Waislam wasiotoa mikono ya salamu wanyimwa uraia Uswizi

Taso

JF-Expert Member
Jun 12, 2010
2,463
2,289
c7d8376889bb2e39f041b5870e5049bd



Manispaa ya mji wa Luasanne, Uswizi, imechana fomu za maombi ya uraia ya Waislam wawili wanandoa kwa sababu ya kukataa kwao kupeana mikono ya salamu na watu wa jinsia tofauti.

Mstahiki Meya wa Luasanne, Gregoire Junod, amesema mamlaka hiyo imekataa kupokea maombi hayo kwa sababu watu hao hawaheshimu usawa wa jinsia. Alisema, waliwahoji waombaji hao mieze kadhaa iliyopita kutaka kujua kama wanafikia vigezo vya uraia na waling'amua kwamba walipungukiwa kwenye eneo la utangamano.

Pia walikuwa na wakati mgumu kujibu maswali yaliyoulizwa na maofisa wa jinsia tofauti, alisema Meya huyo.

Baadhi ya Waislamu wasalihina wanadai Uislam hauruhusu kugusana kimwili na yeyote wa jinsia tofauti, isipokuwa tu na baadhi ya wanafamilia wa karibu.

Mstahili Meya Junod alieleza kwamba uhuru wa kidini na kuamini umesimikwa kwenye sheria za Canton of Vaud, ambayo inajumuisha Lausanne. Lakini "mafanyizi ya kidini hayaangukii nje ya sheria," alisisitiza.

Kwa upande wake Naibu Mstahiki meya, Pierre-Antoine Hildbrand, ambae alikuwepo kwenye jopo lililowahoji wanandoa hao alisema ameridhishwa na uamuzi huo wa kukataa maombi hayo kwa vile "Katiba na usawa kati ya wake na waume uko juu ya ubaguzi."

Wanandoa hao wana siku 30 za kukata rufaa.

Hii si mara ya kwanza kuibuka sintofahamu nchini Switzeland juu ya Waislamu na kupeana mikono.

Mwaka 2016 ilitokea taharuki nchi nzima baada ya sekondari moja Kaskazini mwa nchi hiyo kuwakubalia wanandugu wawili wenye asili ya Syria kutowapa mikono waalimu wao wa kike baada ya kulalamikia utaratibu huo kuwa ni kinyume na misingi ya dini yao.

Ruksa hiyo ilipingana vikali na desturi zilizojichimbia za Kiswizi za wanafunzi kuwapa mikono walimu kama alama ya nidhamu na utii, na katikati ya mtafaruku huo na vilio ya kitaifa mamlaka ya kikanda ilitengua uamuzi wa shule hiyo.

Chanzo: The Guardian
 
Dini wakati mwingine huwa na mambo ya kijinga sana

Sent using Jamii Forums mobile app

I am not sure kama ni ujinga wa dini, mimi sina tatizo na chochote inachotaka dini yeyote.

Ujinga ni kutaka kupeleka ma imani yako na ma utamaduni yako kwenye jamii zingine.

Binti kutoka Switzeland akienda shule Syria ataruhusiwa kuleta ma culture yake ya Ulaya kama kuvaa vi mini shuleni? Waarabu si watamkaanga kwenye pipa la petroli?

Tamaduni zinatofautiana jamani, na ukienda kwa watu saa nyingine inabidi ufiche desturi zako kwenye mfuko wa nyuma ya suruali.

Wanaume wa Afrika Mashariki na Kati, kama Kongo, kwa mfano, wanacheza mziki wakikata mauno. Sasa ukienda New York City ukakata mauno kwenye ukumbi wa starehe watu watakubaashia, watakupiga mabusu! Na usilalamike, for all they know umejitangaza wewe sio ridhiki.

Tamaduni tofauti!
 
Kuna Wayahudi wasiokubali kukaa siti moja na wanawake kwenye ndege, hao sijui watawafanyaje?

Labda kwenye ndege yao ya EL AL ndio wametengwa wa kike kule wa kiume huku, who knows?

Kwenye ndege zingine hakuna kitu kama hicho.

Again, tunarudi pale pale pa awali, kwamba unaweza ku practice dini vyovyote unavyotaka, lakini mambo ya ajabu mbele ya jamii ya wenzio kayafanyie kwenu!
 
“It was narrated that Ma’qil ibn Yassaar said: the Messenger of Allaah (peace and blessings of Allaah be upon him) said: “For one of you to be stabbed in the head with an iron needle is better for him than that he should touch a woman who is not permissible for him.”

Narrated by al-Tabaraani in al-Kabeer, 486. Shaykh al-Albaani said in Saheeh al-Jaami’, 5045, that this hadeeth is saheeh.”

Makafiri mna tabu sana... hao vijana wako sahihi kwa mafundisho ya dini. Nyinyi kama dini yenu inaruhusu fanyeni na sisi tuacheni na dini yetu. Chuki ya nini?
 
Back
Top Bottom