Elections 2010 Waislamu kuzindua mwongozo wa uchaguzi Alhamisi

JoJiPoJi

JF-Expert Member
Aug 8, 2009
2,907
3,260
Hidaya Kivatwa na Salim Said
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14158

SHURA ya Maimamu wa Tanzania, kesho inatarajia kuzindua rasmi mwongozo kwa Waislamu kuhusu uchaguzi mkuu wa 2010 na moto wa siasa za ukombozi.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 8:00 mchana.

Akizungumza na waandishi wa habari Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa kamati kuu ya siasa ya taasisi hiyo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema uzinduzi huo utahudhuriwa na zaidi ya masheikh 100 kutoka katika mikoa 22 ya Tanzania Bara.

Alisema mwongozo huo utagusia masuala mbalimbali ya kitaifa yakiwemo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

“Mwongozo unahusisha masuala ya elimu, afya, uchumi, demokrasia, siasa na kilimo. Mambo mengi zaidi tutayaeleza katika uzinduzi ,” alisema Sheikh Ponda.

Alisema kila mkoa utatoa masheikh watano ambao watawawakilisha Waislamu wa mikoa yao na baadaye kuwarejeshea salamu za pamoja za Waislaam kwa serikali ya CCM.

Alisema mWongozo huo utakuwa na salamu na ujumbe maalum kwa serikali kufuatia kitendo chake cha kukaa kimya wakati Kanisa Katoliki, lilipotoa waraka ambao kimsingi unahatarisha amani, usalama na umoja wa kitaifa.

“Ndani ya mwongozo wetu kuna ujumbe maalum kwa serikali ya CCM kwa kule kakaa kimya kwake kimya baada ya Kanisa Katoliki kutoa waraka ambao kimsingi jamii na serikali zinajua kabisa kwamba unahatarisha umoja wa kitaifa,” alisema Sheikh
Ponda.
Alisema huko nyuma, viongozi wa madhehebu ya Kiislamu walijaribu kutoa elimu ya uraia, lakini serikali iliwakamata na kuwawe ndani kwa madai ya uchochezi.

"Je waraka na ilani ya Wakatoliki hazileti uchochezi,” alihoji Ponda.
Alisema mwongozo huo utaweka mwelekeo na msimamo wa pamoja wa Waislamu kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu na uchaguzi mkuu wa urais, ubunge na udiwani utakaofanyika mwakani.
 
Waislam, kaazi kweli kweli, hivi uislam ni dini kweli au cult ya kiaina?
 
Hey....
its good ideal..tunatarajia mwongozo utakuwa bomba na mwiba kwa CCM,kwani wao ndo wamekuwa wapingaji wakuu wa elimu ya uraia,we are waiting for that...2po pamoja.
 
sasa huo mwongozo una tofauti gani na ule wa katoliki?mi siamini kabisa hawa waislamu viongozi wao kama wana akili,hope ni mambo ya kitoto na utoto unawasumbua.yani unapinga mwongozo wa mwenzio then unatoa wakwako wa aina hiyo hiyo,hii ni akili au matope?kwani wao hawavunji amani?why wa wakatoliki ndo uvunje amani?they are nuts i believe.na hakuna mtu ataeupinga kama ndo matarajio yao,waweke ufitini,uwongo,udini hawatasikia hata neno from katoliki wala govt
 
"Ndani ya mwongozo wetu kuna ujumbe maalum kwa serikali ya CCM kwa kule kakaa kimya kwake kimya baada ya Kanisa Katoliki kutoa waraka ambao kimsingi jamii na serikali zinajua kabisa kwamba unahatarisha umoja wa kitaifa," alisema Sheikh
Ponda.

Kazi kweli kweli. Lini tutajifunza kuwa wabunifu? kwanini kazi yetu iwe kufungwa kamba kuvutwa kama kondoo?
Inaonekana tunatoa waraka kwa kuwa Wakatoliki wametoa.

Je, tumepima kwa mapana na kutafakari maudhui ya waraka wa wakatoliki?

Je, waraka wetu ni kuwajibu wakatoliki au ni kutoa mwongozo kwa Watanzania tunapoelekea uchaguzi mkuu ujao, ili kuhakikisha kuwa tunapata serikali itakayokuwa inawajibika kwa wananchi wake na sio kwa mafisadi na wateule wachache?

Inasikitisha kuwa kumbe waraka unaelekezwa kwa wakatoliki na sio kulenga kumkomboa mTanzania!!!!!!!!!

Kazi kweli kweli!
 
"Ndani ya mwongozo wetu kuna ujumbe maalum kwa serikali ya CCM kwa kule kakaa kimya kwake kimya baada ya Kanisa Katoliki kutoa waraka ambao kimsingi jamii na serikali zinajua kabisa kwamba unahatarisha umoja wa kitaifa," alisema Sheikh
Ponda.



Kweli wanadamu tumetofautiana.
 
Hidaya Kivatwa na Salim Said
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14158

SHURA ya Maimamu wa Tanzania, kesho inatarajia kuzindua rasmi mwongozo kwa Waislamu kuhusu uchaguzi mkuu wa 2010 na moto wa siasa za ukombozi.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 8:00 mchana.

Akizungumza na waandishi wa habari Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa kamati kuu ya siasa ya taasisi hiyo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema uzinduzi huo utahudhuriwa na zaidi ya masheikh 100 kutoka katika mikoa 22 ya Tanzania Bara.

Alisema mwongozo huo utagusia masuala mbalimbali ya kitaifa yakiwemo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

“Mwongozo unahusisha masuala ya elimu, afya, uchumi, demokrasia, siasa na kilimo. Mambo mengi zaidi tutayaeleza katika uzinduzi ,” alisema Sheikh Ponda.

Alisema kila mkoa utatoa masheikh watano ambao watawawakilisha Waislamu wa mikoa yao na baadaye kuwarejeshea salamu za pamoja za Waislaam kwa serikali ya CCM.

Alisema mWongozo huo utakuwa na salamu na ujumbe maalum kwa serikali kufuatia kitendo chake cha kukaa kimya wakati Kanisa Katoliki, lilipotoa waraka ambao kimsingi unahatarisha amani, usalama na umoja wa kitaifa.

“Ndani ya mwongozo wetu kuna ujumbe maalum kwa serikali ya CCM kwa kule kakaa kimya kwake kimya baada ya Kanisa Katoliki kutoa waraka ambao kimsingi jamii na serikali zinajua kabisa kwamba unahatarisha umoja wa kitaifa,” alisema Sheikh
Ponda.
Alisema huko nyuma, viongozi wa madhehebu ya Kiislamu walijaribu kutoa elimu ya uraia, lakini serikali iliwakamata na kuwawe ndani kwa madai ya uchochezi.

"Je waraka na ilani ya Wakatoliki hazileti uchochezi,” alihoji Ponda.
Alisema mwongozo huo utaweka mwelekeo na msimamo wa pamoja wa Waislamu kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu na uchaguzi mkuu wa urais, ubunge na udiwani utakaofanyika mwakani.

And this is different from waraka wa kanisa katoliki how?..........Ngoja tuone wale walio kuwa wanau lalamikia waraka ule kama wata lalamikia waraka huu nao kwa nguvu, kasi na ari ile ile.
 
Bado kunakuja WARAKA wa WASABATO, Waraka wa Anglican, Waraka wa Walutheri n.k.

Nafikiri nchi inaelekea pabaya zaidi kama kila mtu atatoa waraka wake. Hoja yangu ni ile ile kwanini kila dini isianzishe chama chake cha siasa, kama wao mabingwa wa kutoa waraka?
 
Kibabu Kingunge mwanasiasa mkongwe, asiye na dini kutokana na kujikita zaidi katika ukomunisti, ameanzisha vagi ambalo halina maana kiasi kwamba hata wale waliokuwa wamelala nao sasa wanataka wasikike kuwa walikuwa na jambo la muhimu kwa jamii.
 
Back
Top Bottom