Wahanga wa Mafuriko wafukuzwa kambini na RC

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,597
Kwa kadri ya matangazo ya TBC1 saa 2 usiku, RC wa Dar amewapa week moja wahanga wa mafuriko ambao ni wapangaji waliohifadhiwa kwenye makambi mbali mbali, waondoke wakatafute nyumba nyingine. Kwa maoni yake, serikali haina haja ya kuendelea kuwahifadhi watu hawa!

My take,

Kama wameathirika na mafuriko na kupoteza mali zao, watawezaje kupanga nyumba mpya???

Updates:

Wakazi mabondeni vichwa ngumu
na Datus Boniface
WAKATI baadhi ya wakazi wa mabondeni wakikaidi agizo la kuwataka kutorejea kwenye maeneo yao kwa muda, Serikali imeapa kuchukua hatua kali kwa atakayekaidi amri hiyo.Aidha, imesema inatarajia kulisafisha eneo la bonde la Jangwani na Msimbazi ili litumike kwa ajili ya kilimo.
Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick, wakati akizungumza na waandishi wa habari.Mkuu wa mkoa huyo alihoji utimamu wa wakazi hao wa mabondeni kupingana na serikali kwamba hawako tayari kuhama.
"Inaonekana wananchi hao hawana akili timamu kutokana na msimamo wao wa kung'ang'ania kukaa maeneo ya mabondeni ambayo ni hatarishi kwa maisha yao. Lakini pia watu hawa walishindwa kesi mahakamani waliyoifungua wakipinga kuhamishwa na serikali mwaka 2002, lakini bado wameng'ang'ania," alisema RC huyo.
Aliendelea kusema kuwa: "Maeneo ya bonde la Jangwani, Mto Msimbazi awali katika ramani ya uendelezaji mji wa Dar es Salaam, yalitengwa kama maeneo hatarishi, pia kwa mujibu wa sheria za ardhi zilipiga marufuku shughuli zozote kufanyika, lakini wananchi hawa walivamia na kukaidi amri ya kuwataka waondoke katika maeneo hayo.
"Lakini cha ajabu ni kwamba mwaka 2001, walifungua kesi Mahakama ya Ilala wakipinga hatua hiyo, hakimu aliyekuwa akisikiliza shauri ambaye kwa sasa ni marehemu, aliwataka waondoke kwani maeneo hayo ni hatarishi lakini wameshindwa kuondoka hadi juzi mafuriko yalivyowaondoa kwa nguvu," alisema.
Alisema: "Kama wana akili timamu wangetoa vitu vyao. Hawana akili timamu kutokana na kushindwa kuhama na badala yake wanataka wapewe misaada."
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa huyo, kutokana na wakazi hao kukaidi amri hiyo, serikali haitakuwa na urafiki katika hilo na wameamua kuweka doria kwa lengo la kumkamata mwananchi yeyote atakayerudi kuishi au kufanya shughuli katika maeneo hayo.
Mkuu wa mkoa huyo alisema, huduma za nishati ya umeme, maji, barabara na hospitali zimepigwa marufuku katika maeneo ya mabondeni. Alisema kama kigezo ni kumaliza kodi zao za mwaka, ni bora wakaenda kwenye vyombo vya sheria kudaiana. Alisema hakuna haja ya wakazi hao kung'ang'ania maeneo hatarishi wakati tayari kuna viwanja 700 vimetengwa kwa ajili yao.
"Wananchi wa mabondeni, waondoke kwa hiari yao, hakuna taasisi itakayoruhusiwa kufanya shughuli zake katika eneo hilo," alisema.
Kuhusu kugawiwa viwanja, alisema awali serikali ilitoa viwanja maeneo ya Yombo Dovya, lakini waliviuza na sasa itatoa vingine katika eneo la Mabwepande, Machimbo na Kunduchi.
Alisema viwanja hivyo vitagawiwa kwa mpangilio maalumu ili kuepuka uchakachuaji, lakini alionya kuwa si jukumu la serikali kuwajengea nyumba kwani itawapa ardhi bure.
Katika hatua nyingine, Serikali imewataka wananchi waliopanga nyumba maeneo ya mabondeni, waondoke mara moja katika makambi ya waathirika wa mafuriko.
Mkuu wa mkoa alisema serikali haitaendelea kuwabeba wananchi wa aina hiyo kwani wana uwezo wa kijitegemea.
Alisema wapangaji hao watafute nyumba za kupanga badala ya kuendelea kukaa katika makambi bila sababu za msingi.
Kwa upande mwingine serikali imetoa muda wa wiki mbili kwa wananchi wanaohifadhiwa katika makambi hayo kuondoka kabla ya shule hazijafunguliwa.

Mecky Sadick amesema, kama watashindwa kutii amri hiyo watahamishiwa eneo la Mabwepande, Kunduchi ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kuendelea na masomo yao.
Source: Tanzania Daima (
http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=31306)
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mdingi kachemka sana, watu wameathirika na mafuriko kwanza, umiliki wa nyumba lingefuata baadae na fidia ndio lingekuwa la mwisho.
Tulitegemea nhc na TBA wakifuatiwa na nssf, ppf, pspf na lapf wangetangulia huko kujenga majengo na waathirika waendelee kupanga.
Mapema sana huyu mdingi kawatosa wakati hata hesabu ya michango ya pole haijajulikana ni kiasi gani?
Wakapange wapi wakati nyumba ni tabu, watu wameuza sura sasa wananchi wanabwagwa kama ilivyo ada
 
Hayo ndio madhara ya vyeo vya kugawana, mtu anapewa kazi ya kuhudumia wananchi wakati hana mapenzi nao.

Mimi ningeshauri wagome kuondoka.Au mabomu ya machozi na virungu vya polisi vitahusika?
 
walimtaka rais handsome,sasa kazi

Hivi katika hii serikali, hakuna mtu anayeweza kutumia akili ya kawaida na kubaini kwamba ni mapema mno kuwambia watu ambao wamekumbwa na janga kubwa kiasi hicho maneno ambayo hayana hata chembe ya ubinadamu!!

Ila kwa jinsi watanzania walivyo wajinga, hawa hawa ndio utawakuta baada ya muda mfupi wametinga jezi za yellow na kijani na kunengua kwenye mipasho ya Komba na TOT!!
 
Mdingi kachemka sana, watu wameathirika na mafuriko kwanza, umiliki wa nyumba lingefuata baadae na fidia ndio lingekuwa la mwisho.
Tulitegemea nhc na TBA wakifuatiwa na nssf, ppf, pspf na lapf wangetangulia huko kujenga majengo na waathirika waendelee kupanga.
Mapema sana huyu mdingi kawatosa wakati hata hesabu ya michango ya pole haijajulikana ni kiasi gani?
Wakapange wapi wakati nyumba ni tabu, watu wameuza sura sasa wananchi wanabwagwa kama ilivyo ada

Nilimwangalia RC alivyokuwa anatoa hilo agizo hata sikummaliza....Too low!

Labda anadhani kwamba mgao waliopata kambini utatosha kununua vifaa vyao vya ndani vilivyoharibika na kubakiza change ya kupanga nyumba!!
 
Wananchi wanatengezewa zengwe ili ionekane wamejitakia na ni uzembe wao. Ukweli mvua ni kubwa kuliko kawaida toka 54 na hatukuambiwa mwaka huo kilitokea nini na serikali ilifanya nini.
 
RC wa Dar es Salaam ni bomu bomu hana mbele wala nyuma yeye anafyatuka tuu ,Kuna kipindi alibanwa na waandishi wa habari alipowadharilisha wakifuatilia matatizo ya wananchi wakati wa mabomu ya Mbagala
Mameya wa Ilala na Kinondoni wako Likizo kabisa hata mwenykiti wa halmashauri ya Jiji muuza shirika la UDA naye kaingia mitini wananchi sasa wanakebehiwa hivi RC anajua maana ya kupoteza kila kitu,Rafiki yake Jakaya Kikwete kapitishwa na helkopta kaenda mchikichini katoa lugha pale kisha kapanda Tanzania One kurudi Serengeti tutamuona tarehe 31 akitanunua tanua mikono kutosomesha ha ha nchi ya ajabu
 
RC wa Dar es Salaam ni bomu bomu hana mbele wala nyuma yeye anafyatuka tuu ,Kuna kipindi alibanwa na waandishi wa habari alipowadharilisha wakifuatilia matatizo ya wananchi wakati wa mabomu ya Mbagala
Mameya wa Ilala na Kinondoni wako Likizo kabisa hata mwenykiti wa halmashauri ya Jiji muuza shirika la UDA naye kaingia mitini wananchi sasa wanakebehiwa hivi RC anajua maana ya kupoteza kila kitu,Rafiki yake Jakaya Kikwete kapitishwa na helkopta kaenda mchikichini katoa lugha pale kisha kapanda Tanzania One kurudi Serengeti tutamuona tarehe 31 akitanunua tanua mikono kutosomesha ha ha nchi ya ajabu

Kweli kabisa,

Katika hili janga la mafuriko, serikali imeonekana wazi wazi kijivua lawama na kuwabebesha wahanga mzigo wa lawama. Labda ndio maana sasa hata elements za utu zimetoweka kabisa!
 
Hayo ndio madhara ya vyeo vya kugawana, mtu anapewa kazi ya kuhudumia wananchi wakati hana mapenzi nao.

Mimi ningeshauri wagome kuondoka.Au mabomu ya machozi na virungu vya polisi vitahusika?

Nimeipenda sana hii!
 
Tumaweza kuwahifadhi wakimbizi wa Rwanda na Burundi kwa zaidi ya miaka 10, lakini sii raia wananchi wenyewe waathirika!... Na sababu tu kwamba kwa wakimbizi huletewa misaada ya fedha kutoa mfuko wa kimataifa na watu huvuta zao pembeni..

Leo nitawapa neno moja mwaka Mpya kwa Watanzania wote.. Jamani eeeh tuache mawazo ya - KIMACHINGA.... Akili hii ndio inayoturudisha nyuma toka uongozi hadi wananchi wenyewe WATU na UONGOZI BORA). Sisi sii wabunifu, hatuna vision bali tunaendesha uchumi, siasa na hata imani zetu za kimaisha kimachinga kwa malengo ya kuchumia tumbo na kila siku ina mwanzo mpya - Tubadilike!
 
Watanzania wenzangu, hii ndiyo CCM tuliyoichagua wenyewe! Baada ya uchaguzi kwisha haikumbuki tena wanyonge. Wamesahau jinsi walivyokuwa wakitupigia magaoti kutuomba kura. Sasa wametugeuka na hawataki kutuona hasa wakati huu tukiwa kwenye shida. Wakati ule wa uchaguzi tulifikiria kuwa ni wenzetu ambao wangetujali, tukacheka nao huku tukiwakebehi wapinzani na hatimaye tukawapa kura zetu, walahi hatukujua kuwa tulikuwa tukicheka na nyani! Nchi inauzwa, viongozi wanajilimbikizia mali, wezi wanatukuzwa na kutunzwa, wenye kashfa, mfano genge la akina Luhanjo, Jairo na wengine bado wanakula kuku ikulu kana kwamba hakuna kuna kibaya walichofanya kwa taifa. Hata uteuzi wa mabalozi umekwenda kwa uswahiba, wale tuliowakataa kwenye kura zetu kwa sababu hawafai, bado wanaendelea kupiganiwa na mkulu. Kinyume chacke ni wanyonge kukandamizwa, wanafunzi wananyimwa mikopo, tukilalamika tunapigwa na polisi, mahakamani wanyonge ndo anayechukuwa hukumu za mvua, watoto wa wanyonge mashuleni hawana madawati, waliomaliza vyuo vikuu hawana elimu, waliopatwa na majanga kama haya ya mafuriko wanafukuzwa kambini n.k.Sasa wanyonge tuache kulalamika, tujipange upya 2015 watakapokuja tena kutupiga magoti kuomba kura zetu. Kuna mnyonge gani atakayecheka na nyani tena 2015? Mimi hapana.
 
Hivi huyu RC kayasema haya akiwa na akili zake timamu; au alikuwa amelewa??Watu bado wanaomboleza; yeye analeta lugha ya kuwatusi, badala ya kuwafariji.Kwa nchi za wenzetu hii ilikuwa tosha kufukuzwa kazi mara moja.
 
Siombei maafa, lakini majanga mbalimbazi yanapotokea ndani ya nchi yetu huacha funzo fukani kwa wahanga pamoja na viongozi wanaotegemewa kupanga mikakati ya kuwasaidia. Serikali yenyewe imefilisika kwa sasa unategemea nini?
Mdingi kachemka sana, watu wameathirika na mafuriko kwanza, umiliki wa nyumba lingefuata baadae na fidia ndio lingekuwa la mwisho.
Tulitegemea nhc na TBA wakifuatiwa na nssf, ppf, pspf na lapf wangetangulia huko kujenga majengo na waathirika waendelee kupanga.
Mapema sana huyu mdingi kawatosa wakati hata hesabu ya michango ya pole haijajulikana ni kiasi gani?
Wakapange wapi wakati nyumba ni tabu, watu wameuza sura sasa wananchi wanabwagwa kama ilivyo ada
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom