Wahamiaji kutoka Ethiopia na Somalia kufungwa na kuwekwa mahabusu ni msongamano na gharama kwa serikali

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Tangu mwanzo niliwahi sema na ninarudia kusema kwa kuishauri serikali, wahamiaji haramu hasa kutoka nchi mbalimbali na wengine hawa kutoka Ethiopia na Somalia wamejaa katika Magereza yetu.

Nilipokuwa Mahabusu Gereza la Iringa 2018 April, kulikuwepo na Wahamiaji wengi kutoka Somalia, wengine kama wafungwa wengine kama mahabusu .

Wengi walikamatwa wakiwa wanapita Tanzania ili waende nchi zingine na wengine walikamatwa wakiingia kinyemela Tanzania , ila mimi nimekuwa na fikra tofauti katika hili siku zote.

Sijawahi ona sababu ya kuwafungulia kesi na kuwaweka Gerezani kama mahabusu sababu hawa hawana ndugu hivyo Serikali kupitia DPP inapowafungulia kesi hawawezi kupewa dhamana hivyo wanakuwa kama mahabusu na kuwekwa Getezani.

Watakula bure na kuongeza gharama na msongamano katika magereza yetu , niliyo wakuta mahabusu Iringa walikuwa na miezi 8 kesi yao haijaisha , hivyo wanakula bure hadi kesi yao itakapoamuliwa na wakiamuliwa kufungwa watafungwa labda miaka 2 au 3 hivyo kuongeza gharama na msongamano Magereza.

Kuwafungulia mashtaka na kuwafunga haijawahi kusaidia hawa wahamiaji kusita kuingia nchini kinyume na sheria kwa kuogopa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.

Ushauri wangu , hawa Raia hasa kutoka somalia na Ethiopia ni wengi sana katika Magereza yetu wengi wakiwa mahabusu na wengine wafungwa na makosa yao ni aina moja .

Ushauri kwa serikali @tanzaniagovernment ,@wizaramnn , @katibanasheria_
na Mh. @samia_suluhu_hassan ili kukabiliana na msongamano na kupunguza gharama katika Magereza yetu .

1.Kesi za hawa wahamiaji hasa wa Somalia na Ethiopi ambao ni wengi na sasa ni Mahabusu zifutwe tuu ili warejeshwe kwao .

2.Kuna haja ya msamaha wa Rais ili wahamiaji wote ambao ni hao waethiopia ,somalia hata wengine wafutiwe kesi ili warejeshwe kwao kupitia Balozi zao .

3.Njia zingine za ziada zitumike kukabiliana na hawa wahamiaji na kuzuia kuingia nchini , ili kupunguza tatizo hilo .

Ila njia ya kuwafungulia mashtaka na kuwaweka ndani sioni kama ni dawa zaidi naona huongeza gharama na msongamano katika Magereza yetu.

Ahsante.
IMG_20220401_080902_984.jpg
 
Kumbe huwa wanafungwa?
Sasa watetezi wa haki za binadamu wako wapi?
Mbona warundi walipelekwa Camp?
Sijawahi kuwwza hili ila najua huwa wanawakamata na kuwaibia hela zao na chochote walichonacho
Hilo huwa wanasema wekimbizi wakiachiwa huku nje na wanasema ni Africa yote wananyanyashwa na kuteswa na kuporwa

Hawa iliyakiwa wanaotaka kuishi kwetu wapewe permit halafu uraia
Ila kufungwa ni uonezi sana
Kwani ni wahalifu? Haki zao hakuna wa kuwasemea
 
Katika mambo ya hovyo na ajabu Ni Sheria hii ya uhamiaji, AU imeshindwa ku harmonise mifumo. Mataifa Yana Uhuru zaidi miaka 50!

Ajira, njaa, fursa maisha! Hata ukifika boda nchi za Africa mashariki EAC maisha yanabadilika gafla, garama simu nk
 
Hawa tungewafungia macho tu wangi weo kama sio wote wanaokamatwa wanakuwa wanapita njia tu kuna baadhi niliona walikamatwa mpakani Nakonde wakiwa wanataka kuingia Zambia. Yaani wametoka kote huko sijui namanga hadi wanakaribia kutoka Tanzania wanakamatwa
Nakumbua Mexico walivyowaachia caravan iliyouwa inatoka Honduras wakiwa wanakwenda USA bila vibali.
Ila kama tunawazuia tutumie busara na utaratibu wa IMO warudishwe kwao ulipo kuwafunga
 
Wapo tu hata korogwe wapo..
Yule mama yao wakiethiopia kipindi Cha awamu ya tano si alikujaga na nikaski moja ya ombi lake ni hilo.
 
Ata mimi ili jambo huwa linanitafakarisha kwa nini tusiandae utaratibu wa wao kukaa kwenye kambi wanaposhikwa huku tukiandaa utaratibu wa kuwarejesha kwao.

Au kama inakua ngumu bora watumike kama nguvu kazi. Washiriki kwenye kilimo cha umoja watuzalishie kama taifa.
 
Badala uzungumzie Watanzania wenzako wasio na hatia huko Magereza unajadili Wageni wenye hatia Kwa Mujibu wa sheria; badala ufanye utafiti Watanzania wangapi wapo magereza Afrika Kusini Kwa makosa kama haya unajadili Wageni wenye hatia,

Nenda kawakatie rufaa kama unaamini Awana hatia. Hoja hapo siyo idadi hoja ni kuangalia sheria zilizopo zinafuatwa? Fanya utafiti kuhusu sababu za wao kukaa Magereza then shauri njia Gani zitumike ila kuja na hoja kwamba Nchi iache kuchukua hatua Kwa wageni huku ukishangilia wafungwa wa kesi ya kuiba kuku Watanzania nikukosa uelewa

Tuanze kuwatetea Watanzania ambao wakiachiwa wanakwenda makwao Kwa gharama zao tukimaliza tuwajadili qageni wanaohitaji kurudishwa makwao Kwa Kodi za wananchi
 
Badala uzungumzie Watanzania wenzako wasio na hatia huko Magereza unajadili Wageni wenye hatia Kwa Mujibu wa sheria; badala ufanye utafiti Watanzania wangapi wapo magereza Afrika Kusini Kwa makosa kama haya unajadili Wageni wenye hatia,

Nenda kawakatie rufaa kama unaamini Awana hatia. Hoja hapo siyo idadi hoja ni kuangalia sheria zilizopo zinafuatwa? Fanya utafiti kuhusu sababu za wao kukaa Magereza then shauri njia Gani zitumike ila kuja na hoja kwamba Nchi iache kuchukua hatua Kwa wageni huku ukishangilia wafungwa wa kesi ya kuiba kuku Watanzania nikukosa uelewa

Tuanze kuwatetea Watanzania ambao wakiachiwa wanakwenda makwao Kwa gharama zao tukimaliza tuwajadili qageni wanaohitaji kurudishwa makwao Kwa Kodi za wananchi
Haya Mkuu ni maoni na wewe toa yako ya Watanzania hao wasio na hatia tutachangia pia
 
Badala uzungumzie Watanzania wenzako wasio na hatia huko Magereza unajadili Wageni wenye hatia Kwa Mujibu wa sheria; badala ufanye utafiti Watanzania wangapi wapo magereza Afrika Kusini Kwa makosa kama haya unajadili Wageni wenye hatia,

Nenda kawakatie rufaa kama unaamini Awana hatia. Hoja hapo siyo idadi hoja ni kuangalia sheria zilizopo zinafuatwa? Fanya utafiti kuhusu sababu za wao kukaa Magereza then shauri njia Gani zitumike ila kuja na hoja kwamba Nchi iache kuchukua hatua Kwa wageni huku ukishangilia wafungwa wa kesi ya kuiba kuku Watanzania nikukosa uelewa

Tuanze kuwatetea Watanzania ambao wakiachiwa wanakwenda makwao Kwa gharama zao tukimaliza tuwajadili qageni wanaohitaji kurudishwa makwao Kwa Kodi za wananchi
Yaani hapa Nondo ameshindwa kutambua wapo magereza kwa mujibu wa sheria.
Yawezekana huyu kijana wa ACT hana exposure na mipaka ya nchi zingine ndio maana anabwabwaja hapa.
 
Back
Top Bottom