mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,219
- 6,650
Hongera kwa kutetea, kwa nguvu zako zote, viongozi wa chama cha siasa chenye itikadi na malengo ya kitaifa, lakini wao wakikitumia kwa maslahi binafsi.Kitendo cha Wahisani/Wadau wetu wa Maendeleo kuhudhuria kesi ya Mbowe lengo lilikuwa ni kutuma ujumbe kuwa kesi hii tunaofuatili na tunasubiri kuona mwisho wake(hukumu itakuwa ni ipi).
Baada ya hukumu kutolewa, ni wazi na wao wataamua nini cha kufanya na kwakuwa hawezi kuhoji maamuzi yatayotolewa, tusitegemee wataongea chochote bali tutaona vitendo tu.
Kwa mwenye akili, atajua nini kitafuata.
Napalta hisia ya kuongezeka na kuibuka kwa tozo mpya(sababu utaijua wakati ukifika in case unashindwa kuelewa nini kitatokea).
Maisha yakibadilika, wananchi watajua ni nani kabadilisha maisha yao- mpaka hapo, mwenye faida au hasara utakuwa umeshamjua.
Tusubiri .
View attachment 1923825
Kimsingi, Wanachama na Wafuasi wa hao viongozi, wamegeuzwa misukule. Hawahoji kauli na matendo machafu ya hao viongozi wala kukemea. Kutwa ni kuwapamba kama vile wao ni malaika.
Kwa bandiko lako hilo unaomba hao wadau wa maendeleo wasitishe ili iweje? Napende nisiamini kuwa hata wewe, hapo ulipo, unaishi maisha tegemezi na unayafurahia. AIBU