Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,887
- 21,973
Wagongwa na Treni Wakifanya Mapenzi juu ya Reli
Saturday, November 14, 2009 3:22 AM
Mwanaume mmoja wa nchini Afrika Kusini na mpenzi wake wamefariki dunia baada ya kugongwa na treni wakati walipokuwa wakifanya mapenzi juu ya reli.
Mwanaume mmoja wa nchini Afrika Kusini na mpenzi wake wamefariki dunia baada kugongwa na treni katika kitongoji cha Mpumalanga wakati walipokuwa wakifanya mapenzi juu ya reli.
Taarifa iliyotolewa na polisi ilisema kwamba wapenzi hao walipuuzia makalele ya dereva wa treni aliyokuwa akipiga kuwaamuru wapenzi hao watoke kwenye reli wakati treni lilipokuwa likiwakaribia.
Tukio hilo lilitokea majira ya jioni wakati dereva wa treni hilo alipolipitisha treni lake kwenye kituo cha treni cha mji wa Kinross ambacho kilikuwa hakitumiki.
"Wala hawakujali makelele yangu, walienda na shughuli waliyokuwa wakiifanya bila kujali chochote", alisema dereva wa treni hilo.
Taarifa zaidi zilisema kwamba eneo ambalo ajali hiyo ilitokea lilikuwa ni kama pori na kulikuwa hakuna makazi ya watu karibu.
Mwanaume alifariki hapo hapo kwenye eneo la ajali hiyo wakati mwanamke alifariki baadae hospitalini.
Saturday, November 14, 2009 3:22 AM
Mwanaume mmoja wa nchini Afrika Kusini na mpenzi wake wamefariki dunia baada ya kugongwa na treni wakati walipokuwa wakifanya mapenzi juu ya reli.
Mwanaume mmoja wa nchini Afrika Kusini na mpenzi wake wamefariki dunia baada kugongwa na treni katika kitongoji cha Mpumalanga wakati walipokuwa wakifanya mapenzi juu ya reli.
Taarifa iliyotolewa na polisi ilisema kwamba wapenzi hao walipuuzia makalele ya dereva wa treni aliyokuwa akipiga kuwaamuru wapenzi hao watoke kwenye reli wakati treni lilipokuwa likiwakaribia.
Tukio hilo lilitokea majira ya jioni wakati dereva wa treni hilo alipolipitisha treni lake kwenye kituo cha treni cha mji wa Kinross ambacho kilikuwa hakitumiki.
"Wala hawakujali makelele yangu, walienda na shughuli waliyokuwa wakiifanya bila kujali chochote", alisema dereva wa treni hilo.
Taarifa zaidi zilisema kwamba eneo ambalo ajali hiyo ilitokea lilikuwa ni kama pori na kulikuwa hakuna makazi ya watu karibu.
Mwanaume alifariki hapo hapo kwenye eneo la ajali hiyo wakati mwanamke alifariki baadae hospitalini.