Wahanga hawa wako wengi-Mama, mtoto wafia mapokezi ya hospitali kwa kukataliwa huduma

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Mama, mtoto wafia mapokezi ya hospitali kwa kukataliwa huduma
* Ni baada wauguzi kukataa kumhudumia mjamzito

Na Jackson Odoyo


MAMA mjamzito, Teddy Kimoso amefia katika mapokezi ya Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam wakati akijifungua, baada ya wahudumu waliokuwa zamu kugoma kumhudumia kwa vile hakuwa na vifaa vya huduma hiyo.


Mama huyo amekufa pamoja na mtoto wake ambaye alikuwa tayari anaanza kutoka.


Tukio hilo lilitokea juzi usiku baada ya mjazito huo kufika hospitalini hapo akiwa na ndugu zake, huku hali yake ikiwa mbaya na wahudumu waliokuwa zamu wakagoma kumpatia huduma muhimu kwa wakati unaotakiwa.


Akizungumza na mwandishi wa habari hii hospitalini hapo jana, mmoja wa ndugu za marehemu aliyejitambulisha kwa jina moja la Kimoso, alisema alipigiwa simu usiku wa kuamkia jana kwamba, wauguzi wamekataa kumsaidia mgonjwa huyo mpaka wapewe fedha za kununulia vifaa vya kujifungulia.


Alisema baada ya kupokea taarifa hiyo, alianza kuwasiliana na baadhi ya ndugu zake ili waangalie jinsi ya kumsaidia mgonjwa huyo na kwamba, wakati wote huo hali yake ilizidi kubadilika.


Alisema kutokana na muda, aliweza kuwasiliana na ndugu waliokuwa karibu na hatimaye wakafanikiwa kufika hospitali hapo na kununua vifaa hivyo.


Alitaja vifaa hivyo kuwa ni pamoja na 'glovu' (mipira ya kuvaa mikononi), pamba, sindano, dawa za maumivu na maji ya uchungu.


Alisema baada ya vifaa hivyo kupatikana, walimchukua na kumpeleka katika wodi ya Karume, lakini wahudumu hao waliendelea kuwa wazito kumpatia mgonjwa wao huduma kwa wakati unaohitajika.


Alifafanua hata walipoamua kwenda kwa hiyari yao, walikuwa wakitoa maneno ya kejeli kwamba anawapigia kelele wakati anafahamu utaratibu wa hospitali ulivyo.


Alisema wakati huo mtoto alikuwa ameshaanza kutoka, huku hali ya mgonjwa ikizidi kuwa mbaya.


''Siwezi kuzungumza mengi ndungu mwandishi, kwani nina huzuni sana kutokana na hali hii kwani siku hizi watu wa hali ya chini tunakufa kwa sababu ya kukosa fedha, kwani kama ndugu yangu angekuwa na fedha pengine asingefariki dunia,'' alisema Kimoso na kuongeza:


''Mimi si msemaji wa familia, msemaji ameshaondoka na tunakwenda kukusanyika ili tujue cha kufanya, tumeshangazwa na tukio hili na hiki ni kizazi cha tatu cha marehemu. Na kuhusu mazishi, tunategemea kumsafirisha leo kwenda Morogoro,'' alisema.


Ndugu mwingine aliyezungumzia suala hilo ni Yekonia Gabrieli alisema kuwa wanatarajia kumsafirisha marehemu kwenda Morogoro kwa mazishi na baada ya mazishi wataanza kufuatilia kwa undani wa kifo cha ndugu yao.


Mazingira ya kifo cha marehemu huyo, yaliwashangaza wangonjwa wengi waliokuwa hospitalini hapo, huku wakisema kuwa mama huyo alihangaika kwa muda mrefu bila kupatiwa huduma.


Mama mmoja aliyekuwa katika wodi ya Karume, alisema marehemu alipelekwa wodini hapo akiwa hajitambui huku mtoto akiwa ameanza kutoka, lakini wauguzi hao hawakuonyesha jitihada za kumsaidia.


Akizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina lake gazetini, mgonjwa huyo alisema yeye alipelekwa hospitalini hapo tangu juzi asubuhi na akajifungua usiku na kubainisha kwamba, katika kipindi alichokaa hospitalini hapo, amejionea uzembe mwingi unaofanywa na wahudumu wa hospitali hiyo.


Alisema mbali na kifo cha marehemu Kimoso, kuna akinamama wawili walifariki dunia hospitalini hapo wakati wa kujifungua kutokana na uzembe wa wauguzi.


''Marehemu aliletwa hapa wodini akiwa na hali mbaya na ninadhani alishafariki kwani alipoletwa akalazwa kitandani kisha akazungushiwa pazia la kijani na ndani ya pazia hilo kulikuwa na wauguzi watatu huku mmoja akiingia na kutoka. Na baada ya hapo hawakuelewa kilichoendelea,'' alisema na kuongeza:


''Ilipofika asubuhi tukaona anatolewa na kuingizwa kwenye mkokoteni. Ndipo tukagundua kuwa amefariki dunia kwani hali ya uzembe katika hospitali hii inatisha''.


Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Asha Mahita alikiri kuwepo kwa tukio hilo na kusema kuwa hafahamu kama kweli mgonjwa huyo alifariki kutokana na uzembe wa wauguzi.


Mahita alisema hawezi kupinga wala kukubaliana na taarifa hiyo kwa sababu hospitali hiyo ina wahudumu zaidi ya 400 na kati yao, wapo waadilifu na wasio waadilifu.


Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Beatrice Byarugaba alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alisema hana taarifa yoyote juu ya tukio hilo na kwamba atafuatilia ili kufahamu undani wake.


Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Jiji, Judith Kahama alisema hana taarifa japo kutwa nzima alikuwa akiwasiliana na hospitali hiyo pamoja na manispaa na kuahidi kuwa atafuatilia kwa undani suala hilo.


Tuma maoni kwa Mhariri




Habari katika picha na Matangazo
 
Hao wafanyakazi hawana tofauti na viongozi wa ccm wanaonunua ndege na rada mbovu kwa bei za kuruka na kuuza nchi kwa bei za karanga huku wakiacha watz wakila nyasi (kama alivyosema Mramba).

Jamani yaani inatia huruma na hasira ... yaani acha tu.
 
Wakubwa nimempoteza kichanga wangu kwa uzembe wa wauguzi, news kama hii inagusa sana moyo wangu... ninaomba kwa Mungu afanye mabadiliko makubwa ktk vichwa vya wauguzi na waganga

Waziri wa Afya proudly anataja orodha ya watoto na kina mama wanaokufa kwa matatizo ya uzazi halafu hafanyo juhudi zozote kuokoa hali hii.

AFYA NI HAKI YETU YA KIKATIBA LAZIMA TUIDAI
 
Nimeshudia uzembe wa makusudi sana Muhimbili . nilihangaika sana na mtu sikuwa namjua lakini ukimuona mtoto na Mama mtoto ana miaka 28 hajawahi kufika Dar alikuja kwa matibabu anasema aliuza hata sufuria ya kupikia akatoa hongo Muhimbili na huku wanajua mtoto wa umri ule hakustahili OP ambayo walikuwa wanampangia .Baada ya mtaalamu mmoja kukataa x-ray mama akaanza kufukuzwa Muhimbili .Nilipofika PCCB nilikuta na kugundua kitu cha ajabu kidogo .Sitasema kwa sasa .

Nimeshuhudia uozo hapo Mwananyamala usiku mmoja nimeuguliwa ilikiuwa balaa ya ajabu sana lakini baadhi yao kutokana na maswali yangu walishituka na kuyoa huduma wengine wakaachwa wanaumia hapo na hata nikashangaa .

Musoma nimeshuhudia mtu anakufa na risasi za ndege mwilini baada ya kuvamiwa na majambazi .Nililiingilia lakini nilipotoka kila mpango ukaisha nafika Dar next day napiga naambiwa Lunyungu ulipo wapa mgongo wakasema tutakoma ma mgonjwa kafa .

Hizi ndiyo hosp za Mwakyusa na aina ya wakubwa wanasema hawaamini kama madai ni ya ukweli .

Nina msururu wa mifano na hosp hizi ni mbaya sana afadhali kutibiwa kwa mganga wa kienyeji atajali hata kama hana uwezo wa kutibu wala kuongeza damu kuliko kwenda hosp za serikali na hasa ukiwa mmwaga jasho mpaka wa kuonekana ni shida zaidi .
 
Hawa wahudumu kweli wamekula kiapo cha Florence Nightingale au ndiyo tunaokoteza watu wanaotaka kuganga njaa na kuwaita wahudumu?

Kama habari imeripotiwa vizuri, mtu anayefahamu miiko ya uhudumu hawezi kufanya hivi.Hata huku magharibi wanakoijua hela juu chini na kila mtu anapotakiwa kuwa na bima ya afya watu wanaelewa kuwa kwa mambo ya emergency (or will some argue that this is not?) huwa mtu anatibiwa kwanza halafu mengine yanaangaliwa baadaye.

Hospitali haitakiwi kukosa vifaa kwa cases kama hizi.Pia hata kama hospitali imekosa vifaa kama wakunga wa wahenga waliweza kuzalisha bila vifaa hawa maaluni kilichowashinda ni nini?

Hizi kazi zina wenyewe na sio kila mtu kujitwika kazi kwa sababu ya kuganga njaa tu, kazi zinataka watu wenye kujitoa hizi.Ndiyo maana mimi nikasema siwezi kuwa daktari.

Inasikitisha sana. Sasa tunakuwa mabepari kuliko hata hao mabepari wenyewe.Hatuna hata simile.Tunajimaliza wenyewe, by default.
 
Aaaaahhh Ndivyo Tulivyo bana....
Na kwa nini wale kiapo cha mzungu Florence Nightinglae....? Hakuna Mwafrika wanayeweza kula kiapo chake? Kwa mfano, Mwafrika wa Kike....wanaweza kula kiapo chake....
 
Aaaaahhh Ndivyo Tulivyo bana....
Na kwa nini wale kiapo cha mzungu Florence Nightinglae....? Hakuna Mwafrika wanayeweza kula kiapo chake? Kwa mfano, Mwafrika wa Kike....wanaweza kula kiapo chake....

Afadhali wale kiapo cha Florence maana kinaeleweka vizuri na so far kimetumika vizuri. Changu hawatakiweza na watakimbia profession ... lol
 
tupitishe petition Mwakyusa must Go maana sijui anafanya nini pale... madaktari wanaacha kutibu wanakimbilia researches na kutimkia nje je kweli hii serikali inajali maisha ya watu wake kweli??
nina hasira siyo kidogo
 
Hi mentality ya "fulani must go" haitatufikisha popote.

Tuna systemic problem, tunahitaji a systemic solution.

CCM must go is more like it.Mwakyusa as a person may not be the problem and may actually be better than many a possible replacements, but what do you do when the entire system is plagued? You start an overhaul of the entire system, you do not change nuts and bolts.
 
Hawa wahudumu kweli wamekula kiapo cha Florence Nightingale au ndiyo tunaokoteza watu wanaotaka kuganga njaa na kuwaita wahudumu?

Kama habari imeripotiwa vizuri, mtu anayefahamu miiko ya uhudumu hawezi kufanya hivi.Hata huku magharibi wanakoijua hela juu chini na kila mtu anapotakiwa kuwa na bima ya afya watu wanaelewa kuwa kwa mambo ya emergency (or will some argue that this is not?) huwa mtu anatibiwa kwanza halafu mengine yanaangaliwa baadaye.

Hospitali haitakiwi kukosa vifaa kwa cases kama hizi.Pia hata kama hospitali imekosa vifaa kama wakunga wa wahenga waliweza kuzalisha bila vifaa hawa maaluni kilichowashinda ni nini?

Hizi kazi zina wenyewe na sio kila mtu kujitwika kazi kwa sababu ya kuganga njaa tu, kazi zinataka watu wenye kujitoa hizi.Ndiyo maana mimi nikasema siwezi kuwa daktari.

Inasikitisha sana. Sasa tunakuwa mabepari kuliko hata hao mabepari wenyewe.Hatuna hata simile.Tunajimaliza wenyewe, by default.

msikimbilie kusema hizi kazi ni wito wito tu,hivi kwenye pesa wapi pameandikwa wito??kila kazi ni wito mazee..
wewe unafikiri mtu atajitoaje kimasomaso kama kapesa anakopata ni ka duchu hakawezi kumtoa hata kwa wiki 2?Mbunge anapiga porojo bungeni anaondoka na lundo la fwedha,iweje watu muhimu kama hawa serikali haiwajali?Kama mpiga deki wa TRL analipwa mshahara mkubwa kuliko daktari aliyesota more than 5 years kula shule ngumu na katika mazingira magumu,huu wito utatoka wapi hapa?
Pale muhimbili kuna mpaka ma surgeon hawawezi hata ku afford ka mark 2 wanakwenda kazini kwa daladala,sasa hebu jiulize huyu mtu atakuwa na morali ya kazi kweli wakati anamuona jirani yake labba yuko tigo tu ana sukuma mashine.
msikimbilie kulaumu tu ndugu zangu
 
msikimbilie kusema hizi kazi ni wito wito tu,hivi kwenye pesa wapi pameandikwa wito??kila kazi ni wito mazee..
wewe unafikiri mtu atajitoaje kimasomaso kama kapesa anakopata ni ka duchu hakawezi kumtoa hata kwa wiki 2?Mbunge anapiga porojo bungeni anaondoka na lundo la fwedha,iweje watu muhimu kama hawa serikali haiwajali?Kama mpiga deki wa TRL analipwa mshahara mkubwa kuliko daktari aliyesota more than 5 years kula shule ngumu na katika mazingira magumu,huu wito utatoka wapi hapa?
Pale muhimbili kuna mpaka ma surgeon hawawezi bado wanakwenda kazi na daladala,sasa hebu jiulize huyu mtu atakuwa na morali ya kazi kweli wakati anamuona jirani yake labba yuko tigo tu ana sukuma mashine.
msikimbilie kulaumu tu ndugu zangu

Ukitaka fedha ukaenda kwenye unesi Tanzania umepotea njia, tafuta ajira nyingine.

Regardless of the socio-economic situation, wewe unatetea kwa wauguzi kugomea ukunga mpaka watu wanakufa? Huu ndio utu wetu?
 
Ukitaka fedha ukaenda kwenye unesi Tanzania umepotea njia, tafuta ajira nyingine.

Regardless of the socio-economic situation, wewe unatetea kwa wauguzi kugomea ukunga mpaka watu wanakufa? Huu ndio utu wetu?

sasa kama unasema ukitaka umasikini tanzania uende unesi wewe unafikiri kuna binadamu gani anayependa umasikini?kwahiyo nani atakuwa nesi sasa tanzania?mimi sitetei hili.Kwanza habari yenyewe bado haijathibitishwa.Kuna mgonjwa amehojiwa hapo anasema inawezekana huyu mama wakati analetwa alikuwa amekwishafariki tayari.
Hoja yangu ni kwamba tusiangalie pale tulipoanguka bali tuangalie pale tulipojikwaa.Iambie serikali yako badala ya kununua mashangingi,kuilipa richmond 152m kila siku,kupoteza mamilioni kwenda kung'oa meno ulaya na marekani nk itumie hizo pesa kuboresha mazingira ya kazi ya hawa watu,iwalipe pesa ya kutosha hawa watu halafu uone kama kutakuwa na uzembe wowote na virushwa vya kijingajinga.
 
sasa kama unasema ukitaka umasikini tanzania uende unesi wewe unafikiri kuna binadamu gani anayependa umasikini?kwahiyo nani atakuwa nesi sasa tanzania?mimi sitetei hili.Kwanza habari yenyewe bado haijathibitishwa.Kuna mgonjwa amehojiwa hapo anasema inawezekana huyu mama wakati analetwa alikuwa amekwishafariki tayari.
Hoja yangu ni kwamba tusiangalie pale tulipoanguka bali tuangalie pale tulipojikwaa.Iambie serikali yako badala ya kununua mashangingi,kuilipa richmond 152m kila siku,kupoteza mamilioni kwenda kung'oa meno ulaya na marekani nk itumie hizo pesa kuboresha mazingira mazuri ya kazi ya hawa watu,iwalipe pesa ya kutosha hawa watu halafu uone kama kutakuwa na uzembe wowote na virushwa vya kijingajinga.

The real protest would be for people to not go into nursing because of bad conditions and wages, then ungeona hali ingebadilika.

Lakini as long as ume sign up kwa kazi ya wito kama hii huna haki ya kusema nagoma huku watu wanakufa.It is against their very own oath.
 
Kwani kuna Waafrika gani?

Kuna hawa hapo chini, kila nchi iko tofauti na katika kila nchi kuna matabaka tofauti, sasa huwezi kuwa lump together wote, tena katika kila issue kwamba "Waafrika Ndivyo Walivyo"

http://www.who.int/countries/mus/en/

Total population: 1,252,000
Gross national income per capita (PPP international $): 13,510
Life expectancy at birth m/f (years): 69/76
Healthy life expectancy at birth m/f (years, 2003): 60/65
Probability of dying under five (per 1 000 live births): 15
Probability of dying between 15 and 60 years m/f (per 1 000 population): 212/108
Total expenditure on health per capita (Intl $, 2005): 544
Total expenditure on health as % of GDP (2005): 4.3

na hawa

http://www.who.int/countries/zwe/en/

Total population: 13,228,000
Gross national income per capita (PPP international $): not available
Life expectancy at birth m/f (years): 44/43
Healthy life expectancy at birth m/f (years, 2003): 34/33
Probability of dying under five (per 1 000 live births): 85
Probability of dying between 15 and 60 years m/f (per 1 000 population): 755/755
Total expenditure on health per capita (Intl $, 2005): 146
Total expenditure on health as % of GDP (2005): 8.1

Na hawa

http://www.who.int/countries/caf/en/

Total population: 4,265,000
Gross national income per capita (PPP international $): 1,280
Life expectancy at birth m/f (years): 48/48
Healthy life expectancy at birth m/f (years, 2003): 37/38
Probability of dying under five (per 1 000 live births): 174
Probability of dying between 15 and 60 years m/f (per 1 000 population): 471/466
Total expenditure on health per capita (Intl $, 2005): 54
Total expenditure on health as % of GDP (2005): 4.0

Na hawa

http://www.who.int/countries/egy/en/

Total population: 74,166,000
Gross national income per capita (PPP international $): 4,690
Life expectancy at birth m/f (years): 66/70
Healthy life expectancy at birth m/f (years, 2003): 58/60
Probability of dying under five (per 1 000 live births): 35
Probability of dying between 15 and 60 years m/f (per 1 000 population): 229/142
Total expenditure on health per capita (Intl $, 2005): 279
Total expenditure on health as % of GDP (2005): 6.1
 
The real protest would be for people to not go into nursing because of bad conditions and wages, then ungeona hali ingebadilika.

Lakini as long as ume sign up kwa kazi ya wito kama hii huna haki ya kusema nagoma huku watu wanakufa.It is against their very own oath.

mzee hakuna oath inayosema uende unesi ukawe masikini.
halafu kwanini uone manesi tu ndiyo wenye wito?kwani ni wao tu ndiyo wanakula kiapo?mbona hata Rais na mawaziri wanakula kiapo?hivi nani mwenye wito mzito kati ya nesi na waziri let say wa nishati.Nani muuaji kati ya nesi na huyu anayesaini mkataba hotelini unaoliingizia taifa hasara ya mamilioni ya pesa na kusababisha huduma za afya kuwa mbovu na watu kufa kila siku kwa magonjwa yanayozuilika kabisa kama malaria,wakati yeye akiwa na jipu tu anakwenda kulipasulia marekani?
try to figure out bro,swala siyo kuwa discourage wanafunzi wasiende unesi,swala ni kudeal na mamlaka zinazohusika ili kuliondoa hili tatizo.
 
sasa kama unasema ukitaka umasikini tanzania uende unesi wewe unafikiri kuna binadamu gani anayependa umasikini?kwahiyo nani atakuwa nesi sasa tanzania?mimi sitetei hili.Kwanza habari yenyewe bado haijathibitishwa.Kuna mgonjwa amehojiwa hapo anasema inawezekana huyu mama wakati analetwa alikuwa amekwishafariki tayari.
Hoja yangu ni kwamba tusiangalie pale tulipoanguka bali tuangalie pale tulipojikwaa.Iambie serikali yako badala ya kununua mashangingi,kuilipa richmond 152m kila siku,kupoteza mamilioni kwenda kung'oa meno ulaya na marekani nk itumie hizo pesa kuboresha mazingira ya kazi ya hawa watu,iwalipe pesa ya kutosha hawa watu halafu uone kama kutakuwa na uzembe wowote na virushwa vya kijingajinga.


Umesoma na kuelewa habari ya hawa ndugu na mashahidi wa wodini ama unakurupuka unaweka pesa mbele na maisha ya mtu yanapotea ? Let's say kama angalipewa hongo ya 50,000 ingalimsaidia hadi lini ? Nadhani kuna haja ya kuwamata hawa walio husika na mauaji haya na kuwapa kesi ya mauaji na si kusema malipo .Hayo yaje baadaye na namna ya kudai malipo zaidi wanajua
NI wao wenyewe wanalia na CCM kila siku kwamba ni Chama poa leo inakuwaje Chama poa serikali haiwajali tena wanaanza kuua watu ?
 
Umesoma na kuelewa habari ya hawa ndugu na mashahidi wa wodini ama unakurupuka unaweka pesa mbele na maisha ya mtu yanapotea ? Let's say kama angalipewa hongo ya 50,000 ingalimsaidia hadi lini ? Nadhani kuna haja ya kuwamata hawa walio husika na mauaji haya na kuwapa kesi ya mauaji na si kusema malipo .Hayo yaje baadaye na namna ya kudai malipo zaidi wanajua
NI wao wenyewe wanalia na CCM kila siku kwamba ni Chama poa leo inakuwaje Chama poa serikali haiwajali tena wanaanza kuua watu ?

Lunyungu,mwalimu wangu aliyenifundisha kusoma hakupata tabu sana na mimi!
Wewe utaishia kupiga kelele tu wapewe kesi ya mauaji lakini kwa taarifa yako tu ni kwamba hakuna atakayehukumiwa kwa mauaji hapo,kama unabisha subiri uone.
Hayo ya ccm unaweza ku refer kwa post zangu nilizomjibu pundit hivyo sina haya ya kurudia tena kuonyesha mtazamo wangu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom