Wafungwa wa kisiasa kutoka jimbo la Ukerewe washinda rufaa yao na kuachiwa huru

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,263
24,140
28 July 2022
Ukerewe, Mwanza

MAHAKAMA KUU KANDA YA MWANZA KTK KESI No. 171 OF 2021, YAWAACHIA HURU WANACHAMA WA CHADEMA



Waliokuwa wagombea udiwani kupitia chama cha CHADEMA washinda rufaa yao na kuachiwa huru. Mzizi wa Hii kesi ilitokea wakati wa kurudisha fomu za udiwani, walipigwa risasi mwilini na walibabikiwa kesi.

Makamanda hao ni Mateso Mgeta na Alfred Mabagala ambao mbali ya kushinda kesi hiyo walikuwa tayari wametumikia miaka 2 katika ya mitano kabla ya kushinda rufaa yao.

Makamanda hao wa CHADEMA sasa wataenda kukaguliwa afya zao kwani walipata majeraha na vipigo vilivyopelekea kutembelea magongo na walipokuwa jela, mazingira yale yalikuwa magumu kuweza kupata huduma kamilifu za kutibu majeraha yao.

CHADEMA kanda ya Victoria na taifa inaomba wana CHADEMA na waTanzania kwa ujumla kuwaangalia hawa makamanda ili waweze kupata huduma za kiafya baada ya kutoka gerezani na sasa wapo huru.

Jaji wa mahakama kuu kanda ya Mwanza katika uamuzi wake ulio andikwa katika jumla ya kurasa 17 Alfred Mabagala @ Mugeta & Another vs Republic (Criminal Appeal 171 of 2021) [2022] TZHC 10789 (25 July 2022); | Tanzlii na kusomwa mbele ya Mahakama Kuu, alikubaliana na hoja za upande wa utetezi kupiga hukumu ya mahakama ya wilaya ya Ukerewe.

Source : CHADEMA Media TV
 
Soma Hukumu : kamili iliyotolewa na mheshimiwa Jaji M. Mnyukwa wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Tanzania:

IN THE HIGH COURT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MWANZA DISTRICT REGISTRY AT MWANZA CRIMINAL APPEAL No. 171 OF 2021 (Originating from Criminal case No. 46 of 2020 of the District Court of Ukerewe at Nansio before Honourable L.A Nyahega)ALFRED S/OMABAGALA MUGETA AND ANOTHER...........................................-APPELLANTS VERSUS THE REPUBLIC-------------------------------------------RESPONDENT JUDGMENT Last Order: 11.07.2022 Judgment: 25.07.2022 M.MNYUKWA,J. The District Court of Ukerewe at Nansio convicted and sentenced the appellants herein, after they were being found guilty of the 1st count among the three counts which they were charged with, which is the offence of grievous harm contrary to section 225 of the Penal Code, Cap 16 R.E2019. Dissatisfied with conviction and sentence, they have appealed to this court raising three grounds of appealas follows

1.That,the trial magistrate erred in law to the extent that there were procedural irregularities both in proceedings which resulted into convicting the appellants basing on the PF3 tendered by the prosecutor.

2.That, the trial magistrate erred in law and fact by convicting the accused person basing on evidence adduced by the prosecution witnesses which was not sufficient to prove the case beyond reasonable doubt, the required standard.

3.That, the trial magistrate erred in law and fact by convicting the accused person basing on evidence adduced by the prosecution witnesses which was contradicting to each other.

The appellants pray for their appeal to be allowed, conviction and sentence of Ukerewe District Court be set aside and to be released from jail, and any other relief this court may deem just and fit to grant.

At the trial court, the appellants (Alfred Mabagala Mugeta and Mateso Mgeta) were both charged with three counts.

First count being grievous harm contrary to section 225 of the Penal Code Cap 16 R.E 2019, where it was alleged that, the appellants on 25th day of August, 2020 about 10:00hrs at Nyam ......... thebullets. It is not disputed that the 2nd appellant was shot, what is disputed is the circumstance that surrounds his shooting as the evidence shows that, the police officers were also running and it is not clear when did they stop and turn back to save PW1 and shot the 2nd appellant as he wanted to throw another stone. The Court of Appeal in the case of Maulid Hamis Mrisho (supra) it states that: "The law on visual identification is settled before rely in gonit the court should not act on such evidence unless all the possibilities of mistaken identity are eliminated and that the court is satisfied that the evidence before it is absolutely watertight. "Guided by the above decision and in the circumstances of our case at hand, I am not convinced that the appellants were clearly identified as the one who stoned PW1. That being the case I hold that; identification was not water tight taking into consideration the circumstances surrounding the incident. Thus, the identification of the appellants at the trial court was contradictory and therefore the trial court ought not to have acted on such evidence to convict the appellants. On the foregoing I allow this ground and I will not determine the third ground as this ground suffice to dispose the entire appeal. I proceed ......

READ THE FULL JUDGEMENT:

Source : Alfred Mabagala @ Mugeta & Another vs Republic (Criminal Appeal 171 of 2021) [2022] TZHC 10789 (25 July 2022); | Tanzlii

Alfred Mabagala @ Mugeta & Another vs Republic (Criminal Appeal 171 of 2021) [2022] TZHC 10789 (25 July 2022)​

 
28 July 2022
Ukerewe, Mwanza

Waliokuwa wagombea udiwani kupitia chama cha CHADEMA washinda rufaa yao na kuachiwa huru. Hii ilitokea wakati wa kurudisha fomu za udiwani walipigwa risasi mwilini na walibabikiwa kesi.

Makamanda hao ni Mateso Mgeta na Alfred Mabagala ambao mbali ya kushinda kesi hiyo walikuwa tayari wametumikia miaka 2 katika ya mitano kabla ya kushinda rufaa yao.

Makamanda hao wa CHADEMA sasa wataenda kukaguliwa afya zao kwani walipata majeraha na vipigo vilivyopelekea kutembelea magongo na walipokuwa jela, mazingira yale yalikuwa magumu kuweza kupata huduma kamilifu za kutibu majeraha yao.

CHADEMA kanda ya Victoria na taifa inaomba wana CHADEMA na waTanzania kwa ujumla kuwaangalia hawa makamanda ili waweze kupata huduma za kiafya baada ya kutoka gerezani na sasa wapo huru.
Source : chadema media TV
Kila ubaya utalipwa
 
Sio hata kwamba wameshinda rufaa yao, bali walifungwa kwa maagizo ya rais aliyepita kwenye utawala wake wa kidhalimu, na wameachiwa kwa maagizo ya rais huyu kwani anajua kabisa hawakuwa na makosa yoyote zaidi ya kukomolewa.

Kutiwa woga na ukatali. Kwa bahati mbaya mahakama zimekuwa sehemu ya kutekeleza amri za viongozi na sio kutoa haki.
 
Sio hata kwamba wameshinda rufaa yao, bali walifungwa kwa maagizo ya rais aliyepita kwenye utawala wake wa kidhalimu, na wameachiwa kwa maagizo ya rais huyu kwani anajua kabisa hawakuwa na makosa yoyote zaidi ya kukomolewa, kutiwa woga na ukatali. Kwa bahati mbaya mahakama zimekuwa sehemu ya kutekeleza amri za viongozi na sio kutoa haki.
Na yote haya yatakoma baada ya kuwa na Katiba mpya, yenye kutoa haki na huru
 
Tujikumbushe uchaguzi wa 2020 hali ilivyokuwa Ukerewe:

14 Oct 2020 — Uchaguzi 2020 Tundu Lissu amelazimika kuvuka kwa Mtumbwi kuelekea Ukerewe baada ya kuambiwa kuwa kivuko ni kibovu


 
Nchi ilikuwa na watu wenye uvumilivu mkubwa sana 2020.
Kwa kweli CHADEMA mara zote kimekuwa chama kinachoweka maslahi ya watanzania mbele. Kuna wakati unakwenda Polisi halafu unakuta ni mtu wa CHADEMA anawekwa ndani wakati mtenda uovu ni wa CCM.
 
TOKA MAKTABA :

7 May 2021
Dodoma, Tanzania

Serikali imekanusha kuwa na wafungwa wa kisasa na kwamba Rais Samia Suluhu hajaamuru wafungwa wowote watolewe magerezani kama ilivyotangazwa na kituo cha televisheni cha Citizen cha Kenya. Msemaji wa serikali Gerson Msigwa amesisitiza kuwa Tanzania haina wafungwa wa kisiasa na wala hakuna wafungwa wa kisiasa Tanzania bali zipo kesi za makosa ya kijinai yanayoendelea kusikilizwa mahakamani ili haki ipatikane .

Tanzania yakanusha, yasema hakuna wafungwa wa kisiasa



Source : Zanzibar Kamili TV
 
Back
Top Bottom