Wahadhiri vilaza huzalisha wasomi vilaza

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,776
18,189
Tunapojadili kuhusu kushuka kwa elimu yetu na kupungua kwa ubora wa wahitimu tusisahau kuangazia vinu vinavyozalisha wasomi hao. Juzi nilimtembelea rafiki yangu ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) tukabahatika kubadilishana mawazo ya hapa na pale kuhusu elimu inayotolewa chuoni siku hizi.

Moja ya sababu aliyonieleza inayopelekea kushuka kiwango cha elimu yetu ni wahadhili vilaza ambao huzalisha wasomi vilaza. Kwa kusisitiza hili jambo, ilinilazimu kufanya maarifa ya ziada ili kujiridhisha na maelezo yake. Ndipo nilipobahatika kupata paper iliyowahi kutungwa kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka wa pili katika Idara ya Sayansi ya Chakula na Tekinolojia kama inavyoonekana hapo chini.

upload_2016-12-5_16-57-10.jpeg


upload_2016-12-5_16-57-38.jpeg


Nilipoona paper hiyo nilishikwa na butwaa. Nilidhani huenda ilitungwa kwa ajili ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na sio wa mwaka wa pili. Kwa mitihani ya kipuuzi kama hii tutarajie kuzalisha wasomi wa aina gani? Nilichogundua ni kuwa wahadhiri wengi wana uwezo mdogo sana. Ndio maana wanatunga mitihani hafifu kwa sababu hawana uwezo wa kutunga mitihani “akili kubwa”.

TUJADILIANE
Ni nani alaumiwa hasa kwa uuaji huu wa elimu ya taifa? Je ni serikali, wahadhiri, wanafunzi, sayansi na teknolojia, wazazi au jamii nzima ya watanzania?

Serikali ilaumiwe?
Kwa mujibu wa utafiti (usio rasmi) uliofanyika hivi karibuni, serikali ina mkono wake katika kudorora kwa elimu ya nchi hii kwa kuingiza siasa kwenye elimu, kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.

Kivipi? Ili kujijenga kisiasa serikali iliamua kwa makusudi kabisa kurahisisha elimu yetu kwa maana ya kupunguza viwango vya ufaulu (au kutanua goli) ili wanafunzi wengi zaidi wapate nafasi za kuingia sekondari. Mitihani ilirahisishwa mno kwa lengo la kuwafanya wanafunzi wafaulu kwa wingi ili kujaza shule za kata (sema makaburi ya kuzikia elimu) zilizoanzishwa kisiasa na serikali.

Lengo hasa lilikuwa ni kujaza shule za sekondari zilizokuwa zimefunguliwa kwenye kata, hata kama hazina walimu. Ndipo wakaibuka wanafunzi wanaofaulu kwenda sekondari ilhali hawajui kusoma na kuandika. Msumari wa kwanza wa sanduku la kuzikia elimu yetu uligongewa hapa.

Wanafunzi vilaza wakafaulu kwenda sekondari na huko sekondari pia mitihani ikarahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu kwenda vyuo vikuu. Matokeo yake, wanafunzi vilaza wakaingia vyuo vikuu.

Sababu nyingine inayopelekea serikali kulaumiwa katika hii kadhia ni uzembe wake wa kuwahudumia wanafunzi kwa maana ya kuwapa mahitaji yao ya msingi (boom) kwa wakati hivyo kupelekea wanafunzi hao kuishi katika mazingira ya njaa na kukata tamaa.

Na kwa sababu hiyo, wahadhiri wao huwaonea huruma na kuwatungia mitihani rahisi kwa kuwa hawasomi vizuri kwa sababu ya njaa kali waliyo nayo.

Baadhi ya wahadhiri wanalinda ajira zao au nao ni vilaza?
Ili kulinda ajira zao, wahadhiri nao wakaamua kutunga mitihani rahisi ili kupunguza idadi ya wanafunzi wanaoshindwa (discontinue) kuendelea na masomo. Jambo hili tunaweza kulitazama kwa kutumia dhana mbili: Mosi, wahadhiri huamua kutunga mitihani rahisi kwa sababu ya kulinda ajira zao.

Kwamba kama wakiamua kutunga mitihani migumu, na kwa kuwa wanafunzi ni vilaza, wanaweza kufeli darasa zima hivyo mhadhiri kukosa kazi ya kufanya. Kwa hiyo, ili kuhalalisha uwepo wake, inambidi mhadhiri atunge mitihani rahisi kuwawezesha wanafunzi wengi kufaulu.

Dhana ya pili ni kwamba wahadhiri wengi inawezekana kabisa wakawa vilaza, hasa ukizingatia namna wanavyopatikana, hivyo hutunga mitihani rahisi kulingana na uwezo wao mdogo.

Sayansi na teknolojia imechangia?
Kufuatia kukua kwa sayansi na teknolojia asilimia kubwa ya wanafunzi wanamiliki na kutumia vifaa vya intanet (kompiuta, simu, laptops, ipads, nk), hivyo hutumia muda mwingi kuchat na kutafuta wapenzi kwenye mitandao badala ya kujikita kwenye masomo.

NINI KIFANYIKE?
Serikali ichukue maamuzi magumu ya kufufua elimu kuanzia ngazi ya chekechea hadi chuo kikuu. Utaratibu wa kupata wahadhiri uangaliwe upya. Aidha, serikali ikaze uzi kwenye mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati ili kuwachuja vizuri wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu.

Tusiangalie zaidi takwimu za kisiasa. Ule utunzi wa mitihani migumu kama ilivyokuwa zamani urejewe. Hata ikibidi wanafunzi 100 ndio wafaulu kwenda chuo kikuu na iwe hivyo. Kusiwepo na uchakachuaji wa matokeo ili kuongeza kiwango cha ufaulu kisiasa.

MJADALA UMEFUNGULIWA….
Tujadiliane kwa ufasaha kuhusu hili tatizo la ukilaza vyuoni mpaka tupate jibu. Shambulieni hoja badala ya kumshambulia mtoa mada. Hata kama kuna mtu ataona hii hoja inamgusa moja kwa moja, awe mvumilivu…asitukane au kuchangia kwa jazba.

Sote tunajenga nyumba moja, tusigombee fito kamwe. Mods naomba mnilinde maana nina hakika kuna watu wanaoniona mbaya kwa kuwa wanadhani kitumbua chao nimekitia mchanga. Aidha kuna wanaopenda mteremko ambao hawependi kuona wanakaziwa kwa namna yoyote ile.


Nawasilisha.
 
ELIMU YETU NI BOMU LILILOANZA KUTULIPUA WATANZANIA WA KARNE HII.

KUNA CHUO KIPO KULEE SEHEM SEHEM KINATOA SHAHADA YA SHERIA ,KINA MALEKCHALA WATATU TU, TENA WENYEW NA TUTOLIO ASISTANTI.
NA HAWAINGII DARASANI.
NA WATU WANAGRADUETI TU KILA MWAKA.HAHAAAA
KUNA TATIZO KWANI
 
Huo mtihani una tatizo gani??
Mkuu mtihani wa levo ya chuo kikuu unakuwa wa kitoto kama huu? Maswali ya filling in the blanks? You can't be serious. Ndio maana kumbe vilaza wameongezeka siku hizi.
 
We measure Cognitive, Affective, and Psychomotor Domain. Je, Magwiji wa MaProf. Wanaowakalilisha nadharia vijana wetu bila uhalisia kuwaonyesha wanawasaidia nini??????!!!!!!
 
swala la elimu inabidi liwekewe mikakati ya muda mrefu tatizo kila waziri wa sasa anayepewa nafasi anafikiri anaweza kubadilisha mambo kwa wakati mmoja.Tumekuwa na mikakati mingi ya kuboresha elimu lakini wakati tukiandaa mikakati hiyo tunasahau kuboresha maslahi ya walimu matokeo yake watu wenye uwezo wamekuwa wakiikimbia hiyo fani na waliobaki wamekosa morali ya kufundisha. Msingi wa elimu unatakiwa ujengwe kuanzia ngazi ya chini kabisa ila tumekimbili kuongeza idadi ya vyuo vikuu ikiwemo kubadilisha vyuo vya ualimu kama duce na mkwawa bila kuzingatia mahitaji halisi ya nchi.Pia tumeua vyuo na shule za ufundi.Mwisho elimu na siasa visichanganywe.
 
Inamaana hawa viongozi wetu wanaojigamba kuwa wamesoma udsm na bado wanatoa maamuzi ya kijinga jinga, je tuamini wahadhiri wao ni vilaza
 
1. Sasa si tumpe huyu mama support
2. Vyuo viweke elimu mbele siyo biashara
3. Tafiti zaidi unawezakuta maprof wanachangiwa mtonyo
4.Katiba bwana ili serikali yo yote inakuja madarakani wafuate criteria siyo kila kipindi kukarabati gari kwa style kwa matakwa ndiyo waendeshe wakimaliza safari yao wanalibwaga hivyo hadi wangine waje wanalitengeneza kufuatana mahitaji yao hivyo.
 
Tunapojadili kuhusu kushuka kwa elimu yetu na kupungua kwa ubora wa wahitimu tusisahau kuangazia vinu vinavyozalisha wasomi hao. Juzi nilimtembelea rafiki yangu ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) tukabahatika kubadilishana mawazo ya hapa na pale kuhusu elimu inayotolewa chuoni siku hizi.

Moja ya sababu aliyonieleza inayopelekea kushuka kiwango cha elimu yetu ni wahadhili vilaza ambao huzalisha wanafunzi vilaza. Kwa kusisitiza hili jambo, ilinilazimu kufanya maarifa ya ziada ili kujiridhisha na maelezo yake. Ndipo nilipobahatika kupata paper iliyowahi kutungwa kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka wa pili katika Kitivo Cha Sayansi ya Chakula na Technolojia kama inavyoonekana hapo chini.

View attachment 442959

View attachment 442960

Nilipoona paper hiyo nilishikwa na butwaa. Nilidhani huenda ilitungwa kwa ajili ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na sio wa mwaka wa pili. Kwa mitihani ya kipuuzi kama hii tutarajie kuzalisha wasomi wa aina gani? Nilichogundua ni kuwa wahadhiri wengi wana uwezo mdogo sana. Ndio maana wanatunga mitihani hafifu kwa sababu hawana uwezo wa kutunga mitihani “akili kubwa”.

TUJADILIANE
Ni nani alaumiwa hasa kwa uuaji huu wa elimu ya taifa? Je ni serikali, wahadhiri, wanafunzi, sayansi na teknolojia, wazazi au jamii nzima ya watanzania?

Serikali ilaumiwe?
Kwa mujibu wa utafiti (usio rasmi) uliofanyika hivi karibuni, serikali ina mkono wake katika kudorora kwa elimu ya nchi hii kwa kuingiza siasa kwenye elimu, kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.

Kivipi? Ili kujijenga kisiasa serikali iliamua kwa makusudi kabisa kurahisisha elimu yetu kwa maana ya kupunguza viwango vya ufaulu (au kutanua goli) ili wanafunzi wengi zaidi wapate nafasi za kuingia sekondari. Mitihani ilirahisishwa mno kwa lengo la kuwafanya wanafunzi wafauulu kwa wingi ili kujaza shule za kata (sema makaburi ya kuzikia elimu) zilizoanzishwa kisiasa na serikali.

Lengo hasa lilikuwa ni kujaza shule za sekondari zilizokuwa zimefunguliwa kwenye kata, hata kama hazina walimu. Ndipo wakaibuka wanafunzi wanaofaulu kwenda sekondari ilhali hawajui kusoma na kuandika. Msumari wa kwanza wa sanduku la kuzikia elimu yetu uligongewa hapa.

Wanafunzi vilaza wakafaulu kwenda sekondari na huko sekondari pia mitihani ikarahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu kwenda vyuo vikuu. Matokeo yake, wanafunzi vilaza wakaingia vyuo vikuu.

Sababu nyingine inayopelekea serikali kulaumiwa katika hii kadhia ni uzembe wake wa kuwahudumia wanafunzi kwa maana ya kuwapa mahitaji yao ya msingi (boom) kwa wakati hivyo kupelekea wanafunzi hao kuishi katika mazingira ya njaa na kukata tamaa.

Na kwa sababu hiyo, wahadhiri wao huwaonea huruma na kuwatungia mitihani rahisi kwa kuwa hawasomi vizuri kwa sababu ya njaa kali waliyo nayo.

Baadhi ya wahadhiri wanalinda ajira zao au nao ni vilaza?
Ili kulinda ajira zao, wahadhiri nao wakaamua kutunga mitihani rahisi ili kupunguza idadi ya wanafunzi wanaoshindwa (discontinue) kuendelea na masomo. Jambo hili tunaweza kulitazama kwa kutumia dhana mbili: Mosi, wahadhiri huamua kutunga mitihani rahisi kwa sababu ya kulinda ajira zao.

Kwamba kama wakiamua kutunga mitihani migumu, na kwa kuwa wanafunzi ni vilaza, wanaweza kufeli darasa zima hivyo mhadhiri kukosa kazi ya kufanya. Kwa hiyo, ili kuhalalisha uwepo wake, inambidi mhadhiri atunge mitihani rahisi kuwawezesha wanafunzi wengi kufaulu.

Dhana ya pili ni kwamba wahadhiri wengi inawezekana kabisa wakawa vilaza, hasa ukizingatia namna wanavyopatikana, hivyo hutunga mitihani rahisi kulingana na uwezo wao mdogo.

Sayansi na teknolojia imechangia?
Kufuatia kukua kwa sayansi na teknolojia asilimia kubwa ya wanafunzi wanamiliki na kutumia vifaa vya intanet (kompiuta, simu, laptops, ipads, nk), hivyo hutumia muda mwingi kuchat na kutafuta wapenzi kwenye mitandao badala ya kujikita kwenye masomo.

NINI KIFANYIKE?
Serikali ichukue maamuzi magumu ya kufufua elimu kuanzia ngazi ya chekechea hadi chuo kikuu. Utaratibu wa kupata wahadhiri uangaliwe upya. Aidha, serikali ikaze uzi kwenye mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati ili kuwachuja vizuri wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu.

Tusiangalie zaidi takwimu za kisiasa. Ule utunzi wa mitihani migumu kama ilivyokuwa zamani urejewe. Hata ikibidi wanafunzi 100 ndio wafaulu kwenda chuo kikuu na iwe hivyo. Kusiwepo na uchakachuaji wa matokeo ili kuongeza kiwango cha ufaulu kisiasa.

MJADALA UMEFUNGULIWA….
Tujadiliane kwa ufasaha kuhusu hili tatizo la ukilaza vyuoni mpaka tupate jibu. Shambulieni hoja badala ya kumshambulia mtoa mada. Hata kama kuna mtu ataona hii hoja inamgusa moja kwa moja, awe mvumilivu…asitukane au kuchangia kwa jazba.

Sote tunajenga nyumba moja, tusigombee fito kamwe. Mods naomba mnilinde maana nina hakika kuna watu wanaoniona mbaya kwa kuwa wanadhani kitumbua chao nimekitia mchanga. Aidha kuna wanaopenda mteremko ambao hawependi kuona wanakaziwa kwa namna yoyote ile.


Nawasilisha.
Kuna tatizo katika uendeshaji vyuo vyetu vya Serikali. Na hili linachangiwa na mtindo wa wanafunzi kulipa KARO. Vyuo vinachukua wanafunzi wengi sana kiasi inakuwa ni mzigo mkubwa kwa lecturer mmoja. Darasa likiwa zaidi ya wanafunzi 100 ni shida sana! Na haya ndiyo matokeo yake na wakati mwingine kutunga maswali ya multiple choice katika hisabati. Ndugu yangu kindikwili nilipomweleza ukweli kuwa yeye bado ni ni kinda katika maswala ya elimu alipoanzisha uzi wa kudhani ni vyuo vya CBET vilivyooza, akadai kuwa mimi ni wa foundation (ref: NACTE iwe na mitihani kama NECTA).
 
Una lalamika mtihani siyo wa level ya varsity, Je. umeangalia course content inavitu gani, Je wanafunzi walipewa tests ngapi (umeweka test 1, I bet hiyo ilikuwa introductory part ya somo), practicals ngapi, quizzes ngapi, take home assignments ngapi? na je vyote hivyo vilikuwa na quality Sawa na test 1? It is unfair kumuhukumu mwadhiri husika kwa just only single parameter in this case test 1 .

Ni kweli kuna mapungufu mengi kwenye ufundishaji katika ngazi zote za elimu hasa kwa upande wa umma. Mapungufu mengine yanatokana na watawala waliowengi kwenye ngazi za elimu kutotimiza wajibu wao...hasa pale wanapopewa ushauri wa kuboresha sehemu husika na wao kupuuzia hasa ushauri huo ukitolewa na muhusika aliye kada ya chini. Kuna mentality fulani kuwa mwenye dalaja fulani la elimu ama utawala ndiye anayeweza kutoa ushauri unaofaa! Ninayo mengi. Ngoja niishie hapa kwanza!
 
Tunapojadili kuhusu kushuka kwa elimu yetu na kupungua kwa ubora wa wahitimu tusisahau kuangazia vinu vinavyozalisha wasomi hao. Juzi nilimtembelea rafiki yangu ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) tukabahatika kubadilishana mawazo ya hapa na pale kuhusu elimu inayotolewa chuoni siku hizi.

Moja ya sababu aliyonieleza inayopelekea kushuka kiwango cha elimu yetu ni wahadhili vilaza ambao huzalisha wanafunzi vilaza. Kwa kusisitiza hili jambo, ilinilazimu kufanya maarifa ya ziada ili kujiridhisha na maelezo yake. Ndipo nilipobahatika kupata paper iliyowahi kutungwa kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka wa pili katika Kitivo Cha Sayansi ya Chakula na Technolojia kama inavyoonekana hapo chini.

View attachment 442959

View attachment 442960

Nilipoona paper hiyo nilishikwa na butwaa. Nilidhani huenda ilitungwa kwa ajili ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na sio wa mwaka wa pili. Kwa mitihani ya kipuuzi kama hii tutarajie kuzalisha wasomi wa aina gani? Nilichogundua ni kuwa wahadhiri wengi wana uwezo mdogo sana. Ndio maana wanatunga mitihani hafifu kwa sababu hawana uwezo wa kutunga mitihani “akili kubwa”.

TUJADILIANE
Ni nani alaumiwa hasa kwa uuaji huu wa elimu ya taifa? Je ni serikali, wahadhiri, wanafunzi, sayansi na teknolojia, wazazi au jamii nzima ya watanzania?

Serikali ilaumiwe?
Kwa mujibu wa utafiti (usio rasmi) uliofanyika hivi karibuni, serikali ina mkono wake katika kudorora kwa elimu ya nchi hii kwa kuingiza siasa kwenye elimu, kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.

Kivipi? Ili kujijenga kisiasa serikali iliamua kwa makusudi kabisa kurahisisha elimu yetu kwa maana ya kupunguza viwango vya ufaulu (au kutanua goli) ili wanafunzi wengi zaidi wapate nafasi za kuingia sekondari. Mitihani ilirahisishwa mno kwa lengo la kuwafanya wanafunzi wafauulu kwa wingi ili kujaza shule za kata (sema makaburi ya kuzikia elimu) zilizoanzishwa kisiasa na serikali.

Lengo hasa lilikuwa ni kujaza shule za sekondari zilizokuwa zimefunguliwa kwenye kata, hata kama hazina walimu. Ndipo wakaibuka wanafunzi wanaofaulu kwenda sekondari ilhali hawajui kusoma na kuandika. Msumari wa kwanza wa sanduku la kuzikia elimu yetu uligongewa hapa.

Wanafunzi vilaza wakafaulu kwenda sekondari na huko sekondari pia mitihani ikarahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu kwenda vyuo vikuu. Matokeo yake, wanafunzi vilaza wakaingia vyuo vikuu.

Sababu nyingine inayopelekea serikali kulaumiwa katika hii kadhia ni uzembe wake wa kuwahudumia wanafunzi kwa maana ya kuwapa mahitaji yao ya msingi (boom) kwa wakati hivyo kupelekea wanafunzi hao kuishi katika mazingira ya njaa na kukata tamaa.

Na kwa sababu hiyo, wahadhiri wao huwaonea huruma na kuwatungia mitihani rahisi kwa kuwa hawasomi vizuri kwa sababu ya njaa kali waliyo nayo.

Baadhi ya wahadhiri wanalinda ajira zao au nao ni vilaza?
Ili kulinda ajira zao, wahadhiri nao wakaamua kutunga mitihani rahisi ili kupunguza idadi ya wanafunzi wanaoshindwa (discontinue) kuendelea na masomo. Jambo hili tunaweza kulitazama kwa kutumia dhana mbili: Mosi, wahadhiri huamua kutunga mitihani rahisi kwa sababu ya kulinda ajira zao.

Kwamba kama wakiamua kutunga mitihani migumu, na kwa kuwa wanafunzi ni vilaza, wanaweza kufeli darasa zima hivyo mhadhiri kukosa kazi ya kufanya. Kwa hiyo, ili kuhalalisha uwepo wake, inambidi mhadhiri atunge mitihani rahisi kuwawezesha wanafunzi wengi kufaulu.

Dhana ya pili ni kwamba wahadhiri wengi inawezekana kabisa wakawa vilaza, hasa ukizingatia namna wanavyopatikana, hivyo hutunga mitihani rahisi kulingana na uwezo wao mdogo.

Sayansi na teknolojia imechangia?
Kufuatia kukua kwa sayansi na teknolojia asilimia kubwa ya wanafunzi wanamiliki na kutumia vifaa vya intanet (kompiuta, simu, laptops, ipads, nk), hivyo hutumia muda mwingi kuchat na kutafuta wapenzi kwenye mitandao badala ya kujikita kwenye masomo.

NINI KIFANYIKE?
Serikali ichukue maamuzi magumu ya kufufua elimu kuanzia ngazi ya chekechea hadi chuo kikuu. Utaratibu wa kupata wahadhiri uangaliwe upya. Aidha, serikali ikaze uzi kwenye mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati ili kuwachuja vizuri wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu.

Tusiangalie zaidi takwimu za kisiasa. Ule utunzi wa mitihani migumu kama ilivyokuwa zamani urejewe. Hata ikibidi wanafunzi 100 ndio wafaulu kwenda chuo kikuu na iwe hivyo. Kusiwepo na uchakachuaji wa matokeo ili kuongeza kiwango cha ufaulu kisiasa.

MJADALA UMEFUNGULIWA….
Tujadiliane kwa ufasaha kuhusu hili tatizo la ukilaza vyuoni mpaka tupate jibu. Shambulieni hoja badala ya kumshambulia mtoa mada. Hata kama kuna mtu ataona hii hoja inamgusa moja kwa moja, awe mvumilivu…asitukane au kuchangia kwa jazba.

Sote tunajenga nyumba moja, tusigombee fito kamwe. Mods naomba mnilinde maana nina hakika kuna watu wanaoniona mbaya kwa kuwa wanadhani kitumbua chao nimekitia mchanga. Aidha kuna wanaopenda mteremko ambao hawependi kuona wanakaziwa kwa namna yoyote ile.


Nawasilisha.
Mkuu hiyo registration number AGC/__ inaonyesha kuwa huyo mwanafunzi anasoma Agriculture general na sio food science and technology ambao registration number zao huwa ni FST/____.
Pia hiyo kozi ya Ft 211 kwa sasa haipo labda kama ni zamani sana, ila kwa ubora wa mtihani huo napata mashaka mkuu sio kwa SUA hii ninayoifahamu mimi maana hata huo mfumo wa kuandika reg no hautumiki siku hizi ilikuwa ni zamani.
 
Aiseee!!

.. Ngoja nikuache.
Mimi waweza kuniacha lakini usiache kutetea hoja. Je wewe unaona ni sahihi kabisa wanafunzi wa chuo kikuu kutungiwa mtihani shallow kama huu?
 
Lakini haionyeshi ni level gani ie University/ secondary school/
Ni level ya chuo kikuu (SUA) mkuu. Angalia kule juu paper imeandikwa "DEPARTMENT OF FOOD SCIENCE AND TECHNOLOGY".
 
Back
Top Bottom