Wagombea mwakani kubanwa kitaaluma

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Naona wameamua la maana.
Wagombea mwakani kubanwa kitaaluma

Baraza la Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) limepitisha uamuzi wa kuishirikisha Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuhakiki vyeti vya wote wanaoomba kuwania nafasi za kisiasa ili sifa zao kielimu zitambulike.

Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya, aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, TCU imewasiliana na NEC kwa barua, ili utaratibu huo uanze kutumika katika uchaguzi mkuu ujao mwakani.

Nkunya alitoa taarifa hiyo wakati akizungumzia maonyesho ya vyuo vikuu yaliyoandaliwa na TCU yatakayoanza kesho hadi Aprili 24, mwaka huu. “Baraza letu limepitisha uamuzi ili watu wanaotaka kugombea nafasi za kisiasa, vyeti vyao vihakikiwe, ili akipita sifa ijulikane rasmi kama ni daktari basi awe daktari na si daktari feki,” alisema Profesa Nkunya.

Hatua hiyo ya tume inatokana na kilichoelezwa na Nkunya kuwa ni kukithiri kwa vyuo na vyeti bandia nchini, jambo ambalo alisema wamejipanga kulivalia njuga kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha Tanzania haiangamii kitaalamu na kitaaluma.

Alisema orodha ya vyuo visivyotambulika vya nje ambavyo Watanzania wengi wakiwamo mawaziri na wabunge wamesoma, ni ya kweli na kwamba kama kuna mtu anahisi kuonewa ruhusa kwenda mahakamani.

“Sisi TCU tumepewa jukumu na taifa hili, kuhakikisha elimu inayotolewa kwa Mtanzania inatambulika duniani kote na inatolewa na vyuo vinavyotambulika, tulitoa orodha ya vyuo feki sasa kama kuna mtu anapinga aende mahakamani,” alisema Profesa Nkunya wakati akijibu swali juu ya ukweli wa orodha ya vyuo feki iliyotolewa na tume hiyo hivi karibuni.

Akizungumzia tatizo la kughushi vyeti, alisema linazidi kukua, hali ambayo inatishia sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na uwezekano wa Tanzania kuzalisha wataalamu feki. “Tatizo la kughushi vyeti linazidi kuwa kubwa nchini hali ambayo ni hatari na haipaswi kufumbiwa macho, si siri tatizo hili lisipodhibitiwa nchi itaenda pabaya, tushirikiane tulidhibiti,” alisema.

Kwa mujibu wa Katibu Mtendaji huyo wa TCU, katika udahili wa mwaka 2008/09 pekee, tume hiyo ilipelekewa majina ya wanafunzi zaidi ya 200 ambao vyeti vyao vinasadikiwa kughushiwa. “Hii ni hatari, tusaidiane kukabiliana na tatizo hili, tukiacha liendelee nchi yetu itakwenda pabaya na hatari yake ni kuzalisha wataalamu feki,” alisema Nkunya.

Alisema kwa sasa watu wanaoongoza kwa kupeleka vyeti vya kughushi vyuoni ni waliosoma miaka ya nyuma, hali inayoonyesha ni upungufu wa nidhamu ambao inabidi uchukuliwe hatua. Alitoa mfano wa Liberia ambayo iliacha tatizo hilo la kughushi na kuwa na vyuo feki likakua na kusema nchi hiyo imefanya elimu yake kutokuwa ya kuaminika.

“Kwa sasa hali ya Liberia kielimu ni mbaya, waziri anaweza kuanzisha chuo chake na kujipa shahada, hiyo elimu gani?” Alihoji. Profesa Nkunya aliitaka jamii isiliache tatizo hilo mikononi mwa TCU na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) pekee, bali liwe mikononi mwa kila mtu vikiwamo vyombo vya Dola, katika kupambana nalo.

“Sheria ziangaliwe, kwani kukithiri kwake kunatokana na wanaokamatwa kutochukuliwa hatua thabiti za kukomesha tabia hiyo,” alisema. Alisema katika kuhakikisha kuwa hadi kwenye ofisi watu wenye vyeti bandia wanadhibitiwa, TCU pia imejipanga kurekebisha sheria yake, ili iwe na uwezo wa kutembelea ofisi moja baada ya nyingine, kuhakiki vyeti vya watu.

Alisema imeshaanza mchakato wa kurekebisha sheria hiyo. Hivi karibuni, NECTA ilitoa taarifa na orodha ya maelfu ya wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya ualimu wanaotarajia kufanya mtihani wao wa mwisho mwezi huo, ambao walibainika kutumia vyeti bandia na kuwataka wawasilishe vithibitisho, vinginevyo hawataruhusiwa kufanya mtihani.

Hata hivyo, kutokana na kukithiri kwa vyeti bandia, serikali imedhamiria kupambana na watumishi waliowasilisha vyeti bandia baada ya idara zote za serikali kutakiwa kuhakikisha zinawasilisha vyeti vya watumishi wake kwa ajili ya uhakiki, mchakato ambao unaendelea hadi sasa, huku baadhi wakiachishwa kazi kutokana na kukutwa na vyeti bandia.
 
Hizi nazo ni kelele za kisiasa.
tatizo kubwa la kufoji vyeti linasababishwa na mwajiri.Mwajiri ndiye anayeamua cheti gani anakihitaji na hicho cheti kinauwezo gani. Mwajiri mwenye cheti famba, kasoma elimu famba anamwajiri mwenye famba kwani anaogopa cheti cha ukweli kitamsumbua.

Tanzania mwajiri namba moja ni serikali na Serikali hii imekubali kuingiza wasomi feki ikijua na kukuza uzalishaji wa vyeti hivyo. Nijuavyo mwajiri makini huhakikisha kuwa anampata mfanyakazi makini mwenye vyeti kutoka shule inayotambulika na uwezo thabiti.

Sasa unategemea Lawrence Gama atamwajiri nani wakati yeye tayari ni feki, au Mkulo atampa nani ajira wakati yeye ni serikali na yeye ni feki, au Nchimbi au nk hawa wote ni fafa na wengine wengi tatizo tunalo tunalijua halafu tunataka kujifanya tunatengeza system my a......

Sharti la kugombea au kuwa mwanasiasa ni kujua kusoma na kuandika. Wala katiba haisemi uwe na cheti cha darasa la saba. Ni rahisi sana kuizunguka system. Tume ya taifa watasema wanajua kusoma na kuandika wapiga kura wataambiwa kuwa wana PHD. Then what next.

Vyeti feki vibanwe makazini na waliopata faida na vyeti hivyo tuwanyang'anye kazi na wafunguliwe mashitaka ya udanganyifu na hasara walizosababisha na ufeki wa vyeti vyao, na kama wako makini waanze na Mkulo, Nchimbi, Kamala, nk....

Pili swala la baraza la mitihani haya mambo ni ya hawa hawa wanasiasa kama kina Lowasa, na JK na wengine wengi vimemo vyao ndivyo vinavyotoa vyeti feki.

Wakati Magogo akiwa pale utumishi alishuhudia fafa wengi wakiingizwa makazini alipouliza alijibiwa unataka kazi au pitisha Tanzania yetu haina kujiuzulu kwa kukataa ya bosi wako mambo ni kanyaga twende.
 
I would say they should first start screening their professors even before venturing with this hypocrisy.

Yule mwalimu mzuri alisema "Toa boriti iliyopo jichoni mwako kwanza kabla ya kutoa kibanzi kilichopo katika jicho la mwenzako"

I am for verification of purpoted academic qualification, but this piece does not categorically make clear whether this is about verification or "screening", in fact the heading makes it sound like they want to screen out "uneducated" people - read the not formally educated - from entering that august Dodoma house, a tragedy.

And even the case of verification of purpoted academic qualifications, who is to say that this body is not going to be politicized? What precedents are we setting towards an Orwellian police society?

In any case ubunge unahitaji academic qualification? I can go further and even say this proposal has some unconstitutionality about it, since it imposes restrictions on elected office far and above those in the constitution.For this to work, there must be a constitutional amendment.

Don't get me wrong, I hate fake PhD's as much as the next fine Tanzanian, but I smell jockeying for position and all the shenanigans that comes with it here.

Aspiring MPs for intense screening

2009-04-21 12:43:09
By Joyce Kisaka



The Tanzania Commission of Universities has announced that it is seeking permission to make a thorough screening of the academic qualifications of all people planning to vie for parliamentary seats beginning next year.

TCU Executive Secretary Professor Mayunga Nkunya told journalists in Dar es Salaam yesterday that the commission has already sent a proposal to that effect to the National Electoral Commission (NEC).

He said reasons for the move included the fact that the problem of being hunting for employment, benefits and favours on the strength of fake certificates ``has become chronic and serious attention is needed to curb this kind of cheating``.

Should NEC endorse the proposal before the next (late 2010) General Election, all those interested in standing as parliamentary contenstants be given approval for authenticity.

Elaborating, Prof Nkunya said the electoral body would help in ensuring that TCU was furnished with a list of all aspirants well before campaigns got under way to enable the screening exercise to be foolproof and run smoothly.

He added that his office was in the process of reviewing the relevant pieces of legislation, ``and we have every hope that we will be vested with enough powers to move from office to office to trace forged certificates and other credentials``.

``As of now, our commission has no legal authority to make follow-ups on such credentials. We can only do so after the Universities Act is amended accordingly,`` he pointed out.

The professor insisted that the incidence of forgeries of academic certificates in the country had assumed alarming proportions, ``and hence our decision to tackle the vice right at its roots before our nation sinks under the weight of this crime wave because the law as it now stands does not serve as an effective enough deterrent``.

He revealed that TCU intercepted some 200 fake certificates issued by the National Examinations Council of Tanzania (Necta) in 2008/09.

Asked for clarification on the criteria used to discredit cabinet ministers whose PhDs were shot down recently by his commission, Prof Nkunya said TCU experts cross-checked and double-checked with the American Embassy in Tanzania for details on universities recognised by the US education authorities.

Commenting on threats by some of the ministers concerned to take TCU to court over the matter, he said: ``They have the liberty to proceed (with legal action). We have impeccable proof of what we have said and are confident of emerging triumphant.``

``The only message we have for any ministers planning to seek redress in court because they feel that we have lowered their reputation by pointing out that the universities they went to are not recognised is that they can go on - and we will meet there,`` he added.

Prof Nkunya explained that it was not part of TCU`s modus operandi to rush into announcing the findings of its investigations without having made a thorough check on people and educational institutions at the centre of controversies.

He made an impassioned appeal to all the respective stakeholders ``to work together to solve this serious problem facing the credibility of education and institutions of learning in our country and indeed the image of our nation``.

He said TCU’s investigations showed that forgeries of academic credentials in the country have been especially rampant in the last five to six years, but he would not say why.

Recent years have witnessed a rise in the number of allegations of some members of the academic staff of some of the 30-plus officially recognised universities in Tanzania having fraudulently landed employment, including by brandishing fake certificates.

There has also recently been a rise in the incidence of secondary school leavers being found with distorted and otherwise faulty Nacte certificates, some of which have been presented by people seeking employment or admission into training institutions and universities.

Cabinet ministers and legislators are among the recipients of allegedly questionable academic qualifications, chiefly PhDs, from overseas colleges and universities lacking international recognition.

However, the allegations have been commonly dismissed as baseless and driven by malice.

Many of the suspicious credentials have been obtained through undergraduate and advanced correspondence courses, at times online.


SOURCE:
Guardian
 
Last edited:
The Tanzania Commission of Universities has announced that it is seeking permission to make a thorough screening of the academic qualifications of all people planning to vie for parliamentary seats beginning next year.

No no no. No way Jose! This is interference with the democratic process of representation. Academic qualifications have no place in this. Constitutional qualifications are enough. The rest should be up to the constituents to decide.
 
No no no. No way Jose! This is interference with the democratic process of representation. Academic qualifications have no place in this. Constitutional qualifications are enough. The rest should be up to the constituents to decide.
I do agree with you sir.
It looks like we do not know, the root cause of our problems as a nation.
 
Tatizo la nchi yetu linapokuja suala la ajira, what matter is technical know who na si technical know how. Wanatuhadaa wananchi, wanajuana. Sana watakaokamatwa ni vidagaa tu, Mapapa na Masangara yataendelea kutesa kama kawa. Yako wapi ya PCCB? Lini Kigogo amekamatwa kwa rushwa. mwenye macho haambiwi tazama. kalagabaho.
 
As long as sifa za kuwania ubunge zinabakiwa kuwa kujua kusoma na kuandika, sioni ni jinsi gani kampeni hii itawaathiri
 
The issue here should be all citizens and non-citizens looking for employment should go through a verification process of there certificates.Politicians who claim to posess one,two or doctorate degrees should also pass through the same mechanism.I also totally disagree with the notion of a person who can read and write can be a AN EFFECTIVE councillor or member of parliament.
 
The issue here should be all citizens and non-citizens looking for employment should go through a verification process of there certificates.Politicians who claim to posess one,two or doctorate degrees should also pass through the same mechanism.I also totally disagree with the notion of a person who can read and write can be a AN EFFECTIVE councillor or member of parliament.

Are you saying there is no chance that a person who has not been trained formaly can be effective?

Are you saying the measure of effectiveness is in the amount of formal education?

Mbona tunaye Fundi Mchundo hapa, ambaye anasema hajawa formally educated kwa sana (ndiyo maana ni Fundi Mchundo na si Engineer) lakini anatoa hoja hata Ma-Engineer na Wanasheria wanakuna vichwa?

Have you heard of petty herdsmen with knowledge of ecology far exceeding that of foramally trained ecologist? Are you acquinted with the Gerald Diamond's narration (iN "Guns, Germs and Steel" of how he was amazed by the knowledge about their environment possesed by the natives of Papua New Guinea, knowledge gained solely by observation.

Granted, a formally educated person has a higher probability of being exposed to many ideas than one that is not formally educated, but looking at education with the simplistic eye of reducing education to mean "formal education" could equally prove counterproductive and repressive.

People should be elected on the merit of what they have accomplished and what they can demonstrably accomplish, not how many degrees they hold.

The lot of professor-administrators Tanzania has had has produced little if any results so far.

I still say the whole thing has an aura of political intimidation.If they are to verify fake certificates/ degrees, they first of all must start this in their own house so we know the people who will be doing the verification are qualified, that is first.

Second, this whole exercise has an air of precedent setting erosion of liberty and is prone to all sorts of political witchhunt, first of all do we have the right criteria? Do we have the standards? What is our accreditation body/ authority? What does it mean to be accredited? How will the accreditation apply? Will they apply retroactively? You find more questions than answers with the entire proposal.

Third, whatever is done to ensure the integrity of the parliament through the verification of qualification must ensure that no disadvantage is introduced to the not formally educated (are they going to verify prior to elections? If so, will this be a factor in who is nominated/ elected? If so will this not carry a whiff of unconstitutional disadvantage to the not formally educated?)
 
waanze na Nchimbi,kamala,Nagu,mathayo David msuya,makongoro mahanga,lukuvi william hawa wote vyeti feki.
 
Hell No! Hakuna kitu kama hicho hapa tunaachwa solemba unless kunawatu waanahisiwa kuwa threat kwa waliopo madarakani hasa wabunge.
 
Bila kumsahau Aziza Sleyum Aly viti maalum Tabora, aliishiia form two lakini sasa ana cheti cha form six
 
Back
Top Bottom