Waingereza wa tindikali Zanzibar walia na serikali

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Waingereza wa tindikali walia na serikali
KWA UFUPI

Waingereza hao ambao walikuwa walimu wa kujitolea katika shule ya St Monica, Tomondo, Zanzibar, walimwagiwa tindikali na watu wawili wasiojulikana wakati walipokuwa kwenye matembezi ya jioni katika eneo la Mji Mkongwe Agosti 7, mwaka huu.


Dar es Salaam. Familia ya Waingereza, Kirstie Trup na Katie Gee, wote wenye umri wa miaka 18, waliomwagiwa tindikali huko Zanzibar, wameiomba Serikali ya Uingereza kuishinikiza Tanzania kuharakisha kuwawajibisha waliohusika na tukio hilo.

Waingereza hao ambao walikuwa walimu wa kujitolea katika shule ya St Monica, Tomondo, Zanzibar, walimwagiwa tindikali na watu wawili wasiojulikana wakati walipokuwa kwenye matembezi ya jioni katika eneo la Mji Mkongwe Agosti 7, mwaka huu.

Baada ya tukio hilo lililowajeruhi kiasi kikubwa katika maeneo ya kifua na mikononi, walipewa matibabu katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, kisha wakarudishwa kwao kwa matibabu zaidi.

Alipowatembea wasichana hao hospitalini, Rais Jakaya Kikwete alisema tukio hilo limetia aibu kwa mataifa ya nje na kuliamuru Jeshi la Polisi kuhakikisha linawakamata na kuwafungulia mashtaka wote waliohusika.

Taarifa iliyosambazwa kwenye mtandao wa habari wa Polisi wa Kimataifa (Interpol) Kanda ya Tanzania, inaeleza kuwa familia ya wasichana hao hairidhishwi na namna Serikali ya Tanzania inavyolishughulikia suala hilo kwa kuwa hadi sasa imeshindwa kuwatambua wahusika.

Mtandao huo umemnukuu baba yake Trup, Marc alipokuwa akizungumza na Redio 4 ya BBC, kuwa kuna wingu zito lililotanda kuhusu kesi hiyo, kwa kuwa hadi sasa Serikali ya Zanzibar imeshindwa kuonyesha picha za wahusika ili zitambuliwe na wasichana hao, ingawa imekwisha kuwahoji watu kadhaa.

“Picha haziwezi kutumwa katika muundo bora unaokubaliwa na Interpol au Mamlaka za Uingereza, kutokana na sababu hizo hakuna hata mmoja ameshaziona hizo picha,” alisema Marc.

Naye baba mlezi wa Gee, Doug Morris, alisema: “Kama Wizara ya Mambo ya Nje na Ofisi ya Jumuiya ya Madola wako makini kusaidia watu hao kufikishwa mbele ya sheria kwa niaba ya raia wa Uingereza, tulitegemea wafanye kila linalowezekana, lakini hakuna dalili zozote zinazoonekana za kutaka kuharakisha jambo hili.”

Aliongeza:“Kama wanamaanisha wanachokisema na ni muhimu kwao kuwatafuta waliotekeleza kitendo hicho ili wawafikishe kwenye vyombo vya sheria, basi watusaidie kwa kila njia ambayo wanaweza.

“Kila mtu ameanza kufikiri kuwa wanatuchezea, kila wiki tunakatishwa tamaa. Huu ni uharibifu ambao hauwezi kupita tu bila mtu kuadhibiwa kwa manufaa ya wasichana wale au mtu mwingine yeyote.

“Aina gani ya ujumbe unaoletwa, kwamba unaweza kufanya jambo baya halafu usifanywe kitu chochote?”

Alisema kuwa wangependa suala hilo lifike mwisho haraka iwezekanavyo ili haki itendeke.
 
Labda usanii wa jeshi la polisi unaweza kuisha kama hawa wazungu wakiendelea kupga kelele maana sisi tumesha zoea mambo kupita kama upepo
 
Unafiki wa wazanzibari na serikali yao unaondoa uwezo wao wa kufanya kazi kwa uadilifu.
 
maadamu Ponds yupo jela wawe wavumilivu... atafungwa tu... name ndii maana kwa sasa nchi imetulia
 
maadamu Ponds yupo jela wawe wavumilivu... atafungwa tu... name ndii maana kwa sasa nchi imetulia

umevurugwa wewe,Ponda ana tishio gani sasa???Polisi wa mwema ndo tishio maana hawafanyi kazi kwa weledi wanafanya kwa hisia
 
jeshi la polisi ni hodari wa matamko tutahakikisha tunawakamata mpaka leo kimya,tunaendelea na upepelezi hiyo polisi ya tz.
 
London teenagers Kirstie Trup and Katie Gee are recovering after attack during summer volunteering holiday





Kirstie-Trup-011.jpg


Kirstie Trup suffered severe chemical burns to her shoulder and back from the sulphuric acid. Photograph: Barcroft Media



The families of two British women targeted in an acid attack in Zanzibar have spoken of their frustration that the attackers have not been brought to justice.


Londoners Kirstie Trup and Katie Gee, both 18, are recovering after being targeted by two men on a moped on 7 August during a volunteering holiday.


Their families have called on the UK government to apply more pressure on the Tanzanian authorities.


Doug Morris, the partner of Gee's mother, told BBC Radio 4's Today programme: "If the Foreign and Commonwealth Office are as committed to helping to bring these people to justice on behalf of two British citizens, then you would expect them to move hell and high water to do that.


"There just doesn't seem to be any sense of urgency to conclude matters."


There is still confusion over how to get a photograph of a suspect to the women for identification, according to Trup's father, Marc.



He said: "The photograph cannot be sent in the correct format that is acceptable by Interpol, or the British authorities, and as a consequence of that nobody has seen the photo."


The teenagers, from north London, were nearing the end of a month-long stint teaching English when they were attacked.


Trup suffered severe chemical burns to her shoulder and back from the sulphuric acid, which was launched at the pair as they walked back from a restaurant on the predominantly Muslim island.


Police in Zanzibar have interviewed several people, including witnesses, and are believed to have identified a possible culprit.


Trup told Today: "I'm particularly upset with the Tanzanian authorities. I think they just hope this will go away. The Foreign Office do send us emails, but the emails say the same every single time and they seem to imply that the British Foreign Office has clout, it has a voice, but clearly none of that is working because we are not getting any progress whatsoever.


"I suspect the Tanzanian authorities don't take the Foreign Office remotely seriously. We want the judicial system to work properly. I would like to see whoever threw that acid brought to justice. I don't blame the country. I don't blame the religion. I blame the person. He needs to be brought to justice.


"Above all, the girls want to know why he did it and we would like to know why he did it. Was it racial, was it a religious thing? We have no idea why this person did it."


Morris said: "If they mean what they say, if it's important for them to find the perpetrators of this attack, this crime, and bring them to justice – as they said at the time – then they should be assisting us in every way that they possibly can.


"Everybody is trying to sort of give the impression that they are dealing with this, and we are served platitudes on a bi-weekly basis.


"This crime can't go unpunished, for the girls' sake as much as anything else. What sort of message is that, that you can do something horrific, you can do something horrible, and you can get away with it? We don't want it to drag on and on. We want justice done and we want justice done now."


The families said they had no idea why the girls were targeted, as they were behaving respectfully and dressed in accordance with local customs.


Trup said his daughter was recovering from her injuries. "Kirstie is doing well. She's moved to university. She seems to be progressing well mentally and physically. Kirstie is still having treatment at the local hospital. She has to wear a pressure garment over her burns, which she has to wear 23 hours a day for one whole year," he said.


"She goes regularly once a week to hospital for continual physiotherapy on her burns, but she's progressing well physically and mentally she appears to be moving well. She has difficult times."


Morris said: "Katie is remarkable. She's very strong mentally and just coping with the process of healing."

 
Tusitarajie poliCCM kuwakamata wahalifu hao, kwa kuwa tumepata ushahidi usio na shaka yoyote kuwa ndani ya nchi hii, kama uhalifu unafanywa na mtandao wa vigogo wa CCM, hawawezi kamwe kutiwa mbaroni.

Sisi wenyewe si tumemsikia Juma Kapuya akitamba kuwa wao ndiyo wenye nchi, kwa hiyo hakuna wa kuwakamata, akaendelea kutamba kuwa watoto wao ndiyo wanauza madawa ya kulevya, je tumewahi kusikia hata siku moja, kigogo yeyote wa serikali ya CCM, ametiwa mbaroni, kwa kuhusishwa na biashara ya dawa za kulevya?!

Hebu tujikumbushe baadhi ya matukio ya uhalifu yaliyotokea hapa nchini, ambapo hadi hivi sasa hawajakamatwa washukiwa wowote wa matukio hayo.

Alimwagiwa tindikali msaidizi wa mufti wa Zanzibar, Sheikh Soraga, hadi hivi sasa, wahalifu hao hawajatiwa mbaroni.

Aliuawa Padri Mushi kwa kupigwa risasi huko Zanzibar, hadi hivi sasa hakuna chochote kinachoendelea kwenye kesi hiyo.

Waliuawa waumini kanisani kule Arusha kwa bomu la kurushwa, hadi hivi sasa hakuna mtu yeyote aliyeshtakiwa,zaidi ya yule dereva wa bodaboda, ambaye alieleza kuwa yeye alimpakia abiria ambaye ndiye aliyerusha hilo bomu. Sha kushangaza sana Polisi, hawajataka kabisa kuzifanyia kazi taarifa hizo.

Wameuawa wananchi kwa bomu la kurusha kule Arusha, kwenye mkutano wa hadhara wa chama cha Chadema, hadi leo hajakamatwa mtu yeyote, kuhusiana na tukio hilo.

Mwandishi Daudi Mwangosi aliuawa na bomu, lililofyatuliwa na askari polisi, na ushahidi wa wazi wa picha upo, hadi leo hakuna yeyote aliyetiwa mbaroni, kuhusiana na mkasa huo. Hata ile kesi ya yule polisi aliyekuwa wakati wote anapopelekwa mahakamani anakuwa "masked" naye kesi yake imefutwa kimya kimya!!

Mwandishi mwingine nguli Absolom Kibanda, aliteswa na watu wasiojulikana, hadi wakamnyofoa jicho, hivi sasa ni zaidi ya miezi imepita, licha ya kututambia kwa mbwembe nyingi afande Kova, wakati huo kuwa ni "LAZIMA" watawatia mbaroni watu wote waliohusika na tukio hilo, lakini hadi sasa, hajatiwa mbaroni mtu yoyte.

Kapuya amekumbwa na kashfa nzito ya kukabaka kabinti ka shule, na hapo hapo kukatishia kukauwa kabinti hako, huku akitumia namba ya simu iliyosajiliwa na TCRA kwa jina la Kapuya, hadi hivi sasa polisi wamepata "mchecheto" mkubwa wa kumtia mbaroni Kapuya, licha ya binti huyo kufungua RB kwenye kituo cha Oysterbay!

Lakini cha kushangaza sana, Wilfred Lwakatare aliburuzwa fasta fasta mahakamani, akishtakiwa kwa makosa ya ugaidi, kwa ushahidi wa clip tu iliyopostiwa mtandaoni!!

Cha kushangaza zaidi ni pale mbunge Sugu, alipoburuzwa polisi fasta sana, kwa kile polisi walichokiita kuwa Sugu amepost kwenye page yake ya facebook, lugha ya matusi kwa kumwita Pinda m.p.u.m.b.a.v.u!!!!

Huu ni ushahidi usio na mashaka yoyote kuwa kwa Tanzania yetu ya leo, ile ibara ya 13 ya Katiba yetu ya nchi inayosema watanzania wote wako sawa mbele ya sheria, ni usanii wa hali ya juu!!

Na ukweli halisi wa mambo ni kuwa maCCM, yako above law, na siye wengine tusio wanaCCM,ndiyo sheria inatukaba kisawaswa, kiasi hata ukimwangalia vibaya kidogo tu mwanaCCM anayepita mbele yako, inaweza hata kupelekea kuhukumiwa "mvua" ya miaka kadhaa kwa "kosa" hilo!!!!
 
Waingereza wa tindikali walia na serikali
KWA UFUPI

Waingereza hao ambao walikuwa walimu wa kujitolea katika shule ya St Monica, Tomondo, Zanzibar, walimwagiwa tindikali na watu wawili wasiojulikana wakati walipokuwa kwenye matembezi ya jioni katika eneo la Mji Mkongwe Agosti 7, mwaka huu.


Dar es Salaam. Familia ya Waingereza, Kirstie Trup na Katie Gee, wote wenye umri wa miaka 18, waliomwagiwa tindikali huko Zanzibar, wameiomba Serikali ya Uingereza kuishinikiza Tanzania kuharakisha kuwawajibisha waliohusika na tukio hilo.

Waingereza hao ambao walikuwa walimu wa kujitolea katika shule ya St Monica, Tomondo, Zanzibar, walimwagiwa tindikali na watu wawili wasiojulikana wakati walipokuwa kwenye matembezi ya jioni katika eneo la Mji Mkongwe Agosti 7, mwaka huu.

Baada ya tukio hilo lililowajeruhi kiasi kikubwa katika maeneo ya kifua na mikononi, walipewa matibabu katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, kisha wakarudishwa kwao kwa matibabu zaidi.

Alipowatembea wasichana hao hospitalini, Rais Jakaya Kikwete alisema tukio hilo limetia aibu kwa mataifa ya nje na kuliamuru Jeshi la Polisi kuhakikisha linawakamata na kuwafungulia mashtaka wote waliohusika.

Taarifa iliyosambazwa kwenye mtandao wa habari wa Polisi wa Kimataifa (Interpol) Kanda ya Tanzania, inaeleza kuwa familia ya wasichana hao hairidhishwi na namna Serikali ya Tanzania inavyolishughulikia suala hilo kwa kuwa hadi sasa imeshindwa kuwatambua wahusika.

Mtandao huo umemnukuu baba yake Trup, Marc alipokuwa akizungumza na Redio 4 ya BBC, kuwa kuna wingu zito lililotanda kuhusu kesi hiyo, kwa kuwa hadi sasa Serikali ya Zanzibar imeshindwa kuonyesha picha za wahusika ili zitambuliwe na wasichana hao, ingawa imekwisha kuwahoji watu kadhaa.

“Picha haziwezi kutumwa katika muundo bora unaokubaliwa na Interpol au Mamlaka za Uingereza, kutokana na sababu hizo hakuna hata mmoja ameshaziona hizo picha,” alisema Marc.

Naye baba mlezi wa Gee, Doug Morris, alisema: “Kama Wizara ya Mambo ya Nje na Ofisi ya Jumuiya ya Madola wako makini kusaidia watu hao kufikishwa mbele ya sheria kwa niaba ya raia wa Uingereza, tulitegemea wafanye kila linalowezekana, lakini hakuna dalili zozote zinazoonekana za kutaka kuharakisha jambo hili.”

Aliongeza:“Kama wanamaanisha wanachokisema na ni muhimu kwao kuwatafuta waliotekeleza kitendo hicho ili wawafikishe kwenye vyombo vya sheria, basi watusaidie kwa kila njia ambayo wanaweza.

“Kila mtu ameanza kufikiri kuwa wanatuchezea, kila wiki tunakatishwa tamaa. Huu ni uharibifu ambao hauwezi kupita tu bila mtu kuadhibiwa kwa manufaa ya wasichana wale au mtu mwingine yeyote.

“Aina gani ya ujumbe unaoletwa, kwamba unaweza kufanya jambo baya halafu usifanywe kitu chochote?”

Alisema kuwa wangependa suala hilo lifike mwisho haraka iwezekanavyo ili haki itendeke.

''MKRISTO HAWEZI PATA HAKI ZANZIBAR... Kauli hii nitaendelea kuisimamia milelele''
 
Back
Top Bottom