Wageni wa Ulaya, America na Asia hupewa thamani kubwa mno kuliko wazawa wa Tanzania

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,032
Video ya utangulizi hii nasisitiza sana uiangalie mpaka mwisho, utapata picha kamili kabla hujasoma hii maada




Tangu nimezaliwa hapa nchini ma hadi sasa nikiwa na miaka 31 kuna mengi nimeyaona na kujifunza katika hii nchi, kitu kimoja wapo ni thamani kubwa mno anayopewa foreigner kuzidi mwananchi, na hao wageni ninaowazungumzia ni watu wa bara la ulaya (wengi wazungu), wakifuatiwa na watu wa bara la asia (sana sana waarabu)

Nitaanza kuchambua matukio kadha na kadha yaliyonisukuma kuandaa hii maada.

KUWA KIVUTIO KIKUBWA WAPITAPO MITAANI

Hapa nimeshudia matukio kadha na kadha, mzungu/mjapani anapopita mitaani watu wengi hunshangaa, na wengine huanza kumpa salamu hata kwa kiingereza kibovu (hey, how you doing, whats up,n.k) lugha ikikataa hata ishara hutumika, Ni kama anakuwa na positive attention kubwa mno



KUWA NA DHANA YA KUPENDA ZAIDI KUAJIRIWA NA MZUNGU UKIACHANA NA SERIKALI

Hapa wengi wanapokosa ajira serikalini huwa na dhana ya kwamba sehemu nzuri inyofatia ni kwa mzungu, ikumbukwe nae mzungu anafukuza kazi kama mtanzania, mzungu hataki mchezo kwenye kazi kama mtanzania, mzungu yupo kwajiiya faida kama mtanzania.

KUSHUGHULIKIWA KWA UHARAKA NA UMAKINI KWENYE OFISI BILA RUSHWA

Nakumbuka niliwahi kufanya kazi sehemu flani hivi, kuna vibali flani vilikuwa vikitoka kwa biashara flani, wengi walikuwa wanatoa na kitu kidogo ili mambo yaende fasta kidogo, Ila kuna siku alikuja jamaa flani wa sweeden kavaa kikaptura, alifanyiwa haraka tu bila hata kutoa cha ziada, alipotala kuondoka pia alipewa kitabu cha wageni kusaini, nikaona hapa kuna tatizo,Ofisi ya umma mtu mweusi hasa mbongo ukivaa ndala na kipensi hutaruhusiwa kuingia ndani,ila mzungu akivaa kipensi na ndala watamruhusu

HUPEWA THAMANI KWENYE MAHUSIANO YA URAFIKI NA MAPENZI
Tukianza kwenye mapenzi hapa, vijana wengi hupenda ku date na wazungu na hili halina mjadala, wana misemo yap kwamba wanasafosha nyota kwa mwarabu / mzungu. Ukija kwenye urafiki pia ni hivyo hivyo.

KUSAMEHEWA SANA PALE WANAPOKOSEA
Mnaweza kupanga foleni, akatokea mzungu/mwarabu/mjapani, n.j yeye akapita tu ila hakuna wwa kimkoromea tofauti na sisi tukifanya hivi,

Hali inakuwa tofauti sisi tukienda huko kwenye nchi zao hasa ambazo wamejazana wao kama ugiriki, romania, urusi, n.k
 
Wenzetu tayari walishajitengenezea mazingira ya kuogopwa,kuabudiwa,kusifiwa na kunyenyekewa toka zamani hizo,sisi ngozi nyeusi tulishaanzwa kutengenezewa mazingira ya uoga, mazingira ya kutojikubali pia toka zamani na Hilo tukalikubali kwa mikono yote miwili,tumekuwa watumwa wa kiakili muda mrefu Sana bila kufahamu huu ugonjwa umeanzia wapi na ni upi, utumwa huu ndio umetufanya tuwe maskini Hadi le.

Jambo ulilolisema hapo ni kutokana na umaskin wetu uliosababishwa na utumwa kifikra,ili uwe mtumwa lazima ukubali anachotaka bwana wako Sasa sisi tumeshakubali anachotaka bwana wetu ndo Mana unaona hizo shida hapo juu.

Tunakubali kila kitu Sasa hapo kwanini usiwe na 'inferiority complex',ili uonekane umestaarabika lazima ufanye,uishi Kama wao,Mambo uliyosema ni kweli na mzizi wake ni mrefu na tumeukuta...
 
Kuna kinachoitwa shithole countries. Akuheshimu nani kama unatokea kwao huyu:

IMG_20210930_170832_807.jpg


Na maisha yanaendelea kama vile hakuna kilicho wapi kutokea?
 
Mtu mweusi ni dhaifu, mbinafsi, na mpumbavu toka vizazi. Hawa watu walikuja nyumbani kwetu, wakatutawala na kutufanya watumwa, kwa kusaidiwa na baadhi yetu.

Kila race duniani inatuchukulia poa, hata wenyewe tunajichukulia poa.
 
Kuhusu wazungu kuwa kivutio wanopokuwa kwetu nadhani ni jambo la kawaida ata wewe jaribu kwenda kwenye hayo mataifa ya wazungu utakuwa tu kivutio.Jaribu siku moja ufike Russia usipokuwa kivutio siku ukirejea njoo nkupatie gharama ulizotumia.

Kuhusu jambo la watu kupenda ajira za wazungu nadhani ni malipo mazuri.

Kuhusu kushughulikiwa haraka nadhani wazungu wako organised kupita waswahili na kingine ni kwamba tunawahitaji sana wao kama wawekezaji kupita wao wanavyotuhitaji sisi ili watengeneze faida kupitia uwekezaji wao

Kuhusu mahusiano nadhani watu wanataka kupata radha tofauti tofauti.

Sema kikubwa nini ISHI tu man achana na hizi michakato za wazung, na kukupa ukweli wa mamabo ata wachina wamewahi pitishwa katika yote haya lakini nenda sahivi uwaletee wenge lako uone.Unajua walifanya nini kuyamaliza yote? Jibu ni kwamba ISHI basi
 
Kuhusu wazungu kuwa kivutio wanopokuwa kwetu nadhani ni jambo la kawaida ata wewe jaribu kwenda kwenye hayo mataifa ya wazungu utakuwa tu kivutio.Jaribu siku moja ufike Russia usipokuwa kivutio siku ukirejea njoo nkupatie gharama ulizotumia.
Ni rahisi kwa mzungu kitembea peke yake hata uwanja wa taifa kwenye mechi ya watani lakini ni ngumu kwa mwafrika kwenda huko urusi asibaguliwe, jamaa hawa baadhi yao wanabagua mno watu weusi ila wao wakija huku wanaonekana keki
 
Mtu mweusi ni dhaifu, mbinafsi, na mpumbavu toka vizazi. Hawa watu walikuja nyumbani kwetu, wakatutawala na kutufanya watumwa, kwa kusaidiwa na baadhi yetu.

Kila race duniani inatuchukulia poa, hata wenyewe tunajichukulia poa.
Yani hapa nchini tubaguane, ndani ya bara letu tubaguane, khaaa yani nashindwaga kuelewa, hata hapo south africa ni mfano hai
 
Kuhusu wazungu kuwa kivutio wanopokuwa kwetu nadhani ni jambo la kawaida ata wewe jaribu kwenda kwenye hayo mataifa ya wazungu utakuwa tu kivutio.Jaribu siku moja ufike Russia usipokuwa kivutio siku ukirejea njoo nkupatie gharama ulizotumia.
Wewe huwi kivutio....unakuwa KITUKO!
 
Kwanza ni utumwa ndio ulaumiwe na bado ipo vichwani mwa wengi

Mtu yupo tayari kumbebea mzungu mzigo wake hata kama ni afisa huko airport
Kuhusu kutokutoa rushwa hapo umechemka maana ofisi yeyote mswahili hapewi thamani kwa sababu ya hiyo rushwa sana atqpewa buku ila mzungu ni $ na hao wengine pia

Mfanyakazi huyo anaabudu foreigner kwa sababu chakula chake kinachangiwa humo
 
Ni rahisi kwa mzungu kitembea peke yake hata uwanja wa taifa kwenye mechi ya watani lakini ni ngumu kwa mwafrika kwenda huko urusi asibaguliwe, jamaa hawa baadhi yao wanabagua mno watu weusi ila wao wakija huku wanaonekana keki
Kama kubaguliwa sawa sema nilikuwa naongelea kuwa kivutio.Lakini kingine ni kwamba ni uzembe wetu tu jambo la kubaguliwa.Nasema hivi kwa sababu nimewahi kumsikia Michael Jordan siku moja anahojiwa kuhusu ubaguzi wa rangi Marekani alisema ukiwa mzembe utaonekana unabaguliwa ila ukifanya mambo yakaoneka utaheshimika man.
 
Kuhusu kutokutoa rushwa hapo umechemka maana ofisi yeyote mswahili hapewi thamani kwa sababu ya hiyo rushwa sana atqpewa buku ila mzungu ni $ na hao wengine pia
Sisi tunatoa rushwa hata kwenye vitu ambavyo ni haki yetu kabisa kupata kihalali, ila kwa wenzetu yani anashughulikiwa chap chap tena hadi mtu anaemshughulikia anajichekesha flani hivi, nenda wewe sasa uone, mzungu m anatoa rushwa kwenye vitu anavyojua kabisa hapa sheria zinapindishwa, mfano mikataba ya kinyonyaji ya madini
 
Wewe huwi kivutio....unakuwa KITUKO!
Umejibu kwa ufupi na usahibi wa hali ya juu, Mbaya zaidi hata nchi kama brazil huko wachezaji wa mpira weusi wengi wakiyapata maisha ni chap chap wanaoa wazungu, kuanzia kina pele, ronadinho, neymar, n.k
 
Uzi safi kabisa kasheshe inaanza Air Port unapoingia Mzungu anaonekana mwenyeji na wewe unaonekana mgeni wakati umekuja kwenu ,wataanza kukusumbua lkn hii kdg ilikuwa zamani siku hizi kuna mshine za scan any way wakiamua kukusumbua utasachiwa mpk ujutee kuja kwenu lkn mzungu huyooo anapita zake.Ni kweli kabisa maofisi mengi ya serikali wanawajali wazungu sana sana ,niliwahi kugombana nae mmoja bandarini kuelekea Znz tuko kwenye line wale makuli wanampitisha juu juu nikamsomea yule mzungu na wale makuli vile vile.
 
Uzi safi kabisa kasheshe inaanza Air Port unapoingia Mzungu anaonekana mwenyeji na wewe unaonekana mgeni wakati umekuja kwenu ,wataanza kukusumbua lkn hii kdg ilikuwa zamani siku hizi kuna mshine za scan any way wakiamua kukusumbua utasachiwa mpk ujutee kuja kwenu lkn mzungu huyooo anapita zake.Ni kweli kabisa maofisi mengi ya serikali wanawajali wazungu sana sana ,niliwahi kugombana nae mmoja bandarini kuelekea Znz tuko kwenye line wale makuli wanampitisha juu juu nikamsomea yule mzungu na wale makuli vile vile.
😂😂 tuna ukarimu na roho nzuri kwa wageni ila kwetu sasa dahh,
 
Sisi tunatoa rushwa hata kwenye vitu ambavyo ni haki yetu kabisa kupata kihalali, ila kwa wenzetu yani anashughulikiwa chap chap tena hadi mtu anaemshughulikia anajichekesha flani hivi, nenda wewe sasa uone, mzungu m anatoa rushwa kwenye vitu anavyojua kabisa hapa sheria zinapindishwa, mfano mikataba ya kinyonyaji ya madini

Huu unafiki wa kujichekesha nimeuona sana airport yaani mtu anajichekesha ila sasa ifike zamu yako
Unamuona jamaa kabadilika ghafla utafikiri umemgongea dem
Hao wazungu mpaka kwa traffic wanapigwa tena anaona hivi hivi anaibiwa
Kuna mmoja alirekodi akiwa zanzibar traffic officer anaomba rushwa ya lazima jamaa akaiweka kwenye YouTube akasema sirudi tena

Rushwa wanapewa hata kwenye visa tu acha hiyo mikataba mikubwa
 
Back
Top Bottom