Waingereza: Wazenji somo la kujifunza!

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,854
13,139
Waingereza tunaweza kwa sasa kusema ndo waswahili wa Ulaya!
Ule msimamo wa " chako chako, chako changu" umedhihirika kwa hawa wenzetu waliotutawala enzi za ukoloni.

Siyo siri, hii kura ya kubaki ama kuondoka Jumuiya ya Ulaya, EU, imewaumbua vibaya.

Mtu mbinafsi hujifikiria yeye kwanza, na watu wa visiwani wana ugonjwa huu.

Kura ya kujitoa EU kama maamuzi ya waingereza imeibua hasira ya nia ya kuitenga Uingereza na biashara karibu zote, ikiwemo nia ya kuhamisha makao makuu ya kibiashara toka London kwenda Paris au Berlin.

Pamoja na kura hiyo ni wafanya biashara duniani kukosa imani na hela ya Uingereza, hivyo kuanguka thamani vibaya.

Wenzetu wa visiwa vilivyo karibu wajitathmini na msimamo wao unaolingana na msimamo wa Uingereza.

Kama alivosema Mwalimu , dhambi ya kujitenga Zanzibar itawaadhibu wazanzibari zaidi kuliko Tanganyika, funzo tumeliona live.
 
yaani ningelikuwa rais, wazenji wakaleta hizi za kuleta, ningeitisha kura ya maoni haraka sana kwasababu ningejua watajiondoa, na zigo lingepungua. kusema ukweli, nawapongeza marais wetu hawako na akili kama ya kwangu, mimi usumbufu wa aina hii huwa sitaki na nisingevumilia watu wa aina yao (wanaochapa fimbo mtu asiyefunga mchana au aliyefungua mgahawa hata kama hayuko kwenye swaumu au pengine si wa dini yao). wanafanya vitendo vinavyonikwaza sana. ukienda kwao kumiliki ardhi inasemekana ni ngumu kwa mtu wa bara wao hapa wanamiliki, kigamboni wamejaa tunawabeba lakini kutwa wanalalamika hawaridhiki. jamani wazenji mjifunze ya uingereza, kuna siku tanzania tutakuwa na rais kichwa kingine mtaleta za kuleta atavunja muungano na mtakuja kushtuka shuka abusuhi.
 
Walichofanya hawa jamaa hata wenyewe wanajishangaa!
waitishe tena kura ya maoni kuangalia kama wanaona wamefanya kosa na wanataka kurudi Eu, si ndo democrasia? ati wana chadema......si ndo mnayosema democracy, kushabikia kila kitu alimradi tu umeona wenzako wanashabikia.

na ninyi mkienda dodoma mkapigwa virungu na mabom ya machozi huko, mtuletee mrejesho, kwasababu nahisi mnatafuta kupigwa. tunahitaji rais dictator zaidi ya magufuli ili ainyooshe Tanzania. badala ya kufanya kazi ati watu wamejaza hotel za dodoma, hizo hela wametoa wapi? na kwa maslahi gani, na ni faida gani kwa watanzania kwenu bavicha kuzuia hicho mnachoenda kuzuia, na kwanini msitumie formal way, badala ya hayo mashindano....mnashindana mwisho ni fujo, zitawafaidishan ini...mkitulia na mkifanya fujo kipi kina faida kwenu?
 
waitishe tena kura ya maoni kuangalia kama wanaona wamefanya kosa na wanataka kurudi Eu, si ndo democrasia? ati wana chadema......si ndo mnayosema democracy, kushabikia kila kitu alimradi tu umeona wenzako wanashabikia.

na ninyi mkienda dodoma mkapigwa virungu na mabom ya machozi huko, mtuletee mrejesho, kwasababu nahisi mnatafuta kupigwa. tunahitaji rais dictator zaidi ya magufuli ili ainyooshe Tanzania. badala ya kufanya kazi ati watu wamejaza hotel za dodoma, hizo hela wametoa wapi? na kwa maslahi gani, na ni faida gani kwa watanzania kwenu bavicha kuzuia hicho mnachoenda kuzuia, na kwanini msitumie formal way, badala ya hayo mashindano....mnashindana mwisho ni fujo, zitawafaidishan ini...mkitulia na mkifanya fujo kipi kina faida kwenu?
Mkuu hao jamaa hawajielwi kabisaa!!!
 
Kama alivosema Mwalimu , dhambi ya kujitenga Zanzibar itawaadhibu wazanzibari zaidi kuliko Tanganyika, funzo tumeliona live.
Hivi mwalimu ni nani kwa Zanzibar? na imemuhusu nini? Watanganyika wana matatizo sana. Akili zao kama visiki wao kubwa mwalimu kasema, mwalimu katenda! ovyooo. Ondokaneni na fikra mgando na sisi Zanzibar tulikuwa na Karume wetu, lakini hatumuabudu kifikra wala kimawazo. Yeye ni binadamu na ameishi kwa wakati wake kama wengine!
 
Wajitenge tu maana wamekuwa mzigo kwa Tanganyika
Tatizo lenu si wa kweli. Tumekuoneni kwenye bunge la katiba mnavyo utetea muungano, wakati wazanzibari waziwazi wamesema hawautaki au kuwa lazima uwepo uwe wa kataba.

Mkapigisha kura mpaka wafu ili mradi muulinde muungano. Mnarudi kwenye Baraza mnasema Zanzibar na wajitenge tu. Tumesema mara ngapi? na kila tukisema majeshi , vifaru na maji ya kuwasha tunaletewa. Muwe wa kweli sio kujikaza kisabuni
 
Hivi mwalimu ni nani kwa Zanzibar? na imemuhusu nini? Watanganyika wana matatizo sana. Akili zao kama visiki wao kubwa mwalimu kasema, mwalimu katenda! ovyooo. Ondokaneni na fikra mgando na sisi Zanzibar tulikuwa na Karume wetu, lakini hatumuabudu kifikra wala kimawazo. Yeye ni binadamu na ameishi kwa wakati wake kama wengine!
Mbona mko wengi huku kwetu , bora tuwatawale tu.
Mwalimu alisema na Karume aliridhia.
 
ukienda kwao kumiliki ardhi inasemekana ni ngumu kwa mtu wa bara wao hapa wanamiliki, kigamboni wamejaa tunawabeba lakini kutwa wanalalamika hawaridhiki.
Hivi kweli wewe umekwenda shule au ulikuwa unaogopa umande? Hivi inaingilia akilini utoke bara yenye eneo la square Km 947,303 uje Zanzibar kugombania eneo dogo lenye ukubwa wa square Km 1,666? Hapa ndipo nashindwa kupima uwezo wa watanganyika kupima na kutafakari mambo!
 
Mbona mko wengi huku kwetu , bora tuwatawale tu.
Mwalimu alisema na Karume aliridhia.
Tuko wengi huko kwa sababu wenyewe hamjielewi!

Karume aliridhia vipi, unamjua Karume au unamsikia. Wakati wa uhai wa Karume hakuna ofisa yoyote kutoka bara ikiwa na pamoja na jeshi aliokuwa ana fanya kazi Zanzibar.Tulikuwa bado tunajitawala na tulikuwa na mamlaka kamili.

Ofisi zote za kibalozi za nje zilikuwa na tawi lake Zanzibar au ofisi kamili. Upuuzi wote wa Nyerere kama vile Azimio la Arusha alilipiga marufuku lisiingie Zanzibar na kusema mwisho Chumbe na ilikuwa hivyo na Nyerere hakusema nyoko. Huyo ndio alikuwa Karume, na huo ndio muungano tuliokuwa tunaoutaka.

Karume alimfukuza Sheikh Yahya Hussein na kumpa saa 24 tu kuhama Zanzibar ambapo aliishi zaidi ya miaka 30, Alimfukuza Mwakanjuki, Mfaranyaki na wabara wengine na hawakukanyaga Zanzibar mpaka alipozikwa. Huyo ndio Karume tunaemtaka!
 
Tuko wengi huko kwa sababu wenyewe hamjielewi!

Karume aliridhia vipi, unamjua Karume au unamsikia. Wakati wa uhai wa Karume hakuna ofisa yoyote kutoka bara ikiwa na pamoja na jeshi aliokuwa ana fanya kazi Zanzibar.Tulikuwa bado tunajitawala na tulikuwa na mamlaka kamili.

Ofisi zote za kibalozi za nje zilikuwa na tawi lake Zanzibar au ofisi kamili. Upuuzi wote wa Nyerere kama vile Azimio la Arusha alilipiga marufuku lisiingie Zanzibar na kusema mwisho Chumbe na ilikuwa hivyo na Nyerere hakusema nyoko. Huyo ndio alikuwa Karume, na huo ndio muungano tuliokuwa tunaoutaka.

Karume alimfukuza Sheikh Yahya Hussein na kumpa saa 24 tu kuhama Zanzibar ambapo aliishi zaidi ya miaka 30, Alimfukuza Mwakanjuki, Mfaranyaki na wabara wengine na hawakukanyaga Zanzibar mpaka alipozikwa. Huyo ndio Karume tunaemtaka!
Usimzingizie Karume kwa mengine ambayo hakufanya.
Ila kumbuka tu ni ninyi wenyewe mlimuondoa duniani, sijui kwa mapenzi gani mliyokuwa nayo kwake.
 
Hivi mwalimu ni nani kwa Zanzibar? na imemuhusu nini? Watanganyika wana matatizo sana. Akili zao kama visiki wao kubwa mwalimu kasema, mwalimu katenda! ovyooo. Ondokaneni na fikra mgando na sisi Zanzibar tulikuwa na Karume wetu, lakini hatumuabudu kifikra wala kimawazo. Yeye ni binadamu na ameishi kwa wakati wake kama wengine!
Isingekuwa Karume kumpigia magoti Mwalimu ili apate ulinzi baada ya mapinduzi, sijui mgekuwa mmeuana wangapi.
 
yaani ningelikuwa rais, wazenji wakaleta hizi za kuleta, ningeitisha kura ya maoni haraka sana kwasababu ningejua watajiondoa, na zigo lingepungua. kusema ukweli, nawapongeza marais wetu hawako na akili kama ya kwangu, mimi usumbufu wa aina hii huwa sitaki na nisingevumilia watu wa aina yao (wanaochapa fimbo mtu asiyefunga mchana au aliyefungua mgahawa hata kama hayuko kwenye swaumu au pengine si wa dini yao). wanafanya vitendo vinavyonikwaza sana. ukienda kwao kumiliki ardhi inasemekana ni ngumu kwa mtu wa bara wao hapa wanamiliki, kigamboni wamejaa tunawabeba lakini kutwa wanalalamika hawaridhiki. jamani wazenji mjifunze ya uingereza, kuna siku tanzania tutakuwa na rais kichwa kingine mtaleta za kuleta atavunja muungano na mtakuja kushtuka shuka abusuhi.
tatizo sio rais anashindwa ila katiba inambana usifikiri hao marais wengine walikuwa hawana mawazo hayol kwani zanzibar imekuwa ikiwasumbua sana hata rais wa kwanza ambaye ni mwasisi wa muungano aliwahi kusema angekuwa na uwezo angesukumizia mbali visiwa hivyo
 
Usimzingizie Karume kwa mengine ambayo hakufanya.
Ila kumbuka tu ni ninyi wenyewe mlimuondoa duniani, sijui kwa mapenzi gani mliyokuwa nayo kwake.
Umepiga bull!
Hawa wenzetu, kama walivyo waingereza kwa unafiki hawajambo.
Wanatumia jina la marehemu Karume kwa convenience tu, lakini dhamira yake ya dhati hawaiongelei.
 
Akili yako na yangu ni sawa . Mi pia kusumbuka kumshikia mtu kinachomnufaisha bila yeye kukithamini sichelewi kumtupia ktk methali nazikubali sana kwenye maamuzi yangu ni "Mtoto akililia wembe mpe" Ningekuwa Rais wa Tanzania ningeshaitisha kura ya maoni najua huku bara hatuna faida na muungano huu hvyo kura za bara zngekuwa wajitenge na kura za zenji pia zngekuwa hvyo maana wanaamini wananyonywa.Harafu baada ya kujitenga tu narudisha kwa watu wa bara ardhi yote inayomilikiwa na wazenji.
 
Back
Top Bottom