FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,872
- 109,170
FaizaFoxy, unaonekana kuwazimia sana wahindi, hili ndo tatizo linalosababisha hata wazawa wanakosa haki zao kwa sababu ya hizo stereotype kama zako za kudhani wahindi/watu weupe ni bora kuliko wazawa, mswahili akishaona ngozi nyeupe anachanganyikiwa. siku hizi mambo hayo yanakwisha kwa hiyo anza kujiandaa kwa mabadiliko watu wameamka sasa, na hizo nyumba kama zilikuwa zao kwa nini wanaomba kuuziwa si wazichukue tu?
Kwa nini nisiwazimie? hivi wewe hujuwi hata jina Tanzania katowa muhindi? hakuna cha stereotype, ukweli unabaki kuwa ukweli. Mtakufa navyo vijiba vya roho, kwani wahindi hatuwapati kwa kuchapa kazi na ndio maana wanaendelea haraka haraka, kokote wanapo kuwepo, iwe Tanzania au kwingine kokote, wahindi wana super speed katika maendeleo yao binafsi, jee umesha jiuliza ni kwa nini? badala ya kukaa na kuwashutumu? Wacheni roho za kichawi, kumchukia tu mtu na kumfanyia hiyana na uhasidi eti kwa sababu anakaa Upanga! Looo, mnanini nyie? nani aliyewakataza kukaa Upanga? mbona waafrika wengi tu wapo huko? hata hamuoni haya wala hamjuwi vibaya? nyumba mziuze wenyewe kwa njaa zenu halafu leo ohhh, wahindi.