Waitara: CHADEMA inapokea ruzuku ya sh 329 milioni kila mwezi, Dr Mashinji analipwa mshahara sh 7mil kwa mwezi!

Ni dhahiri kwa sasa tunahitaji madaktari bingwa wengi wa magonjwa ya akili.Maana ukisikiliza hoja zinazoongelewa na mtu mzima ni afadhari za mtoto zinakuwa na logic.
 
Alichokosea waitara ni kuhama chama kwa kigezo cha kugombana na mbowe, kulipwa katibu mkuu ni sawa tu, mbona wa ccm analipwa 12 milion?
 
Wabunge na Madiwani wakihama wengi kutoka cdm ruzuku itapungua na mshahara wa 7m utapunguzwa hadi 3.5m vinginevyo uwezo wa chama kujiendesha utakuwa matatani.
 
Anaongea sana awe anaweka akiba. Hao anaodai alikosana nao bado wako ccm. Na akikosana na wengine ataelekea wapi? Badala ya kuongelea issues yeye amejikita kwenye personalities. Huyu elimu haijamsaidia anaonekana ni mjinga zaidi ya wale wenye elimu ya darasa la saba
 
Ha ha ha yaani Hospitali ya Chanika iliyowekewa misingi na mkataba na Jerry Silaa, wakati wa ufunguzi Bashite akajiona ameijenga yeye hlf ghafla paaah eti Waitara naye ameijenga. Kweli wanasiasa wamekosa aibu mno.
 
Jamaa anaropoka sana hadi ccm wanaweza kumpiga chini..

"Nilihama ccm sababu nilikorofishana na Makamba na Nchimbi" ameshau Makamba na Nchimbi bado wapo ndani ya ccm.

"Nimehamia ccm baada ya kuona sina cha kupoteza maana nitarudi tena bungeni"

Hizi kauli zinaweza kumgharimu ndani ya ccm.!
Ina maana ccm wamesha muahakikishia kurudi bungeni wala hata sio wananchi wapiga kura.
 
hata kwenye nyumba za ibada watumishi wake wanakula sadaka. sasa waitara anataka viongozi wa vyama waishi bila mishahara? amehamia ccm huko atakuwa mzalendo bila mshahara. napendekeza hata kwenye ubunge asipokee hata posho
 
Aliyekuwa mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara yupo mubashara Clouds 360 anaelezea jinsi ruzuku ya chama inavyofisadiwa.

Mwita anadai mbunge wa Tarime John Heche alipokuwa mwenyekiti wa Bavicha alikuwa analipwa mshahara sh 1.5 mil kila mwezi kinyume cha utaratibu.

Anadai wabunge wa viti maalumu ndio mtaji wa Mbowe pale CHADEMA.

Anadai yeye ndio mbunge bora wa jiji la Dsm, amejenga madaraja na hospitali pale Chanika na kwamba wakati wa mafuriko wapiga kura wake huja nyumbani kwake kupata hifadhi.

Kadhalika anadai ameondoka Chadema baada ya Mbowe na Dr Mahanga kumhakikishia kuwa hataitishwa kugombea tena 2020.

Mwita anadai mwaka 2008 alihama CCM na kwenda Chadema baada ya kugombana na aliyekuwa Katibu mkuu mzee Makamba na yule mwenyekiti wa UVCCM Dr Nchimbi.

Amesisitiza kuwa amejiuzulu ubunge muda huu baada ya kuona kuna fursa ya yeye kurudi tena bungeni katika uchaguzi mdogo kwa tiketi ya CCM hivyo hakuna atakachopoteza. Pia amedai yeye hakuutaka uenyekiti bali alitamani sana Mwenyekiti wa chama taifa awe Tundu Antipas Lissu.

Amemaliza kwa kusema ameshachukua fomu ya kugombea tena ubunge wa Ukonga na kwamba katika mazingira ya kisiasa akitokewa na baya lolote atamhisi Mbowe!

Source: Clouds tv!
Ni mkurya was Kwanza asiyekuwa na msimamo. Mkurya was Kwanza mwenye tamaa ya fedha ambaye anajijali yeye KULIKO wengine. Anasema KUWA wanagongolamboto wanaenda kuomba au kukaa kwake kujiifadhi. Kama siyo kuwadhalilisha wanagongolamboto Ni nn anaouwezo gani was kuifadhi hata zaidi ya watu 20. Amekimbilia ccm baada ya kuona hatagombea ubunge na yy alivyo bila ubunge haweziishi. Sijawahi kuona mkurya mwenye njaa Kama huyu. Tangu amehama Ni chadema tu Hana jipya. Tutaona mwisho wake
 
Huyu mbona anaonekana kama amegeuka na kuwa punguani? Hayo ni maneno ya kutamkwa na mtu mwenye akili timamu?
 
Back
Top Bottom