Waislam Dodoma watoa Tamko kumwombea mwislam mwenzao Gaddafi

Wana Jf, kila mara huwa nakumbusha kuwa hoja hujibiwa kwa hoja. Inapojibiwa kwa hisia(emotion) basi hupoteza muelekeo.
Voingozi wa dini ni wanadamu kama walivyo wanadamu wengine, tena wapo viongozi waliooza kiimadili kuliko waamuni wao. Inategemea kiongozi huyo yupo wapi na anawaumini wenye uelewa kiasi gani.
Hoja hapa ni kumwambia sheikh kuwa kama hao ni wahuni je Tunisia, Algeria, Morocco, Egypt, Bahrain, Jordan na hata Saudia ambako king amefanya mabadiliko kuepeuka Jasmine revolution, je nako wanakula vidonge.? Ukisoma hoja za sheikh, haraka utatambua kuwa uwezo wake wa kufikiri na kupata habari ni finyu sana. Kama ilivyo CCM kule vijijini inapowaambia watu tumeleta maendeleo na watu wakapiga makofi ndivyo ilivyo katika jamii zetu zenye uelewa finyu! hatuwezi kukataa ukweli huu.

Ninachosisitiza hapa ni kuwa suala hilo lisifanywe au lisiunganishwe na imani za dini. Hao mamilion ya watu mideast wangemsikia sheikh wa dodoma pengine wangezimia wote. Lakini hata hapa JF na Tanzania kwa ujumla na pengine ndani ya msikiti huo wa sheikh kuna maelfu ya waislam waliochukizwa na kushangazwa na kauli ya sheikh. Hatutawatendea haki kama kauli ya mtu mmoja itafungamanishwa na imani za mamilioni ya watu. Kauli hii ni yake na sidhani kuwa ni ya waislam. Kama alivyowahi kusema Askofu kilaini, JK ni chaguo la mungu, ile imebaki kuwa kauli yake na si kauli ya Wakristo. Tujaribu kuchambua hoja zaidi kuliko kuweka mbele hisia zetu au kutowatendea haki wasiojihusisha na kauli za baadhi ya watu.

wewe uko sahihi maelezo yako ni safi na muafaka,tusitumia uelewa wa mtu mmoja mpumbavu hata kama ni kiongozi wa dini au asasi kujudge waumini wote kwani hawa viongozi wetu huwa wanateleza,huyo shekhe ni mawazo yake ya kijinga tu hivyo ni kumpuuza yeye tu na sio waislamu wote.
 
Hoja kubwa kwa huyu Shehe ya kum-support Ghadafi ni kwa kuwa "alijenga msikiti pale Dodoma"; hayo mengine yote hayana maana. Kwamba ni wa-Libya wangapi wamekufa kwa ajili ya huyo dikteta kwake hiyo si issue.

Tatizo la viongozi wetu wengi wa dini ni kutosimamia UKWELI hata kama ni mchungu. Kiongozi wa dini yuko tayari kusimama hadharani kutetea UONGO wa kila namna alimradi ana vimaslahi fulani na huyo anayemtetea kwa mfano urafiki binafsi, amewahi kutoa vimisaada fulani, na baya zaidi ni "wa dini yangu"! This is very bad! Mara ngapi tumesikia baadhi ya viongozi wa dini waiuteteta mafisadi na viongozi walioshidwa kwa kigezo tu ni mwenzetu; wa dini yetu.

Huwezi kuniambia waislamu wote wa Libya wanaoandamna ni wajinga na huyu shehe mmoja tu wa Dodoma ndiye mwenye akili kushinda maelfu wote hao. Hata hayo maneno aliyotumia kwamba wanaondamana ni WALEVI na WAPENDA MADAWA YA KULEVYA kwenye hoja yake amenakili tu kutoka kwa Ghadafi. Ghadafi ndiye wa kwanza kuyatumia akiongezea kwamba ni "al-Qaeda" akimlaumu sana Osama bin Laden ndio waanzilishi wa vurugu hizo.

Hii ni mara ya kwanza kutomsikia kiongozi wa taifa la kiislamu hususan mashariki ya kati kutolaumu ulimwengu wa magharibi kwa matatizo yanayotokea nchini kwake - ni ajabu, na si kwa bahati ila ukweli uko wazi kiasi kwamba kushindana nao ni kama kupiga ukuta ngumi.

Hebu tusimamie ukweli tuachaneni na blabla za kipuuzi.
 
Wana Jf, kila mara huwa nakumbusha kuwa hoja hujibiwa kwa hoja. Inapojibiwa kwa hisia(emotion) basi hupoteza muelekeo.
Voingozi wa dini ni wanadamu kama walivyo wanadamu wengine, tena wapo viongozi waliooza kiimadili kuliko waamuni wao. Inategemea kiongozi huyo yupo wapi na anawaumini wenye uelewa kiasi gani.
Hoja hapa ni kumwambia sheikh kuwa kama hao ni wahuni je Tunisia, Algeria, Morocco, Egypt, Bahrain, Jordan na hata Saudia ambako king amefanya mabadiliko kuepeuka Jasmine revolution, je nako wanakula vidonge.? Ukisoma hoja za sheikh, haraka utatambua kuwa uwezo wake wa kufikiri na kupata habari ni finyu sana. Kama ilivyo CCM kule vijijini inapowaambia watu tumeleta maendeleo na watu wakapiga makofi ndivyo ilivyo katika jamii zetu zenye uelewa finyu! hatuwezi kukataa ukweli huu.

Ninachosisitiza hapa ni kuwa suala hilo lisifanywe au lisiunganishwe na imani za dini. Hao mamilion ya watu mideast wangemsikia sheikh wa dodoma pengine wangezimia wote. Lakini hata hapa JF na Tanzania kwa ujumla na pengine ndani ya msikiti huo wa sheikh kuna maelfu ya waislam waliochukizwa na kushangazwa na kauli ya sheikh. Hatutawatendea haki kama kauli ya mtu mmoja itafungamanishwa na imani za
mamilioni ya watu. Kauli hii ni yake na sidhani kuwa ni ya waislam. Kama alivyowahi kusema Askofu kilaini, JK ni chaguo la mungu, ile imebaki kuwa kauli yake na si kauli ya Wakristo. Tujaribu kuchambua hoja zaidi kuliko kuweka mbele hisia zetu au kutowatendea haki wasiojihusisha na kauli za baadhi ya watu.
Nimependa ulivo na uwezo wa kuchangia na kutuelekeza.Ila mostly leaders wa dini hii,tukimuondoa Mwinyi na Sheikh Simba, matamko yao huwa hayana maana uongozwa na hisia.Nachofurahia ni kwamba maandamano katka nchi hizi yameanzishwa na Waislam wenyewe,yangechochewa na Magharibi tungesikia Matamko ya kutosha hapa nchini,ohh Makafir wanatuonea tuungane kulaani!!!!!!!!!!!!
 
Duh! Jamaa kalishwa tende mpaka kalewa. Hana tofauti na wale masangoma wa Kenya waliomvika Gaddafi ufalme wa Africa hapo juzi. Ni kuganga njaa tu. Hata mwandishi wa gazeti la Mwananchi hayuko makini, hii si habari ya kujaza kurasa za gazeti.
 
Wana Jf, kila mara huwa nakumbusha kuwa hoja hujibiwa kwa hoja. Inapojibiwa kwa hisia(emotion) basi hupoteza muelekeo.
Voingozi wa dini ni wanadamu kama walivyo wanadamu wengine, tena wapo viongozi waliooza kiimadili kuliko waamuni wao. Inategemea kiongozi huyo yupo wapi na anawaumini wenye uelewa kiasi gani.
Hoja hapa ni kumwambia sheikh kuwa kama hao ni wahuni je Tunisia, Algeria, Morocco, Egypt, Bahrain, Jordan na hata Saudia ambako king amefanya mabadiliko kuepeuka Jasmine revolution, je nako wanakula vidonge.? Ukisoma hoja za sheikh, haraka utatambua kuwa uwezo wake wa kufikiri na kupata habari ni finyu sana. Kama ilivyo CCM kule vijijini inapowaambia watu tumeleta maendeleo na watu wakapiga makofi ndivyo ilivyo katika jamii zetu zenye uelewa finyu! hatuwezi kukataa ukweli huu.

Ninachosisitiza hapa ni kuwa suala hilo lisifanywe au lisiunganishwe na imani za dini. Hao mamilion ya watu mideast wangemsikia sheikh wa dodoma pengine wangezimia wote. Lakini hata hapa JF na Tanzania kwa ujumla na pengine ndani ya msikiti huo wa sheikh kuna maelfu ya waislam waliochukizwa na kushangazwa na kauli ya sheikh. Hatutawatendea haki kama kauli ya mtu mmoja itafungamanishwa na imani za mamilioni ya watu. Kauli hii ni yake na sidhani kuwa ni ya waislam. Kama alivyowahi kusema Askofu kilaini, JK ni chaguo la mungu, ile imebaki kuwa kauli yake na si kauli ya Wakristo. Tujaribu kuchambua hoja zaidi kuliko kuweka mbele hisia zetu au kutowatendea haki wasiojihusisha na kauli za baadhi ya watu.

Umenena vema,
Inanipa wakati mgumu kuamini/kuona jinsi tunavyo by-pass topic na kuanza kuangalia NANI KATOA UHURU WA MAONI YAKE kwa mujibu wa katiba ya JMT, inanisumbua sana hali hii.
 
Sishangai waislam wa dodoma kusimama upande wa gadaffi maana msikiti alioujenga gadaffi pale jamhuri street ni mkubwa sijapata kuona nadhan ndio msikiti mkubwa tanzania. Hivyo basi katika hali ya kawaida sioni tatizo kwa waislamu kumtetea gaddafi kwa sababu amewawezesha. Hata wewe great thinker sidhani kama utamtega mgongo mtu aliyekuwezesha kwa kiasi kikubwa, utajitahidi kumsifu na kumuona wa maana hata kama amekosea utaona aibu kumkosoa.
 
sipendi kuamini, sitaki kuamini na hata nikilazimishwa sikuabli kuamini kuwa Libya hakuna mgogoro mkubwa na kuwa Dikteta Gadhafi anapendwa sana na watu wake.

Babu, mficha maradhi kifo kitamuumbua ima siri ya mtungi aijuae kata.
Au la sivyo ndugu wakigombana chukua jembe ukalime wakipatana wee kavune!
Mifano hiyo ipo hai hadi leo huyo anayejiita msomi aliye somea Libya hajitambui kwamba wanaoijua Libya ni Walibya wenyewe na sio yeye wakuja.
 
Daah, kumbe kumbe hata nchi za kiarabu kuna idadi kubwa vile ya walevi wa pombe?
 
Yoote hiyo coz kajengewa msikiti tu hamna kingine. Ukizingatia na yeye kama shehe wa mkoa lazima alipata ulaji.
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, Sheikh Shaaban alisema tamko la Waislam wa Mkoa wa Dodoma ni kuwataka wenzao nchini na duniani, kuhakikisha hawaungi mkono kikundi hicho cha kihuni.

Kanali Gaddafi amejenga msikiti mkubwa mjini Dodoma na nchini Uganda. Pia, alifadhili ujenzi wa msikiti wa Butiama, baada ya Baba wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Nyerere kumuomba.

Source: Mwananchi

Kwa uelewa wa huyu Sheikh Ukijenga misikiti unakuwa juu ya sheria na unaweza kufanya lolote ikiwemo kuua raia wenzio na kutawala milele Nobody should touch you. Poor Sheikh..
 
Nahisi kujumlisha waislamu wote si haki.
Ninacho shukuru kwa hili wote wakiwemo waislamu wamemgombea huyo shehe kama mpira wa kona.
Bado basaleh$company!
Naipenda hii tumeshaanya kujitambua na kulenga adui wa kweli.
 
Kujumuisha waislamu wote sio sensible thing! Cha kushangaza ni ilikuwaje akawa kiongozi wao? ooh hang on amesomea sheria Libya ok! sasa tatizo linalokuja ni kwamba hao waumini wake sijui noa watakua vipi yarabi salama (muelewo wao utakuwa mdogo), maana kama kiongozi mwenyewe ndio hivi sasa waumini si itakuwa balaa! anyway we need to stop generalising things the guy is a comedian! he has got nothing to do with genuine Muslims out there! how could he leak Gaddafi's back side when he has so far killed about 1000 civilians and so many injured!? Joker!
 
Shehe na degree yako on top unasema gaddaf mtu safi? Kisa msikiti mliopewa? Hivi akishatolewa kwa hiyo rais atayechaguliwa atakuwa teja.? mkubwa ukikosea na ukajua umekosea ni bora ukaomba radhi.
 
Hao wanao itwa wahuni ni watoto wa walibya, tena ni waislamu swafi acha hawa wa huku kujengewa msikiti tu wanaona wamemaliza. Libya Mtu akimaliza shule na kuoa, anapewa nyumba, umeme wa majumbani ni bwerere tena full quality, simu za mkononi ukipiga ndani ya nchi ni chee. Libya iko jangwani lakini hakuna njaa wala uhaba wa maji, matibabu ya uhakika ni free. Mafuta lita moja petrol sawa na Tshs. 200/= za bongo.

Lakini walibya wana sema "ang'oke amekaa mno" wanataka uhuru zaidi siyo kubanwa banwa!

Hapa kwetu mambo shaghala baghala na mkwere analala usingizi mnono pamoja na kelele za mlango kuongezeka. Anawajua wabongo ni maneno tu hawawezi ku-act.
 
inawezekana huyo shehe ana degree ya islamic law-kwa hio hawez jua asemacho-ataamini kuwa alidanganywa na hio source yake of information pindi atakaposikia gadafi kasalim amri kwa waandamanaji
 
Kumbe wanaotaka kumnyofoa jamaa madarakani ni makafiri? Halafu trend inaonyesha kuwa mapinduzi yanayoendelea yanazidi kukumbana na vikwazo. Hadi yafike bongo yameshachakachuliwa vya kutosha
 
Back
Top Bottom