Wahujumu uchumi waanza kuachiwa...... Watuhumiwa 5 wameachiwa leo baada ya DPP kusema hana nia ya kuendelea na kesi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewafutia mashtaka na kuwaachia huru, washtakiwa watano waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kujiunganishia isivyo halali bomba la mafuta, mali ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Uamuzi huo umetolewa leo, Septemba 23, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza Mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Walioachiwa huru na mahakama hiyo ni Audai Ismail (43)mkazi wa Kibaha, Chibony Emmanuel, Roman Abdon, Amina Shaban na Zubery Ally.
 
Swali ni je, wana kosa au hawana? Hii ya kusamehe wengine na wengine kuendelea kusota gerezani haina haki yoyote! Eti waandike barua ya kuomba msamaha; na kama hawana kosa je? Maana wako wale wanaodaiwa kuwa walikuwa wanafanya kazi na serikali, na hivyo mwenye kosa si wao bali serikali?
 
Nasikia huko eithopia ukikamatwa na rushwa au kesi kama hizi za uhujumu uchumi unatupwa kwenye jela na kusahaulika huko huko, yaani wana adhabu mbaya na ngumu ndio maana hiyo nchi huoni rushwa za hapa na pale
Unaiongelea Ethiopia gani mkuu
 
kabendera kazi kwake sasa,ametuibia sana huyu mhujumu uchumi,ashukuru msamaha umetolewa,arudishe hela zetu ili awe huru
 
Nasikia huko eithopia ukikamatwa na rushwa au kesi kama hizi za uhujumu uchumi unatupwa kwenye jela na kusahaulika huko huko, yaani wana adhabu mbaya na ngumu ndio maana hiyo nchi huoni rushwa za hapa na pale
Ila wanaongoza kukimbia kwao
 
kabendera kazi kwake sasa,ametuibia sana huyu mhujumu uchumi,ashukuru msamaha umetolewa,arudishe hela zetu ili awe huru
Hakuna lolote, wameshaona hawana ushahidi wakajidai eti tunawasamehe wakilipa
 
Tatizo hatumuelewi mkuu wa nchi tumelogwa na marehemu.Ebu angalia watendaji wanavyokazana kupeleka watu mahakamani hata bila kuwa na ushahidi mzuri,tazama watendaji wanavyoshupalia kupinga dhamana itachukua muda mrefu kucheza tune inayopigwa.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewafutia mashtaka na kuwaachia huru, washtakiwa watano waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kujiunganishia isivyo halali bomba la mafuta, mali ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Uamuzi huo umetolewa leo, Septemba 23, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza Mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Walioachiwa huru na mahakama hiyo ni Audai Ismail (43)mkazi wa Kibaha, Chibony Emmanuel, Roman Abdon, Amina Shaban na Zubery Ally.
Yule mmiliki wa princes muro anaitwa nani
 
Back
Top Bottom