Wahadhiri Wanne Wafukuzwa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania!

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Imeandikwa na Gloria Tesha.

CHUO Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), kimewafukuza kazi wahadhiri wanne, mfanyakazi mmoja, na kimefuta matokeo ya wanafunzi 20 baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu katika matokeo ya mitihani.

Wanafunzi wengine 71 wapo hatarini kufutiwa matokeo endapo mpaka kesho hawatajitokeza kwenye kamati maalum iliyoundwa kuchunguza kadhia hiyo ya udanganyifu wa matokeo iliyoibuka miezi takribani minne iliyopita na gazeti hili kuwa la kwanza kuitangaza kwa umma.

Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Tolly Mbwette aliwaeleza waandishi wa habari jana Dar es Salaam, kuwa uamuzi huo umefikiwa katika kikao cha Baraza la Seneti kilichokaa Ijumaa iliyopita na kikao cha jana cha Baraza la Chuo, kilichohitimisha suala hilo lililochunguzwa chini ya mfumo wa Student Academic Recording System (SARS).

Aliwataja wahadhiri waliofukuzwa na nafasi zao katika mabano ni Saimon Kitila (Mhadhiri Msaidizi, Kitivo cha Uongozi na Biashara); Jovin Mwehozi (Mhadhiri Msaidizi, Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii); Juma Kanuwa (Mhadhiri Msaidizi, Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii) na Jamal Mwasha (Mkufunzi Msaidizi, Kitivo cha Sheria).

Mtumishi mwingine aliyefukuzwa kazi ni Richard Ngwalida, ambaye ni mtaalamu wa kompyuta ambaye amedaiwa alipokea hongo na kumsaidia mwanafunzi kujaribu kughushi matokeo.

Hata hivyo, Profesa Mbwette hakuwa tayari kueleza ni hongo ya kiasi gani na hatua zilizochukuliwa kwa mtoa hongo.

Kuhusu wahadhiri hao, Mbwette alisema, "Uchunguzi uliofanywa na kamati maalumu iliyoundwa na chuo kuchunguza suala hilo, ulibaini kuwa walihusika kughushi matokeo ya wanafunzi kwa kuyaingiza katika vitivo mbalimbali

bila idhini na huku ni kughushi na ni kosa, Baraza la Chuo halikupendezwa na suala hili na hatupo tayari kuvumilia haya."

Akifafanua kuhusu wanafunzi, Profesa Mbwette alisema uchunguzi wa chuo ulioanza Oktoba mwaka jana, uliwezesha kuandikiwa barua wanafunzi 278 kutoka ofisi ya Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma ikiwataka wafike katika kamati maalumu ya Baraza la Seneti kuhojiwa kuhusu tuhuma hizo, ambapo 207 waliitikia mwito.

"Kati ya hao 207 waliofika, mpaka Januari 8, mwaka huu, wanafunzi 120 walishajieleza na kuonekana hawana makosa yoyote, 31 vitivo vyao vimeagizwa vihakikishe takwimu za matokeo yao kwa upya, 36 takwimu tuna mashaka nazo na vitivo vyao vinachunguza ambapo Baraza la Seneti la Februari mwaka huu, litatoa uamuzi dhidi yao, lakini 20 tumewafutia matokeo na 71 tumewapa muda, wasipotokea mpaka keshokutwa (kesho) tunajua wamejifuta wenyewe," alisema Makamu Mkuu wa OUT.

Katika hatua nyingine, wanafunzi 50 ambao majina yao hayakuwemo katika orodha ya wahitimu mwaka jana kutokana na uzembe wa chuo, watashiriki mahafali ya mwaka huu na kwa mujibu wa Profesa Mbwette, matokeo yao watapewa wakati wowote kuanzia sasa ili wayatumie katika kazi na ajira zao.

Oktoba mwaka jana, uongozi wa OUT ulibainisha kuhusu kuwepo kwa wanafunzi wanaotuhumiwa kufanya udanganyifu katika matokeo ya mitihani, ambapo gazeti hili pia lilibaini kuhusu wahadhiri hao wanne kuhusika pia katika sakata hilo.

Pamoja na mambo mengine, Profesa Mbwette amevishauri vyuo vingine kufanya uchunguzi kama huo ili kulinda hadhi ya elimu nchini.

SOURCE: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=5205
 
Wapelekwe kortini kwa kudhalilisha taaluma na ubunifu. Hizi chunguzi zisiishie hapo.
 
huyo juma kanuwa namfahamu personally, anaonekana kijana mzuri, mtulivu na anayejiheshimu. nimesikitika sana kwa utou wa maadili aliofanya.
 
Aliwataja wahadhiri waliofukuzwa na nafasi zao katika mabano ni Saimon Kitila (Mhadhiri Msaidizi, Kitivo cha Uongozi na Biashara); Jovin Mwehozi (Mhadhiri Msaidizi, Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii); Juma Kanuwa (Mhadhiri Msaidizi, Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii) na Jamal Mwasha (Mkufunzi Msaidizi, Kitivo cha Sheria).

Huyu dogo wa Kitivo cha Sheria namfahamu, sikujua kama naye ana vijimambo!
 
Lakini system nzima ya chuo nafikiri ni ya kulaumiwa. Unajua unapokuwa unaweka fedha zako nyingi katika sehemu ambazo zinaonekana unaleta ushawishi wa kuziiba hata kama mtu hakuwa na nia ya kufanya wizi. Kwa upande wa OUT systems ziko loose mno, Just imagine wanafunzi hawaonyeshi vitambulisho vyao wakati wanaingia kwenye mitihani. Assignments nasikia kuna watu waliunda timu za kusolve assignments za wanafunzi wa OUT, wewe ni kupeleka mshiko wako tu na maswali, unajiondokea na kurudi baada ya maswali kufanywa na timu hiyo unayachukua na kwenda kukusanya. Kwa upande wa kuingiza matokeo kwenye kompyuta ni kwamba system haikuwa tight enough kiasi kwamba mtu anaweza kuhonga ili atengenezewe matokeo yawe "mazuri." Sasa naona asilaumiwe mwizi tu, bali hata aliyemfanya mtu kuiba naye alaumiwe!
 
Open chuo chote kinabidi kisafishwe,kuanzia ma TA paka VC.kinamapungufu mengi sana.....hususan watu kufanyiwa assignments na UEz.
 
Lakini system nzima ya chuo nafikiri ni ya kulaumiwa. Unajua unapokuwa unaweka fedha zako nyingi katika sehemu ambazo zinaonekana unaleta ushawishi wa kuziiba hata kama mtu hakuwa na nia ya kufanya wizi. Kwa upande wa OUT systems ziko loose mno, Just imagine wanafunzi hawaonyeshi vitambulisho vyao wakati wanaingia kwenye mitihani. Assignments nasikia kuna watu waliunda timu za kusolve assignments za wanafunzi wa OUT, wewe ni kupeleka mshiko wako tu na maswali, unajiondokea na kurudi baada ya maswali kufanywa na timu hiyo unayachukua na kwenda kukusanya. Kwa upande wa kuingiza matokeo kwenye kompyuta ni kwamba system haikuwa tight enough kiasi kwamba mtu anaweza kuhonga ili atengenezewe matokeo yawe "mazuri." Sasa naona asilaumiwe mwizi tu, bali hata aliyemfanya mtu kuiba naye alaumiwe!

1. Kuingia kufanya mitihani wanacheki vitambulisho (walau nilishaona ikifanyika Temeke Regional Centre), teketi ya mtihani (au test) na picha ya mhusika.

2. Kuhusu 'assignments' ni kweli. Kuna wanafunzi (hasa wale wenye hela) hawataki usumbufu na wanawashawishi wengine ili 'assignments' zao zifanywe na 'teacher' na 'teachers' wenye njaa hawakatai.

3. Ni kweli 'system' nzima na 'functining' ya OUT haijakaa sawa. Bado kuna 'loopholes' nyingi sana! Nashangaa kwa nini Prof Mbwette na wakuu wengine wasiende kujifunza kutoka vyuo vingine vyenye programu za 'Distance Learning' kama London University na kuona wao wanafanyaje.

4. OPEN inatakiwa ifanyiwe marekebisho mengi sana na pia staff wajifunze customer care na siyo kufanya kazi kama wamelazimishwa (kwa kununa na kutotaka kuwaelekeza wanafunzi/wateja vizuri)!
 
1. Kuingia kufanya mitihani wanacheki vitambulisho (walau nilishaona ikifanyika Temeke Regional Centre), teketi ya mtihani (au test) na picha ya mhusika.

2. Kuhusu 'assignments' ni kweli. Kuna wanafunzi (hasa wale wenye hela) hawataki usumbufu na wanawashawishi wengine ili 'assignments' zao zifanywe na 'teacher' na 'teachers' wenye njaa hawakatai.

3. Ni kweli 'system' nzima na 'functining' ya OUT haijakaa sawa. Bado kuna 'loopholes' nyingi sana! Nashangaa kwa nini Prof Mbwette na wakuu wengine wasiende kujifunza kutoka vyuo vingine vyenye programu za 'Distance Learning' kama London University na kuona wao wanafanyaje.

4. OPEN inatakiwa ifanyiwe marekebisho mengi sana na pia staff wajifunze customer care na siyo kufanya kazi kama wamelazimishwa (kwa kununa na kutotaka kuwaelekeza wanafunzi/wateja vizuri)!

1. Huko kuonyesha vitambulisho na picha sio kila sehemu na kama kuna sehemu wanaonyesha vitambulisho lwakati wanaingia kwenye papwe abda hiyo system imeanza hivi karibuni, hasa baada ya wanafunzi kuanza kucheat.
2. Kuhusu customer care, kwa kweli hawa watu customer care yao ni very poor, utafikiri wamelazimishwa kufanya kazi, wamenuna utafikiri kuna mashindano ya kununa!
 
Chuo chenyewe kinaitwa "Open Uni" unategemea nini kama mambo sio "Open"??
 
Chuo chenyewe kinaitwa "Open Uni" unategemea nini kama mambo sio "Open"??

hahaaa wewe ngoshwe!!!

pesa msema kweli!!!! unanunua madesa vichwa mpaka na grades!!!

uko wapi ubora wa elimu sasa?????????? na hii na imani si open uni tu hata vyuo vingine itakuwepo.

wat a dirty game!!!!!!!!!
 

2. Kuhusu 'assignments' ni kweli. Kuna wanafunzi (hasa wale wenye hela) hawataki usumbufu na wanawashawishi wengine ili 'assignments' zao zifanywe na 'teacher' na 'teachers' wenye njaa hawakatai.

3. Ni kweli 'system' nzima na 'functining' ya OUT haijakaa sawa. Bado kuna 'loopholes' nyingi sana! Nashangaa kwa nini Prof Mbwette na wakuu wengine wasiende kujifunza kutoka vyuo vingine vyenye programu za 'Distance Learning' kama London University na kuona wao wanafanyaje.

4. OPEN inatakiwa ifanyiwe marekebisho mengi sana na pia staff wajifunze customer care na siyo kufanya kazi kama wamelazimishwa (kwa kununa na kutotaka kuwaelekeza wanafunzi/wateja vizuri)!


Hii ni serious issue. waneweza kujifunza toka Sweden pia kuna vyou vinatoa programme kama hizo lakini wana control system kuona kuwa mtu anastahili kupata hicho cheti. mfano BTH, LTU (Luleå).
Na la kufanyiwa assignment nishalisikia hata mlimani especially kwa programme za MBA. Watu wanafanyiwa hadi thesis. Kazi ipo kwa Tanzania.
 
Hii ni serious issue. waneweza kujifunza toka Sweden pia kuna vyou vinatoa programme kama hizo lakini wana control system kuona kuwa mtu anastahili kupata hicho cheti. mfano BTH, LTU (Luleå).
Na la kufanyiwa assignment nishalisikia hata mlimani especially kwa programme za MBA. Watu wanafanyiwa hadi thesis. Kazi ipo kwa Tanzania.

Nchi hii kuna eneo ambalo kuna control system ambayo ni tight?
 
Ni aibu sanaaa! mwaka jana zilipatikana scholarship nyingi za kwenda kusoma Ubelgiji lakini baada ya kyfatilia ikaonekana asilimia kubwa ya walipata walipeleka vyeti vya kufoji!! wakatupiliwa mbali na sasa wanafanya hali ya kupata hata kwa wanaostahili kuwa ngumu zaidi, Tunaelekea kubaya saaaana.
 
Ni aibu sanaaa! mwaka jana zilipatikana scholarship nyingi za kwenda kusoma Ubelgiji lakini baada ya kyfatilia ikaonekana asilimia kubwa ya walipata walipeleka vyeti vya kufoji!! wakatupiliwa mbali na sasa wanafanya hali ya kupata hata kwa wanaostahili kuwa ngumu zaidi, Tunaelekea kubaya saaaana.

Whaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaat?
 
hahaaa wewe ngoshwe!!!

pesa msema kweli!!!! unanunua madesa vichwa mpaka na grades!!!

uko wapi ubora wa elimu sasa?????????? na hii na imani si open uni tu hata vyuo vingine itakuwepo.

wat a dirty game!!!!!!!!!

Mzee sio utani,

Haya mambo "huria" na "Ubinafsi" tulipaswa kwanza tujifunze kwa wale waliotutaka tufanye. Wenzetu walioendelea wana mfumo mzuri wa kudhibiti ujinga kama huu.

Hivi unategemea nini kama Mhadhiri wa chuo kikuu huria anaishi maisha huria, mhadhiri kasoma kiujanja, ujanja tu kwa kuiba mitihani na kudesa!.

Huyo hawezi kuacha tabia yake. Vigezo vinavyotumika katika vyuo vyetu kupata wahadhiri ni "just awe" na "Upper second" nzuri au "1st Class" Hilo sio shida kwa sasa kwenye mfumo wa elimu huria na ya kununua. Hii ni tofauti na walimu wa kawaida wanavyuo vya ualimu, wanajifunza pia maadili ya kazi na jinsi ya kufundisha.

Hizi digrii za "chupi" na "rushwa" siku hizi zimeua kabsaaa taaluma.

Nimewahi kufanya kazi na jamaa ana "first class" ya chuo kimoja binafsi (...) tuliajiriwa siku moja, masikini jamaa mkichwa alikuwa ni "o" kabsaaa, anaangalizia mpaka kuandika barua ya kiofisi (mimi na "ka lower 2nd" kangu tu). Jaama alikuwa hawezi kujieleza kwa kingereza wala kiswahili, kujibu hoja kwenye jalada atakutafuta kokote ulipo hata kama umesafiri atasubiri mpaka urudi, huyo jamaa sasa ni mhadhiri katika chuo fulani! kudadadeki, unategemea nini hapo??

Zamani nilijua ni product ya vyuo binafsi tu vinavyofanya biashara, hivyo havisiti kutoa "first class" za kumwaga ili kuvutia wateja, kumbe sasa hata vile vya umma vimeingia kwenye wimbi la udanganyifu mkubwa!.Nilipata kusikia tatizo hilo la kugawana digrii "kufanya biashara ya mabadilishano ya "digrii na sehemu za siri" au "digrii na fedha" katika chuo kimoja cha umma kule Morogoro....Baada ya kuwauliza waliosoma hapo, walithibitisha kuwa ni jambo la kawaida tu kwa sababu wahadhiri wengi ni vijana wanafundisha "part time" na wananatafuta maisha "chap chap" .......
 
Back
Top Bottom