eden kimario
JF-Expert Member
- Jun 13, 2015
- 10,227
- 16,178
Nakumbuka vizuri ccm katika hali ya kutafuta kuendelea kuwa madarakani, waliwatumia baadhi ya waislam, wakapanga kwenye ilani yao enzi za kikwete akiwa mgombea kwamba, atawapatia mahakama ya kadhi endapo atashinda katika uchaguzi ulioonekana upinzani kuja kwa kasi nchini
Waislam waliotumiwa wakapambana kuhakikisha kikwete anashinda, na kweli akashinda
Nakumbuka wengi wa hawa waislam walisema tumpe mwislam mwenzetu kura kwa kuwa tu aliwaahidi mahakama ya kadhi, na pia kupinga kwa nguvu mgombea wa upinzani asipewe kura na waislam, kwa kuwa alikuwa mtumishi wa kanisa, na kwamba akiingia ikulu hawataipata mahakama ya kadhi ambayo waliahidiwa na Ccm kupitia ilani yao.
Baada ya kumpigania mtu wao na akashinda japo alipigiwa kura na pande zote za Dini, wakawa wanasubiri kwa hamu utekelezwaji wa ilani ya Ccm kuhusu mahakama ya kadhi waliyoahidiwa,
Serikali haikuwakatalia kuunda mahakama ya kadhi, Bali iliwataka waislamu waiunde wenyewe na sio kuihusisha na serikali, kwa kuwa serikali haina Dini!
Waislamu wale wakaja juu wakisema kama serikali haina Dini kwa nini mliliweka kwenye ilani ya Ccm
Mpaka Leo ndugu zangu waislam wana kinyongo lakini wameshasahau na maisha yanaendelea
My take
Ccm kila unapokaribia uchaguzi huja na kitu ambacho kitawabakiza madarakani
Hutumia hata Ukabila, Udini, kuhakikisha wanaendelea kuwa madarakani
Kwa sasa mbinu zimebadilika wanaitumia tume ya uchaguzi, police na hata wanajeshi hivi sasa ili kusalia madarakani
Tusiongopewe kwa kugawiwa, tishert, kofia na pesa mnasahau machungu mliyonayo,
Kwa sasa nchi inapitia hali ngumu ya kiuchumi kwa wananchi wake, yote haya inaonyesha serikali ya Ccm kutothamini wananchi wa Tanzania
Nawatakia heri ya mwaka mpya wa 2019 na kwa herini mwaka 2018
Eden kimario
Sent using Jamii Forums mobile app
Waislam waliotumiwa wakapambana kuhakikisha kikwete anashinda, na kweli akashinda
Nakumbuka wengi wa hawa waislam walisema tumpe mwislam mwenzetu kura kwa kuwa tu aliwaahidi mahakama ya kadhi, na pia kupinga kwa nguvu mgombea wa upinzani asipewe kura na waislam, kwa kuwa alikuwa mtumishi wa kanisa, na kwamba akiingia ikulu hawataipata mahakama ya kadhi ambayo waliahidiwa na Ccm kupitia ilani yao.
Baada ya kumpigania mtu wao na akashinda japo alipigiwa kura na pande zote za Dini, wakawa wanasubiri kwa hamu utekelezwaji wa ilani ya Ccm kuhusu mahakama ya kadhi waliyoahidiwa,
Serikali haikuwakatalia kuunda mahakama ya kadhi, Bali iliwataka waislamu waiunde wenyewe na sio kuihusisha na serikali, kwa kuwa serikali haina Dini!
Waislamu wale wakaja juu wakisema kama serikali haina Dini kwa nini mliliweka kwenye ilani ya Ccm
Mpaka Leo ndugu zangu waislam wana kinyongo lakini wameshasahau na maisha yanaendelea
My take
Ccm kila unapokaribia uchaguzi huja na kitu ambacho kitawabakiza madarakani
Hutumia hata Ukabila, Udini, kuhakikisha wanaendelea kuwa madarakani
Kwa sasa mbinu zimebadilika wanaitumia tume ya uchaguzi, police na hata wanajeshi hivi sasa ili kusalia madarakani
Tusiongopewe kwa kugawiwa, tishert, kofia na pesa mnasahau machungu mliyonayo,
Kwa sasa nchi inapitia hali ngumu ya kiuchumi kwa wananchi wake, yote haya inaonyesha serikali ya Ccm kutothamini wananchi wa Tanzania
Nawatakia heri ya mwaka mpya wa 2019 na kwa herini mwaka 2018
Eden kimario
Sent using Jamii Forums mobile app