Wahadhiri wa Vyuo Vikuu na mishahara ya Wabunge na Wakurugenzi Mashirika ya Umma

Nakuelewa sana tu. Hata hivyo sometimes ni lazima ukweli usemwe ili nchi yetu ipige hatua kwa ajili ya future ya nchi yetu, watoto wetu na vizazi vyetu vijavyo.

Vyuo vyetu vikuu ni sehemu ya ujinga mwingi uliomo kwenye nchi yetu wa kutumia pesa za umma bila tija yoyote ya maana inayoonekana kwenye jamii. Ungekuwa umo ndani ya system ya vyuo vikuu vya umma vya Tanzania ungeshangaa kuona jinsi wakuu wa vyuo wanavyoprioritize maslahi yao binafsi kuliko agenda halisi za uwepo wa vyuo vikuu.

  • Utashangaa kuona magari ya viongozi wa vyuo yakiharibika kesho yake linaenda kutengenezwa fasta au kununuliwa jipya kabisa (pesa hiyo huwa haikosi), lakini vifaa vya maabara vikiharibika hiyo ndio ntolee.
  • Utashangaa kuona vyuo vikuu vyenye idara za sayansi (kama biolojia, chemia na fizikia) havina maabara functional yenye vifaa hata basic katika kufanyia tafiti, lakini vyuo hivyo havikosi bajeti ya kununua magari mapya.
  • Utashangaa kuona vyuo vinakaa vikao mbali mbali vinavyolipa mapesa mapesa lakini wakati huo huo havina bajeti ya kufanya tafiti.
  • Na mifano mingi kama hiyo.

Vyuo vya umma vipo kwa ajili ya kufanya tafiti, kufundisha na kuleta innovations za maana kwa faida ya nchi, na matumizi ya pesa za serikali huko vyuoni yanapaswa kuakisi hilo.

Ni kweli mishahara ya wahadhiri wa vyuo vya umma ni miduchu lakini pia kazi zao za msingi hawaonekani kama wanazifanya kwa ufanisi. Wapo wapo tu yaani.
Wangekuwa wanalipwa vzr wasingebuni vikai vya ajabu ajabu ili wapate posho.
 
Nchi zilizoendelea maprofesa wanajikita katika taaluma zao kwa manufaa ya Taifa, ila nchi masikini maprofesa wanakimbilia kwenye siasa, imekaaje?
 
Ushauri wako mzuri Sana lkn wanaopaswa kulifanyia kazi wazo lako ndiyo hao hao akina msukuma na kibajaji ambao kila kukicha wanaiponda elimu ndani ya bunge. Unategemea mwitikio chanya ktk hili??
 
Wangekuwa wanalipwa vzr wasingebuni vikai vya ajabu ajabu ili wapate posho.
Hiyo haiwezi kuwa excuse! Unaweza kushangaa chuo kikuu kisicho cha umma kama SAUT (wajenge majengo, walipe mishahara, walipe gharama za uendeshaji wa chuo za kila siku, umeme, maji, usafi, n.k) kupitia ada za wanafunzi na mambo yao yanakwenda.

Linganisha Chuo cha umma ambapo majengo yote serikali,,gharama za uendeshaji serikali, wanafunzi wengi wanaenda vyuo vya umma maana yake ada ya kutosha, magari serikali, mishahara ya walimu na wafanyakazi waendeshaji serikali.

Lakini linapokuja suala la impact hakuna tofauti kati ya chuo cha private kama Saut chenye resources chache na vyuo vya umma vyenye support ya serikali asilimia 100.

Huo si upuuzi tu.
 
Yaani utakuta mtu hana hata ubongo wowote, lkn kwa sababu anajua kubwabwaja na figisu, basi tayari anakuws mwana siasa, baadaye mbunge. Huu ni ujinga ulioje!!
Hii ni nchi ya figisu, fitina na kujipendekeza ili mradi tu mkono uende kinywani
 
Habari wana bodi, nimekuwa nikisoma baadhi ya articles zinazo ongelea mchango wa vyuo vikuu marekani katika uchumi wa taifa hilo especially kutengeneza innovators "silicon valley".

Kwa kiasi kikubwa maendeleo ya taifa la marekani yamechangiwa sana na innovations zinazofanywa na taasisi zake za elimu ya juu kama "think tank" ya nchi, kuanzia sera za uchumi, sera za mambo ya nje, etc.

Ukiangalia Taifa letu, wahadhiri wa vyuo vikuu ambao ndio wazalishaji wa wataalamu mbalimbali wamekuwa wakilipwa pesa kidogo sana ukilinganisha na wakurugenzi wa mashirika ya Umma au wabunge( ambao hawana mchango wa maana kwenye taifa hili uki compare na mchango unaotolewa na wahadhiri wa vyuo vikuu. Jiulize kibajaji au musukuma anawezaje kulipwa mshahara na marupurupu kuliko Prof au Dr, wa chuo kikuu?

Mimi ningemuomba Rais Samia waangalie hawa watu kama kweli tunataka hili taifa lisonge mbele. Licha ya kuongezewa mishahara serikali ipeleke pesa za kufanya tafiti mbalimbali na maamuzi ya wanasiasa yazingatie recommendations za wataalamu wetu.

Mtu ana PhD analipwa mshahara wa mil 3 au 4 na hapo bado makato kweli unategemea atakuwa na morale ya kufundisha? Au ndio atakuwa busy kufanya kazi zake za nje? Serikali inatakiwa kuona wapi inaweza kuwekeza pesa na zikawa na tija kwa taifa hili.
LOGIC
 
Hii ya kusingizia PhD za kupika ni uzushi, ingekuwa rahisi kupika PhD kama unavyopika mlenda kila mtu angekuwa nayo, kifupi nchi hii haithamini wasomi na wataalamu ndo maana haiendi popote. Ukishaua morale ya wasomi hakuna watakachofanya zaidi ya kutumia vichwa vyao kuendelea kufuga nywele, hakuna anayekubali kuhangaisha kichwa chake pale ambapo hathaminiwi.......
Yani inashangaza sana mtu ana PhD anapata mshahara hawezi hata ku afford a comfortable life. Wengi wana stress sana vyuoni. Wanafanyakazi siku ziende wapate wanachopa.

Serikali ufanye uchunguzi tu, wengi wana stress na depression.
 
Moja ya sifa kubwa ya nchi zinazoendelea (maskini) ni kutojali elimu.

Zitamlipa mamilioni jamaa fulani anayeenda kusema kuwa daraja la pale kata ya mjimwema ni la muhimu (wakati mkuu wa wilaya, mkoa, madiwani wanajua na wanaweza fikisha habari) halafu litamlipa vijisenti jamaa anayekwenda kutoa maarifa jinsi ya kulitengeneza.

Kwa mwendo huu tutajengewa na kutengenezewa sana vitu vyetu na wazungu na wachina.
 
Back
Top Bottom