ulitaka waje kufanya nini? kuaga ili iweje? wote wangeenda ingekuwaje? angefufuka? JF itumike kujenga uelewe na kujiamini kwa wa TZ kuliko kuwa sehemu ya majungu. Bila kujiamini tutaendelea kufanyiwa mbaya na watawala kwa sasabu hakuna mtawala anayetaka wanachi wawe wajuzi wa mambo. Nchi hii ni yetu tujipange kuiweka vile tunavyotaka. Bei kupanda holela kwa vyakula wakati vyote vinapatikana hapa kwetu ni hujuma na ufisadi mkubwa-tunaangalia, sasa umeme. Zambia waligoma kwa mkate kupanda bei, Tazama Misri, Tunisia, Algeria, Libya, Syria Nigeria -hawaogopi kufa japo wanavyo vya kuacha sembuse wewe na mimi ambao hatuna hata chumba cha kulala tunaogopa hata risasi ya moshi na mpira: eti tunataka kusonga kwa vile tumethubutu, na tume? POLE SAAAANA