Wahadhiri Chuo cha Uhasibu Arusha wagoma

Belo

JF-Expert Member
Jun 11, 2007
12,882
10,193
Wahadhiri Chuo cha Uhasibu Arusha wagoma
WAHADHIRI wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) wamegoma kufundisha chuoni hapo kutokana na uongozi kushindwa kuwapa nyongeza ya mishahara yao iliyotolewa na Hazina.
Mgomo huo ambao ulianza rasmi jana umesababisha kuathirika kwa shughuli za kitaaluma chuoni hapo kwani wanafunzi wameshindwa kuingia madarasani kuendelea na vipindi vya masomo.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mmoja wa wahadhiri hao alieleza jana kuwa mgomo huo umefikiwa baada ya uongozi wa chuo kupuuza malalamiko yao ya muda mrefu kuhusu nyongeza ya mishahara.
Pamoja na Hazina kuwaongezea mishahara yao kwa asilimia 20 uongozi wa chuo hicho umekuwa ukiwalipa kwa viwango vya chini, alisema.
Alisema malalamiko mengine ni uongozi kujumuisha fedha za posho nyingine za kikazi katika mishahara yao kinyume cha utaratibu wa kawaida ambapo fedha hizo hutengwa na kulipwa kwa mtumishi huku malipo yakiainishwa wazi.
Akizungumzia madai hayo Mkuu wa Chuo hicho, Fredrick Manangwa alikanusha kuwapo kwa mgomo huo na kueleza kuwa uongozi ulikuwa kwenye mkutano na wawakilishi wa wahadhiri hao.

CHANZO NI HABARI LEO
 
Anakanusha hata kilichoandikwa na gazeti la magamba?watampeleka guantanamo
 
Back
Top Bottom