Wahenga ni akina nani hawa?

IsangulaKG,

Wahenga ni wazee wenye hekima na busara za juu sana ambao husema maneno ambayo hutumiwa na jamii kwa ajili ya kuadibu,kuadilisha na kuonya. Wahenga husema busara zao kabla ya kufa, hivyo wahenga ni wazee ambao huheshimika sana katika jamii kwa hekima na busara zao.
 
Sasa hizi posts za siku za hivi karibuni juu ya uhenga wa wahenga zimeanza vipi?

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
 
Bila shaka wahenga watakua babu zetu kweli kwa sababu hii misemo hata sie tumezaliwa tukaikuta ikitumika japo waloongea ni vigumu kuwajua because it was a long time ago.
 
wahenga ni wazee wa zamani ambao kiukweli walikuwa waongo waongo na wanapendwa kutukuzwa au kuonekana wana busara kumbuka haohao walisema polepole ndio mwendo haohao wakasema chelewa chelewa utakuta mwana si wako.

Yaani walitafuta sababu ya kuonekana wapo sahihi kwa kila jambo mfano wa methali hizo juu ukichelewa ukakosa kitu fulani atakwambia nilisema chelewachelewa utakuta mwana si wako na ukifanya harakaharaka ukapata tatizo atasema nilikuasa polepole ndio mwendo vivyohivyo kwa misemo mingine mfano
mvumilivu hula mbivu na ngojangoja yaumiza matumbo.
 
Wahenga wana misemo yao ambayo ina mafundisho makubwa sana mfano
Mficha uchi hazai
Nyani haoni kundule
Bibi alikuwa binti
Mchelea mwana ubeba jiwe..
Je hawa wahenga wali ishi zama zipi mpaka kujua haya yote?
 
Wahenga ni watu wenye hekima, busara na uwezo wa kufanya mamuzi sahihi.

Tatizo langu na mimi lipo hapo kwamba ni kama vile walikuwepo zamani tu na siku hizi hawapo. Wahenga walisema....kwa nini hatusemi wahenga wanasema?

Hehehe... Wahenga
 
wahenga ni wazee wa zamani ambao kiukweli walikuwa waongo waongo na wanapendwa kutukuzwa au kuonekana wana busara kumbuka haohao walisema polepole ndio mwendo haohao wakasema chelewa chelewa utakuta mwana si wako.

Yaani walitafuta sababu ya kuonekana wapo sahihi kwa kila jambo mfano wa methali hizo juu ukichelewa ukakosa kitu fulani atakwambia nilisema chelewachelewa utakuta mwana si wako na ukifanya harakaharaka ukapata tatizo atasema nilikuasa polepole ndio mwendo vivyohivyo kwa misemo mingine mfano
mvumilivu hula mbivu na ngojangoja yaumiza matumbo.
 
Wahenga ni wazee wenye hekima na busara katika jamii ambao maneno yao aghalabu yamekuwa yakitumiwa kama msingi wa kuonya, kuadibu na kuadilisha jamii.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom