Uchaguzi 2020 Wagombea 8 wajitokeza kutaka kumng'oa Job Ndugai Kongwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,635
218,067
Taarifa kutoka Kongwa zinaeleza kwamba mpaka jana watia nia 8 walishachukua fomu za kugombea ubunge Jimbo la Kongwa ambalo lilikuwa chini ya Job Ndugai ambaye pia alikuwa Spika wa bunge la 11 , ambalo wadau wa siasa wanadai lilivunja rekodi , haifahamiki lilivunja rekodi gani .

Bali kinachofahamika ni kuzomewa kwa Job Ndugai na wapiga kura wa Kongwa kwenye mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mwenyekiti wa ccm Ndugu Magufuli .

Majina yao haya hapa : Moris Zaidi , Dr Samora Mshang'a , Apiov Lywiva , Dr Philemon Saigodi , Dotto Chibupa , Martin Chihimba na Sahewa Elias (majina yanaweza kuongezeka kwa vile muda bado unaruhusu )
 
Atawatandika bakora. Hawamjui Ndugai hawa. Yule aliyepigwa 2015 alipozwa kwa kupewa uDC sijui uDED.

Dawa waungane waweke mshindani mmoja dhidi ya Ndugai.
 
Kama aliweza kumyima mgonjwa matibabu na isitoshe akamfukuza mpaka ubunge aliopewa na wananchi huyo ni binadamu kweli? Serious nikumuangalia huwa nawazaga huyu ni binadamu wa kawaida kweli? Yaani Mungu anakazi sana siku ya kiama.
Alimtegemea binadamu mwenzake Bw.Jiwe..muache afe kibudu shenzytaipu!
 
Kuna majimbo ya kutia nia harafu unapita kule mojawapo ni la Ndugai, Majaliwa, maana unajua huwezi pita ata shetani ashuke duniani
Wapumbavu tu ndo wataenda tia nia huko. Magu alishasema akiwa kwenye hayo majimbo, atawashangaa watakaochukua fomu kutaka kushindania hayo majimbo. Wenye majimbo yao kwa kazi walizofanya, waatakiwa kupita bila kupingwa.

Watia nia hao wajue hata Ukatibu tarafa au kata hawata upata.
 
Back
Top Bottom