Wageni kuwepo na kibali cha kufanya kazi

geosenny

New Member
Sep 2, 2011
2
0
ndugu zangu kuna maeneo mengi nimefanya uchunguzi na kubaini wageni wanafanya kazi hata bila kibali cha nchi cha kazi ( working permitt)
je ndugu zangu hili mmeshaliona? au na serikali yetu ipo au haijapata taarifa . tufanyeni uchunguzi ili tuisaidie serikali kuwafichua hawa watu ili tuwe wazalendo wa kweli.
 
Wewe ndiyo uwe mfano kwa kuwapeleka hao uliowaona kwenye vyombo vya sheria. Sasa unapoanza kulalamika haisaidii kitu, sana sana utaonekana mzandiki tu.
 
Serikali bila raia si Serikali. Onesha mfano na kuwa Umeifanyia Serikali yako kitu cha maana na si kungoja ikufanyie tu.
 
Acha wafanye kaz,kama pesa za kibali zinaliwa na watu binafsi bila kwenda TRA,nafikiri mlisikia kuhusu rushwa za uhamiaji kwa wale wa pakistan,rushwa imekuwa kubwa,ata ukireport baada ya muda utashikwa na police kwa maojiano zaidi uku watuumiwa wakienjoy na kula bata,nafikiri ulisikia kuhusu mwanaharakat msema kweli,ivo waache tu wapige kaz,kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe
 
Hii biashara ipo na inashughulikiwa, ila raiya nao wanapaswa kushirikiana na uhamiaji, si kila kitu kuiachia serikali.
 
Raia wanajitahidi sana katika hili nikiwemo mmoja wao katika kuisaidia serikali yetu, ila isipokuwa wahusika hawaonyeshi ushirikiano na wanaojitolea kuwafichuwa watu kama hao. Pesa inaongea zaidi.
 
kwanza wanyasa wamejazana nao wanajiita watz hata kiswahili shida bado mataifa mengine yan nchi yetu bado sana ila ww toka nenda kwenye nchi zao shida utakayoipata kama huna vibali lkn kwetu fresh tu yaaaaan haina nouma tubadilike jaman
 
wewe ndiyo uwe mfano kwa kuwapeleka hao uliowaona kwenye vyombo vya sheria. Sasa unapoanza kulalamika haisaidii kitu, sana sana utaonekana mzandiki tu.

haya mambo mnachukulia kimchezo sana,labda hujaelewa topic inazungumzia nini
 
haya mambo mnachukulia kimchezo sana,labda hujaelewa topic inazungumzia nini

Naungana mkona hoja nawe,

Mwita maranya 25/FaizaFoxy ndugu zangu sidhani hata nyie hii topic mtaipinga fika kabisa sidhani humu ndani ya JF mnataka kuniambia UHAMIAJI hawachakachui? Mikoa iliyo na mahoteli mkaulize kama vibali hutoka kihalali na kama utakuta kapewa kibali na ukikichunguza vizuri sicho sawa na kazi aliyo omba au aliyo ajiriwa. pili kuna unyanyasaji esp kwenye mahotel wazungu na wahindi hawa wao wanalipwa vyema kabisa lakini mwafirika unaye pigika huko viwandani na kwenye mahoteli duuuu kipato chako hata nauli ya daladala kwa mwezi hakifiki alafu JK huko Arusha alipo fungua hotel ya Snow-crest akatamka kuwa watanzania tuna tabia ya kudokoa je alithibitisha hilo vipi? kwa kuambiwa na yule rafiki yake mwenye hotel kule bagamoyo?? au.Mh. Pinda nae akasema bungeni kipindi cha maswali na majibu elimu yetu bado anakithibitisho gani kuwa elimu yetu ya Hotelia ni bado???

Haya matamko yote ya viongozi wetu wakuu serikalini ni tosha kabisa kuwapa mianya huru ya wenye mahotel(Wamiliki) kuajiri watu wa nje kwa hali na mali kwa aina yoyote na kuhakikisha wanapata vibari fake toka Uhamiaji na kukiuka sheria za nchi,

Hebu tuwaulize hawa Uhamiajai hawa wageni wa nje wakija nchini hufanya kazi kwa muda gani na wakisha tupa huo ujuzi wanatupisha au wana baki??? maaana una mkuta Financial Controller ni Mhindi kwa kiwanda mmoja amefanya kazi zaidi ya miaka 7 mahali pamoja na cheo kile kile hapo ndugu zangu mwataka kuniambia hatuna CPA holder wa kuzifanya kazi hizo? tuna Chef wangapi humu nchini wamesoma jamani tuache kubeza elimu yetu tuna uwezo haya tunayo yasema hapa kuna baadhi yetu na uhamiaji wao wanaona sawa kwani wanafaidika kwa namna mmoja au nyingine.

My Take;


Utoaji wa vibari kwa wageni kufanya kazi nchini kwetu rushwa ni nyingi sana vibari havizingatii sheria ya nchi inavyo takiwa
 
Hii biashara ipo na inashughulikiwa, ila raiya nao wanapaswa kushirikiana na uhamiaji, si kila kitu kuiachia serikali.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Uhamiaji kazi yao nikutoa vibali vya wageni kuingia nchini na si vinginevyo: kama kuna wageni wanaofanya kazi nchini bila kuwa na vibali vya kufanya nchini, peleka taarifa haraka TIC au Wizara ya Kazi na Ajira kupitia ofisi zao za Idara ya Kazi zilizoko takribani kila mkoa na baadhi ya Wilaya.

TIC na Wizara ya Kazi na Ajira ndiyo wenye mamlaka ya kutoa vibali vya wageni kufanya kazi Nchini.

Tafadhari wenye taarifa madhubuti ziwakilishe panapostaili.
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Uhamiaji kazi yao nikutoa vibali vya wageni kuingia nchini na si vinginevyo: kama kuna wageni wanaofanya kazi nchini bila kuwa na vibali vya kufanya nchini, peleka taarifa haraka TIC au Wizara ya Kazi na Ajira kupitia ofisi zao za Idara ya Kazi zilizoko takribani kila mkoa na baadhi ya Wilaya.

TIC na Wizara ya Kazi na Ajira ndiyo wenye mamlaka ya kutoa vibali vya wageni kufanya kazi Nchini.

Tafadhari wenye taarifa madhubuti ziwakilishe panapostaili.


Idara ya kaziu ndio uozo mtupu hata kutetea maslahi ya watanzania wafanyakazi ndio hakuna na hao uhamiaji wao ni kama wamejiaralishia kuwa ndio watoa vibari vya kazi na ndio maana nika sema ukichunguza sna unakuta kibari cha mgeni kuwa nchini kina sema kazi yake tofauti na kazi aliyo mleta nchini hapo tayari uhamiji na idara ya kazi ni zero
 
Naomba ku uliza swala moja.....

Ni nini inayemfanya mfanybiashara amlipe mgeni mshahara mkubwa kuliko mtanzania???

Ninavyo waelewa wanabiashara, niya yao ni kupunguza gharama zao ili kuongeza faida yao.

Hivi kumleta mgeni na kumlipa mshahara mkubwa, na nyumba, na usafiri, na kumpatia kibali.....

Hawa wafanya biashara kweli hawajui biashara, wanakula gharama bure tuu.

Ngoja nianzishe biashara langu. Nitafaidika kweli kweli.
 
Jethro: kumbe unaelewa baadhi ya kazi za idara ya kazi lkn utaki kuzithamini tu; <br />
<br />
unaposema idara ya kazi ni zero ktk kutetea haki za wafanyakazi, siyo SAWA ndugu: zipo standards ambazo zimewekwa na ILO kupitia Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini No 6 ya 2004 ambayo iko wazi kwa @ Mtanzania kwamba mwajiri na mwajiriwa hana haja ya kusema haijui. <br />
<br />
Lkn pia Maafisa wa kazi wamekua wakipita mahala pa kazi na kuelimisha. Kinachobakia ni waajiriwa na vyama vyao vya wafanyakazi(Trade Unions) kulinda kile kilichoainishwa kama haki zao. <br />
<br />
Inapobainika haki hazitendeki kabisa ndo wanashauriwa wapeleke malalamiko/mgogoro kwenye tume ya usuluhishi na uamuzi-CMA kwa ajiri ya utatuzi/ufumbuzi wakisimamiwa na wawakilishi kutoka trade unions siyo tena Watu wa idara ya kazi.<br />
<br />
Kuhusu vibali vya watu wa kigeni kufanya kazi nchini, nendeni Wizara ya Kazi na Ajira au TIC ndo kuna ufumbuzi, kama mnafikiri Uhamiaji kwa vile wanavaa magwanda wana tabia za kipolisipolisi eti ndiyo suluhisho kila siku mtaona wageni wakifanya kazi nchini na wenyeji mkiishia kulalamika tu.<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
.
 
Uhamiaji kazi yao nikutoa vibali vya wageni kuingia nchini na si vinginevyo: kama kuna wageni wanaofanya kazi nchini bila kuwa na vibali vya kufanya nchini, peleka taarifa haraka TIC au Wizara ya Kazi na Ajira kupitia ofisi zao za Idara ya Kazi zilizoko takribani kila mkoa na baadhi ya Wilaya.

TIC na Wizara ya Kazi na Ajira ndiyo wenye mamlaka ya kutoa vibali vya wageni kufanya kazi Nchini.

Tafadhari wenye taarifa madhubuti ziwakilishe panapostaili.
Hapo kwenye red siyo kweli.Wao wanatoa barua ya kuonyesha unavigezo vya kufanyakazi Tz na uhamiaji wanatoa permit.Na permit ni kwa miaka miwili na unarenew kwa miaka miwili basi.Zaidi ya hapo lazima uende kwenu lakini siyo hivyo watu wanakaa mpaka miaka 15.
 
Back
Top Bottom