Waheshimiwa Wabunge kulala Bungeni: Je ni kutafakari au kusinzia?

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Sasa hivi kuna lugha mpya imekuja tunapoona waheshimiwa wakiwa wamesinzia huku vikao vya bunge vikiendelea pale bungeni, kwa mfano gazeti moja la kilasiku kutoa picha ya muheshimiwa naibu waziri wa ushirikiano wa Africa Mashariki, Dk. Abdulla Juma Saadalla akiwa ameuchapa usingizi kabisa pale bungeni siku ya jumanne katika kikao cha kuchangia bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2011 -2012 lakini lugha ilyotumika pale ni kua alikua ANATAFAKARI jambo!

Haya tena siku ya jumatano gazeti hilohilo limetoa picha ya muheshimiwa waziri wa Nnchi,ofisi ya Raisi (Mahusiano na uratibu) Stephen Wassira naye kwenye picha gazeti la jumatano akiwa anaonekana ameuchapa usingizi kabisa, lakini lugha iliyotumika pale ni kua ANATAFAKARI!

Jamani wanaJF wenzangu nisaidieni kuhusiana na hii lugha!

106dlxt.jpg
 
wewe nawe akili zako kama za fizafoxy.....hukusoma lugha ya picha nini???
 
Pale inamaanisha amelala!

Ni lugha ya KEJELI na maudhui ya habari ile ni kumdhalilisha mheshimiwa... kwa kuwa I bet hata kama ingekuwa ni mwenye kuandika habari hii most likely na yeye angepitiwa. They spend alot of time ndani ya mjengo wakiwa wamekaa ukichanganya na umri kupitiwa na usingizi si jambo la ajabu sana.

Wengi wetu wamekuwa wakipitwa na usingizi wakati tulipokuwa shule mathalan wakati wa muhadhara yaani lecture na waswahili wanasema "usingizi hauna baunsa" hivyo sio ajabu kwa mzee kama mh.wassira ama mh.TOT kujikuta kapitiwa na kausingizi...

Muandishi angeweza kumpotezea tu kama binadamu mwingine....
 
Ajabu ni kwamba wanasinzia lakini bado wanendelea kugonga meza bila hata kujua ni kitu gani kimeongelewa!
Teh teh teh!!! uzinduka pale makofi yanapopigwa kwa hivyo anapotezea kwa kupiga makofi akiulizwa kilichozungumzwa haelewei kazi kweli kweli, mashangingi na posho za kodi ya wananchi ndo zinawavimbisha na kuwakilisha wananchi kwa shibe (usingizi totolo)
 
Duh hii kali! Usingizi hauna Baunsa!
kamstue huone ndo utajua sio baunsa au ndiyo. si unajua mtu akikurupuka kutoka usingizini? yani ni aibu kwa Taifa jamani hivi usiku halali mpaka anavizia usingizi kwenye vikao vya bunge? kazi kweli kweli.
 
mjengo wetu umekaa kianasa zaidi..mara mh. ajigeuze huku,kule akijizungushazungusha sana anakuwa kama mtoto anaebembelezwa iili alale, lazima atalala..angalia jengo la bunge la uingereza, cheki kenya huwezi kulala, ukilala tu unamwangukia mwenzako naye anakukandamiza bonge la knuckle, mabunge yao moto, letu bariiiiidi..bora hawa CDM kidogo waanza kutoa ule mfumo wa business as usual...endeleeni kutafakari sana waheshimiwa
 
Ni kweli mkuu MCHEMSHO kuhusiana na mabunge kama la Uengereza na hata Kenya mabunge yao yamekaa kikazi zaidi! lakini hili bunge letu limekaa kianasa sana angalia hata vile viti wanavyokalia vinazunguka halafu kuna mtu alinitonya eti mbele ya vile viti vya bunge letu kwa mbele ya wanapokaa hawa jamaa kuna kiyoyozi aisee kama ni kweli lazima watakua WANATAFAKARI SANA! A.K.A KULALA!
 
Kumbe ndio maana wamama na wadada walikuwa wakivaa mavitenge makubwa ili wakijambiwa wanawaziba harufu isifike kwao
lo good style
 
KIBUGUMO nakuunga mkono!!! Mapumziko ni haba sana!! Watu wako kwenye ULABU hadi saa za usikiu mkubwa; wakiondoka waondoke na mzigo wa chumbani (bed room baggage)..Kweli asubuhi utayasikia yanayojadiliwa??? Ndiyo maana wengi wao hata MAKABRASHA wanayowekewa kwenye pigeon holes (visanduku kwa kila Mh kwa ajili ya documents) huwa hazisomwi!! Toka lini mtu kama siyo JINIASI akaweza kusoma mambo muhimu na kuyaelewa wakati yu KILAJI CHAKARI??!! MUNGU SAIDIA Tz
 
Hivi unajua Wassira ndio amekaimu uwaziri mkuu pale bungeni??badala ya kusikiliza yy anauchapa!!
 
Anawakilisha yakuwa Muh. Waziri Mkuu anatakiwa awe hivyo yani usingizi kwa kwenda mbele, nalo bunge liishe tu maana kuna vitu vinakera ndani yake ukitupilia mbali na umeme wa mgao ndo kabisa.
 
Naomba anayeweza atuwekee picha ya wasira, kama alivyoonekana leo kwenye gazeti la mwananchi. Mi nimejaribu ku-upload lakini kuna matatizo kidogo ya ssystem. Mwenye uwezo tunaomba atuwekee.
 
kweli mkuu bunge letu lime kaa ki anasaaa sanaa ndomanaa wabunge wanakua na mda wa kulala na sio kusinziaaa!tatizo uma rufuuuu ndooo shida kutaka mambo makubwa!wakati tuna tegemea misaada!
 
Akishtuka usingizini, utasikia 'ndiyooooooo' bila ufahamu wa kilichojadiliwa,wananiudhi sana hawa
 
Back
Top Bottom