kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,888
Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka MSF limesema kwa akali Waislamu 6,700 wa jamii ya Rohingya waliuliwa katika kipindi cha mwezi mmoja nchini Myanmar, tangu operesheni mpya iliyoungwa mkono na serikali ianzishwe na jeshi la nchi hiyo dhidi ya jamii hiyo ya wachache.
Shirika hilo limeyasema hayo leo Alkhamisi na kuongeza kuwa, miongoni mwa Waislamu hao wa Rohingya waliouawa ni watoto wadogo 730 wenye umri chini ya miaka mitano.
Mkurugenzi wa Matibabu wa shirika hilo, Sidney Wong amesema takwimu hizo zimetokana na uchunguzi wa kina wa taasisi hiyo kwa familia zipatazo 2,434.
Amesema karibu asilimia 70 ya vifo hivyo vimetokana na majeraha ya risasi za jeshi la nchi hiyo, katika operesheni yake maalumu mkoani Rakhine, kuanzia mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka, asilimia 9 ya Waislamu hao wa Rohingya waliuawa kwa kuteketezwa kwa moto hadi kufa wakiwa ndani ya majumba yao, huku asilimia 5 wakipoteza maisha kutokana na kupewa kichapo cha mbwa na wanajeshi hao makatili wa Myanmar wakisaidiwa na Mabudha wenye misimamo ya kuchupa mipaka.
Hii ni katika hali ambayo, jeshi hilo limekuwa likidai kwamba eti 'limeua watu 400 pekee' katika operesheni zake mkoani hapo.
Jinai kubwa wanazofanyiwa Waislamu hao na wanajeshi na Mabudha wa nchi hiyo wenye misimamo ya kufurutu ada katika mkoa wa Rakhine magharibi mwa Myanmar tangu tarehe 25 mwezi Agosti mwaka huu, hadi sasa zimepelekea kuuliwa maelfu ya Waislamu Warohingya, mbali na kusababisha wengine zaidi ya laki 6 na elfu 50 kuwa wakimbizi.
Parstoday.com
Shirika hilo limeyasema hayo leo Alkhamisi na kuongeza kuwa, miongoni mwa Waislamu hao wa Rohingya waliouawa ni watoto wadogo 730 wenye umri chini ya miaka mitano.
Mkurugenzi wa Matibabu wa shirika hilo, Sidney Wong amesema takwimu hizo zimetokana na uchunguzi wa kina wa taasisi hiyo kwa familia zipatazo 2,434.
Amesema karibu asilimia 70 ya vifo hivyo vimetokana na majeraha ya risasi za jeshi la nchi hiyo, katika operesheni yake maalumu mkoani Rakhine, kuanzia mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka, asilimia 9 ya Waislamu hao wa Rohingya waliuawa kwa kuteketezwa kwa moto hadi kufa wakiwa ndani ya majumba yao, huku asilimia 5 wakipoteza maisha kutokana na kupewa kichapo cha mbwa na wanajeshi hao makatili wa Myanmar wakisaidiwa na Mabudha wenye misimamo ya kuchupa mipaka.
Hii ni katika hali ambayo, jeshi hilo limekuwa likidai kwamba eti 'limeua watu 400 pekee' katika operesheni zake mkoani hapo.
Jinai kubwa wanazofanyiwa Waislamu hao na wanajeshi na Mabudha wa nchi hiyo wenye misimamo ya kufurutu ada katika mkoa wa Rakhine magharibi mwa Myanmar tangu tarehe 25 mwezi Agosti mwaka huu, hadi sasa zimepelekea kuuliwa maelfu ya Waislamu Warohingya, mbali na kusababisha wengine zaidi ya laki 6 na elfu 50 kuwa wakimbizi.
Parstoday.com