu safari hii hakuweza kuhoji chochote kuhusu jina kutoka Dar....

==========================
Binafsi nampongeza sugu kwa ujasiri aliouonyesha kwa kuwatetea wananchi wake hadi kufikia hatua ya kutaka kujiuzulu ubunge.

Pia ni vyema Chadema ijitafakari, mambo kama haya ndio yanafanya viongozi wengi kuhamia Chama tawala.....

Hili swala la viti maalum limeumiza majimbo mengi sana, akina mama wanapambana na polisi wanapigwa virungu wanamwagiwa maji ya washawasha halafu mwisho wa siku mnaambiwa jina limetoka Dar.

 
Kama wanaojiuzulu ubunge wanaandika barua kwenye chama mbona yeye hakuandika baada ya kuhongwa hela ndogo ambayo angeniomba ningempa bila shaka ?

Waitara mtu aliyeokotwa na chadema baada ya kugoma kumpikia chai Emmnuel Nchimbi pale UVCCM leo kasahau yote masikini !
 
Siasa za Africa zinahitaji Unafiki wa kiwango cha Juu sana ili uweze kuendana na Matakwa ya Wakubwa..,
 
==========================
Binafsi nampongeza sugu kwa ujasiri aliouonyesha kwa kuwatetea wananchi wake hadi kufikia hatua ya kutaka kujiuzulu ubunge.

Pia ni vyema Chadema ijitafakari, mambo kama haya ndio yanafanya viongozi wengi kuhamia Chama tawala.....

Hili swala la viti maalum limeumiza majimbo mengi sana, akina mama wanapambana na polisi wanapigwa virungu wanamwagiwa maji ya washawasha halafu mwisho wa siku mnaambiwa jina limetoka Dar.

kwenye hiki kipande chako ulipohitimisha kwa mawazo yako binafsi nimepata shida sana kukuelewa wewe umethibitisha vipi madai ya waitara kama ya kweli? Unataka kutuambia kwamba mama wa taifa kwa maneno yasemwayo mtaani ukuu wa wilaya aliopewa na jiwe ni chakula yake? Mi nafikir conclution hutolewa baada ya kupata habar kamili vinginevyo umekurupuka.
 
Nijuavyo mimi, kuna utaratibu maalum hufuatwa na chama katika kuteua viti maalum, na orodha huwa wazi kabla haija pelekwa tume. Utaratibu huo hufuatwa na tume kutokana na wabunge wa majimbo wanavyo patikana. Jinsi chama kinavyo kuwa na wabunge wengi kuna uwiano wa viti maalum.
Hata akifa mbunge wa viti maalum Chama hakichagui tena mbunge bali NEC inachagua kutoka listi waliyo nayo.
 
~~~>>> Swala la viti maalumu halina Usawa iwe kwa CCM ama kwa Chadema........ Wote wanachaguana kwa KUJUANA....
Ni bora iwe anatoka jimbo husika lakini sio mnaletewa kuwa ni huyu, bila kushirikishwa kwa lolote inaumiza sana...

Siasa zetu ni za jasho na damu hivyo ni vyema kutambua mchango wa wadau..,. Sugu alitambua shida alizopata na akina mama wa Mbeya ndio maana ilimumiiza sana
 
Back
Top Bottom